Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

Pesa watakayoipoteza serikali na mitandao kwa kushuka kwa mauzo ya airtime na charges za miamala ya simu itawarudisha kwenye mstari.
 
Makuwadi wa sheria za kipumbavu utawajua tu...

Hivi mtu unasajili laini kwa fingerprints kitambulisho cha uraia cha kaz gani?

Funga laini funga kila kitu.. its about time.. mateso wanayopata wananchi kwa kitu ambacho si cha lazima sana ipo siku wataelewa maana yake na ku revenge.
 
Sio watu wote wanaochukua vitambulisho vya taifa kwa ajili ya kusajili simu. Unaweza kutumia kutembelea Kenya bila kuwa na passport, kurasimisha kiwanja au kusjili kampuni.
Kinaruhusiwa kweli kwendea Kenya bila passport
 
Na nyie kijani hua mnalalamika?ni mwiko kulalamika we lumumba,endelea kusifu na kuabudu atakuja jiwe kukutetea
Nyumbu mkubwa
Wapi nimeandika mi kijani..? Hizi ndo akili za kuazima
 
Je baada ya kuzuia mikutano ya siasa hawa watu wana hofu ya wananchi kumiliki simu?
Kwamba kampeni zikianza mamilioni ya wananchi watafikiwa kirahisi kupitia hizi simu kwa hiyo inabidi baadhi ya watu haswa wa huko vijijini inabidi wawekwe offline lkwa muda?
Ndio lengo lake huyu ntarahamwe.
 
Hili zoezi ni la kipumbavu haijawahi tokea,wataweka vipi dead line wakati si wananchi wote wana vitambulisho vya Nida?Kupata Kitambulisho chenyewe unaweza hata zimia kwenye foleni.Kwanza sidhani kama kuandikisha line ndo kitu mtanzania anahitaji ili aishi.Mtanzania anahitaji Maji safi na salama,Kazi,huduma bora za jamii kwa ujumla.
 
Sijui kama kumbukumbu zangu zinaniangusha kuhusu hili suala la usajili wa namba za simu. Ninavyokumbuka mimi, awali mwanzoni mwa mwaka 2019 TCRA walitoa ratiba yao ya kuishia Desemba. Serikali ikawakemea kuwa muda walioweka ulikuwa mfupi! Sawa. Tukategemea kuwa mashauriano yatafanyika ili muda uongezwe. Mwezi Novemba, 2019 katika kikao cha mwisho cha Bunge serikali kupitia waziri mwenye dhamana na vitambulisho vya taifa akatoa kauli bungeni kuwa simu hazitazimwa. Wananchi wengi wakapumua. Majuma matatu baada ya kauli ya waziri ikatoka kauli ya Rais kuwa simu zitazimwa kama TRCA walivyopanga lakini kwa hisani yake kama kiongozi mkuu anaongeza siku 20 hadi Januari tarehe 20! Pamoja na kwamba tatizo la msingi ni NIDA kauli hizi za serikali zimewavuruga sana wananchi. Wananchi wengi walikuwa wanasubiri maelekezo kupitia kwenye ofisi zao za mitaa na vitongoji kuhusu vitambulisho au namba za NIDA. Ghafla zoezi likageuka operesheni ya zima moto ambapo wanaacha shughuli zao za kiuchumi na kijamii kuhangaikia kupata namba ya NIDA!. Hapa kuna tatizo kubwa sana la kiuongozi.
 
1.Mtaani wanapita vijana wamachinga na maspika yao, wanatangaza "tunasajili laini kwa alama za vidole".
Wanachomoa vimtambo vyao, wanakuomba kitambulisho wanakusajili. Ni nani anaweza kupreserve integrity ya zoezi?. hivi watu wenye ajenda zao wakiwapa hawa vijana pesa na wakisajili kwa fingerprints za watu wengine zoezi hili umakini wake utakuwaje?

2. Mtandao mmoja mtu anaweza kuwa na laini hadi 5, Je mtu mmoja mwenye kitambulisho akisajili laini kadhaa na kugawa nyingine kwa ndugu, jamaa na marafiki itakuwaje?

3. Huko vijijini interior kabisa hao wanaosajili kwa alama za vidole capacity yao ya kufika huko ndanindani ikoje?

MY TAKE:
Hii nchi ni nchi ya watu masikini sana, kinachosikitisha ni kwamba pale kunapoanza kutokea mwangaza fulani hivi wa sekta fulani kuanza kuchomoza na kushine ili baadae iwe nguzo muhimu ya kiuchumi na kijamii, huwa zinatokea forces fulani kutoka kwa serikali ileile kuanza kuweka regulation ngumungumu zinazorudisha mafanikio ya wananchi nyuma. Kwa mfano:

a) Wananchi walikuwa wameshapiga hatua kubwa kweli kwenye kumiliki TV, kiufupi nyumba za wananchi wengi vijijini na mijini walishaanza kuona TV kama sehemu ya utamaduni wao. Cha ajabu serikali ikaja na mambo ya kuhama Kutoka Analojia kuja Dijitali, na kusababisha kuleta watu wa ving'amuzi kitu kilichopekekea gharama za kumiliki TV kuwa juu, na matokeo yake nyumba nyingi nchini leo hii TV ni anasa!. Watu leo hii imefikia hafua kuangalia Taarifa za habari Bar, au kuangalia mpira wa ligi yao wenyewe kwenye mabanda ya mpira!
Kiufupi base ya wananchi wamiliki TV, imeshrink mno

b) Leo tena baada ya mafanikio ya wananchi mamilioni kwa mamilioni kumiliki laini za simu, serikali ile ile yenye kawaida ya kuvuruga baada ya mambo kuanza kuonekana kukaa kwenye msitari inakuja na reguation juu ya regulation, leo inataka watu wajisajili kwa vitambulisho vya NIDA plus fingerprints, wakati inajua ipasavyo kuwa capacity ya kuprovide vitambulisho hivyo kwa kasi ni ndogo lakini pia uwezo wa kusajili hizo alama za vidole kwa kasi ya kutosha hadi kucover huko vijijini ni mdogo!
Matokeo ya hili zoezi la usajili wa laini ni ama watu wengi watacheat kwa kutokuwa na usajili sahihi au kupelekea upunguaji wa umiliki wa laini za simu, matokeo yake wamiliki simu watapungua kama ilivyotokea kwenye zoezi la TV
kwa kweli hata mimi nina mpango wa kutumia kitambulisho changu kusajili laini za ndugu wa karibu wote ambao hawana no au Id ya Taifa
 
Yaani sisi dah! Kuna kitu kweli tunaweza kukifanya kwa weledi kabisa kabisa kikaenda kitaalamu bila figisu figisu? Kwa nini inakuwa hivi lakini?

Hapa utakuta watu wameiba mpaka basi. Watu weusi sisi tuna matatizo sana wallahi.
 
Tcra wao naona hawana communication nzuri na NIDA!

Watu tulijiandikisha toka mwaka jana, lakini waliopata namba ni wachache, sisi wengine eti tusubirie awamu ya pili!

Walojiandikisha miezi miwili iliyopita wameshapata namba ila sisi wa toka mwaka jana tunaambiwa subiria awamu ijayo. Na bado line zetu wanataka kuzipiga nyundo!?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo ya kusajiri line na kumpatia ndugu asiyeweza kusajiri kutokana na factors mbali mbali nadhani halina shida.

Mfano wazee wetu huko vijijini unaacha kuwasajiria line unadhani watafikiwa lini na nida ili kupata vitambulisho kama hata hapa mjini ni shida.

Ukizingatia ni kupitia simu tunawasiliana na kuwasapoti hao wazee wetu kwa kuwatumia pesa kupitia hizo simu wanazoenda kuwazimia, kesho kutwa kama kweli.
 
Sijui kama kumbukumbu zangu zinaniangusha kuhusu hili suala la usajili wa namba za simu. Ninavyokumbuka mimi, awali mwanzoni mwa mwaka 2019 TCRA walitoa ratiba yao ya kuishia Desemba. Serikali ikawakemea kuwa muda walioweka ulikuwa mfupi! Sawa. Tukategemea kuwa mashauriano yatafanyika ili muda uongezwe. Mwezi Novemba, 2019 katika kikao cha mwisho cha Bunge serikali kupitia waziri mwenye dhamana na vitambulisho vya taifa akatoa kauli bungeni kuwa simu hazitazimwa. Wananchi wengi wakapumua. Majuma matatu baada ya kauli ya waziri ikatoka kauli ya Rais kuwa simu zitazimwa kama TRCA walivyopanga lakini kwa hisani yake kama kiongozi mkuu anaongeza siku 20 hadi Januari tarehe 20! Pamoja na kwamba tatizo la msingi ni NIDA kauli hizi za serikali zimewavuruga sana wananchi. Wananchi wengi walikuwa wanasubiri maelekezo kupitia kwenye ofisi zao za mitaa na vitongoji kuhusu vitambulisho au namba za NIDA. Ghafla zoezi likageuka operesheni ya zima moto ambapo wanaacha shughuli zao za kiuchumi na kijamii kuhangaikia kupata namba ya NIDA!. Hapa kuna tatizo kubwa sana la kiuongozi.
Nchi hii shagalabagala na viongozi wake wote ni shagalabagala
 
Nasikia nyerere aliwahi kushauri rais asitoke usukumani sijui nani alimpendekeza huyu mchattle
 
Hii nchi kila kitu ni vululuvululu

Hakuna kitu kinachofanywa nchi hii kikanyooka, kiasi kwamba mtu ukasema naam hapa kuna weledi makini unetumika hapa.

Kuandaa mazoezi na operesheni mbalimbali za kijamii, kiichumi na kisiasa inahitajika vichwa makini vilivyotulia kuyaaandaa, siyo kukurupuka tu
 
Back
Top Bottom