Kuelekea mchezo wa Taifa Stars dhidi ya Harambee Stars AFCON2019, Nchi gani Kung'ara?

Kuelekea mchezo wa Taifa Stars dhidi ya Harambee Stars AFCON2019, Nchi gani Kung'ara?

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars leo kinaingia Uwanjani kuwakabili timu ya Taifa ya Kenya Harambee Stars katika mfululizo wa michuano ya fainali ya mataifa ya Afrika AFCON2019, utakaopigwa leo Juni 27, 2019 saa 5:00 majira ya usiku Cairo, Misri.

Taifa Stars imetamba kucheza kufa na kupona ili kuweza kushinda mchezo huo wa kundi C na kuweza kufuzu hatua inayofuata huku Rais wa TFF Wallace Karia akiwatia moyo wale ambao wamekata tamaa baada ya Taifa Stars kufungwa na Senegal.

Kocha wa Taifa Stars Emmanuel Amunike, amesema anatambua umuhimu wa mchezo huo, huku akiongeza kuwa lazima ashinde ili matumaini yao ya kusonga mbele yasalie hai.

Harambee Stars wamekiri mchezo si rahisi mchezo itakuwa ngumu, lakini wametaja kuwa mchezo wao dhidi ya Taifa Stars kuwa ni fainali kwao ambayo inawapa fursa ya kipekee kushinda.

Kocha wa Harambee Stars, Sebastien Migne, amesema kwamba kupoteza mchezo wa ufunguzi dhidi ya Algeria iliiweka timu yake pabaya hivyo amewataka vijana wake kuonyesha ukatili wao dimbani kwenye mechi na Taifa Stars.

••••Je? Wajeruhiwa Wawili wa Mechi Zao za Ufunguzi wa Michuano ya AFCON2019..Nchi gani Kung'ara? Tanzania ama Kenya?
FB_IMG_1561612783139.jpeg
 
Hivi tunawapiga mangapi leo hawa jirani zetu Wakenya...!

Kila la heri Taifa Stars..Kanyaga Kanyaga..!
 
Kama kweli wabongo kauli ya jagwa imewauma basis wafungeni Kenya leo
 
Kama kweli wabongo kauli ya jagwa imewauma basis wafungeni Kenya leo
Ile ilikuwa kauli au maoni yake binafsi na siyo kauli ya Serikali ya Kenya..! Leo ni Fainali ambayo ambayo haina uhusiano na yule Jagwa.
 
Ile ilikuwa kauli au maoni yake binafsi na siyo kauli ya Serikali ya Kenya..! Leo ni Fainali ambayo ambayo haina uhusiano na yule Jagwa.
wakenya wangefanya kweli ingekuwa ni kauli ya nani
 
wakenya wangefanya kweli ingekuwa ni kauli ya nani
Tunajadili jambo ambalo halipo kwa Serikali ni kupoteza muda, narudia tena ile ilikuwa kauli yake binafsi

Jaguar amefanya Xenophobia asili ya tabia ya Kikaburu hiyo.
 
Itokee Bahati tushinde lakini wakenya wametuzidi kidogo..... Na ndiyo maaana miaka miwili mfululizo wananyakua kombe la sportipesa mikononi mwetu na timu zao zinapata fursa kucheza na everton...
 
Hata Taifa stars wakifungwa waonyeshe viwango. .Manula ataenda Ulaya kama kipa wa Cameroon (Ajax Amsterdam )
 
Itokee Bahati tushinde lakini wakenya wametuzidi kidogo..... Na ndiyo maaana miaka miwili mfululizo wananyakua kombe la sportipesa mikononi mwetu na timu zao zinapata fursa kucheza na everton...
Sio kweli. .timu ya Kenya kucheza robo fainali ya CAF Champions League mara ya mwisho ilikuwa lini? ??
 
Back
Top Bottom