Kuelekea mechi ya VPL' Kariakoo Derby | Yanga SC na Simba SC, Huku Pira Biriani kule Pira Gimbi

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Naaaam!

Kuelekea patashika ya Ligi Kuu Tanzania Vodacom Premier League VPL, Jumamosi November 7 2020 kutavurumishwa mchezo wa watani wa Jadi katika soka la Tanzania kati ya Yanga SC dhidi ya Simba SC

Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana
Wekundu wa Msimbazi Mabingwa wa Nchi, Simba SC klabu kubwa na bora Afrika, ambayo imekuwa ikitoa burudani uwanjani kwa soka la Pira Biriani pamoja na ushindi mnono, wapo tayari kabisa wakiwa wamejiandaa vilivyo kukutana na Yanga SC ambayo haijawa bora kutokana namna ambayo wanapata ushindi dhaifu kabisa kwenye Ligi Kuu Tanzania VPL, ushindi ambao umekuwa ukiwapa tumbo joto mashabiki wao.

Katika mchezo huo Simba SC kuhakikisha inawavuruga kabisa Wanajangwani, itaingia na mbinu ya kumiliki sana mpira uwanjani kama ilivyo asili ya Wanalunyasi, ambapo itawachukua takriban dakika 1-3-4 wakimiliki mpira hali itakayopelekea Yanga kupoteana uwanjani hatimaye kujikuta wakifungwa huku wakishangaa wasiamini kinachotokea.

Wanasimba na mdau wa soka popote pale shuhudia kabumbu lenye ushawishi kutoka kwa Simba SC lililothibitishwa na Shirikisho la Soka Barani Afrika CAF kutoka kwa Wekundu wa Msimbazi Mabingwa wa Nchi.

Tukutane kwa Mkapa. Zuio kipigo kama unaweza.
 
Mnyama anakufa kesho, hapa Tuisila pale mkukoko tunombe wanatokaje wanatokaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…