Kuelekea Mei Mosi, Walimu tunaomba Rais Samia Suluhu uunde tume ya kuichunguza CWT

Kuelekea Mei Mosi, Walimu tunaomba Rais Samia Suluhu uunde tume ya kuichunguza CWT

Jensen salamone

JF-Expert Member
Joined
Sep 28, 2019
Posts
320
Reaction score
641
Zikiwa zimesalia siku chache kuelekea kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi(mei mosi), walimu tunakuomba mheshimiwa Rais uunde tume ya elimu kukichunguza chama cha walimu (CWT) kwakuwa kimeshindwa kutimiza wajibu wake wa kututetea na kutuhudumia.

Mbali na kushindwa kutimiza wajibu wake wa msingi wa kutulinda na kututetea, chama hiki ni mwiba kwa walimu kwani kimejaa uozo na uzandiki wa kila aina. Miongoni mwa uozo huo ni pamoja na haya yafuatayo:

CWT kinafanya biashara kupitia kampuni ya TEACHERS DEVELOPMENT COMPANY LIMITED ambayo inaendeshwa kwa michango yetu wanayotukana kila mwezi lakini faida inayopatikana kupitia kampuni hiyo hatujui inamnufaisha nani.

CWT wanatukata pesa ya kuchangia mfuko kila mwezi wakati vyama vya watumishi wengine vinachukua michango kwa mwaka.

CWT kupitia michango wanayotukata kila mwezi wamejenga benki ya mwalimu (MCB) lakini sisi kama wanachama ambao tulipaswa tuwe wanufaika wa kwanza hatuelewi chochote kuhusu benki hiyo wala mapato yanayopatikana huko hatuelewi yanakoelekea.

Kila mwezi walimu tunakatwa kuchangia hiki chama lakini uwazi na matumizi ya pesa tunazochangia hakuna na hivyo sisi kama walimu tuna wasi wasi kwamba huenda michango tunayokatwa inaishia kwenye mifuko ya wachache.

CWT kupitia michango wanayotukata kila mwezi, wametengeneza vitega uchumi karibia kila mkoa ikiwemo mwalimu house lakini sisi kama wachangiaji hivi vitega uchumi havitunufaishi kwa chochote.

CWT pamoja na kwamba tunawafikishia vilio vyetu huwa hawatusikilizi na mbaya zaidi wametunyima uhuru wa kufanya vikao kwenye vituo vyetu vya kazi kujadiliana shida mbali mbali zinazotuandama.

Wito wetu kwako mheshimiwa Rais
Tunakuomba uunde tume ya kukichunguza hiki chama na tuhuma zote zinazokikabili ili utusaidie kututua huu mzigo mzito tuliotwishwa na watu wasiotutakia mema sisi walimu.

Mheshimiwa Rais, sisi kama walimu tunaomba tukutoe wasi wasi kwamba hautakuwa wa kwanza kukifuta hiki chama. Kwani uamuzi kama huu uliwahi kufanywa na mwl Nyerere mwaka 1982. Katika kuweka kumbukumbu sawa naomba nikukumbushe kidogo ilivyokuwa.

Katika miaka ya 80 kuliibuka na vilio kama tulivyonavyo sisi walimu leo. Sasa baada ya madai na malalamiko ya walimu kuwa mengi, Rais Nyerere aliunda tume maalum ya elimu kuchunguza madai hayo.

Tume ilipofanya uchunguzi ilibaini kuwa Unified Teachers Service(UTS) ambacho kilikuwa ndicho chama cha walimu kwa wakati huo kwamba kilishindwa kuwahudumia walimu kikamilifu, hivyo tume ikapendekeza kuundwa kwa chama kingine kitakachohudumia na kuwatetea walimu ndipo Rais Nyerere akakivunja na chama kingine kikaundwa.
 
Mnamtuma mkuu wa serikali ambayo inakiua chama chenu?
Achunguze na kukiweka sawa, muelimike ili msiwaibie kura2025?
Ninyi mandondocha yao, mnafanya kila wanachotaka kwenye chaguzi. Wakuu wenu wanakula tu.
Mwende mkatambike kwenye mbuyu
Mkuu...!

Bandiko lako linaonyesha ni kwa kiasi gani una chuki dhidi ya walimu...!

Lakini nachokuomba uwe siriasi kidogo kwenye mambo nyeti kama haya maana yanagusa maisha ya watu na kama wewe hayakugusi pita kimya kimya sio unaandika rubbish...!!
 
ninyi c ndo wale wa kura zote kwa ccm na cwt ndo mpaka kinagawia fedha sirikali na cwt kumejaa makada wa chama.cwt ni maficho ya makada chipukizi wa chama. TULIENI TU KIMYAA mnyolewe!
kada wa Mkuu...!

Bandiko lako linaonyesha ni kwa kiasi gani una chuki dhidi ya walimu...!

Lakini nachokuomba uwe siriasi kidogo kwenye mambo nyeti kama haya maana yanagusa maisha ya watu na kama wewe hayakugusi pita kimya kimya sio unaandika rubbish...!!
 
ninyi c ndo wale wa kura zote kwa ccm na cwt ndo mpaka kinagawia fedha sirikali na cwt kumejaa makada wa chama.cwt ni maficho ya makada chipukizi wa chama. TULIENI TU KIMYAA mnyolewe!
Siasa na mambo ya uchaguzi vinaingiaje hapa kama sio kutaka kupotosha maudhui ya msingi ya huu uzi...??
 
Nakuunga mkono kwa asilimia zote mkuu. Chama cha walimu ni mojawapo ya mizigo inayowatinga walimu na kuwaongezea ugumu wa kazi na maisha. Chama hiki kimekuwa chaka la kuficha makada wa CCM wanaosaidia kuhujumu masilahi ya walimu kupitia serikali yao ya kidhalimu.
 
Zikiwa zimesalia siku chache kuelekea kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi(mei mosi), walimu tunakuomba mheshimiwa Rais uunde tume ya elimu kukichunguza chama cha walimu (CWT) kwakuwa kimeshindwa kutimiza wajibu wake wa kututetea na kutuhudumia.

Mbali na kushindwa kutimiza wajibu wake wa msingi wa kutulinda na kututetea, chama hiki ni mwiba kwa walimu kwani kimejaa uozo na uzandiki wa kila aina. Miongoni mwa uozo huo ni pamoja na haya yafuatayo:

CWT kinafanya biashara kupitia kampuni ya TEACHERS DEVELOPMENT COMPANY LIMITED ambayo inaendeshwa kwa michango yetu wanayotukana kila mwezi lakini faida inayopatikana kupitia kampuni hiyo hatujui inamnufaisha nani.

CWT wanatukata pesa ya kuchangia mfuko kila mwezi wakati vyama vya watumishi wengine vinachukua michango kwa mwaka.

CWT kupitia michango wanayotukata kila mwezi wamejenga benki ya mwalimu (MCB) lakini sisi kama wanachama ambao tulipaswa tuwe wanufaika wa kwanza hatuelewi chochote kuhusu benki hiyo wala mapato yanayopatikana huko hatuelewi yanakoelekea.

Kila mwezi walimu tunakatwa kuchangia hiki chama lakini uwazi na matumizi ya pesa tunazochangia hakuna na hivyo sisi kama walimu tuna wasi wasi kwamba huenda michango tunayokatwa inaishia kwenye mifuko ya wachache.

CWT kupitia michango wanayotukata kila mwezi, wametengeneza vitega uchumi karibia kila mkoa ikiwemo mwalimu house lakini sisi kama wachangiaji hivi vitega uchumi havitunufaishi kwa chochote.

CWT pamoja na kwamba tunawafikishia vilio vyetu huwa hawatusikilizi na mbaya zaidi wametunyima uhuru wa kufanya vikao kwenye vituo vyetu vya kazi kujadiliana shida mbali mbali zinazotuandama.

Wito wetu kwako mheshimiwa Rais
Tunakuomba uunde tume ya kukichunguza hiki chama na tuhuma zote zinazokikabili ili utusaidie kututua huu mzigo mzito tuliotwishwa na watu wasiotutakia mema sisi walimu.

Mheshimiwa Rais, sisi kama walimu tunaomba tukutoe wasi wasi kwamba hautakuwa wa kwanza kukifuta hiki chama. Kwani uamuzi kama huu uliwahi kufanywa na mwl Nyerere mwaka 1982. Katika kuweka kumbukumbu sawa naomba nikukumbushe kidogo ilivyokuwa.

Katika miaka ya 80 kuliibuka na vilio kama tulivyonavyo sisi walimu leo. Sasa baada ya madai na malalamiko ya walimu kuwa mengi, Rais Nyerere aliunda tume maalum ya elimu kuchunguza madai hayo.

Tume ilipofanya uchunguzi ilibaini kuwa Unified Teachers Service(UTS) ambacho kilikuwa ndicho chama cha walimu kwa wakati huo kwamba kilishindwa kuwahudumia walimu kikamilifu, hivyo tume ikapendekeza kuundwa kwa chama kingine kitakachohudumia na kuwatetea walimu ndipo Rais Nyerere akakivunja na chama kingine kikaundwa.
Laiti walimu mngeacha kutumika kama toilet paper ningesoma huu Uzi wote ila kiukweli tunawaheshimu sana walimu lakini hamtuheshimu kabisa. Nyie mnachojua ni kutumika kila uchaguzi.
 
Hivi walimu mlishaomba radhi kwa kubariki mambo kama haya?
2599060_IMG_20201023_124952.jpg
 
Tume mbona ilishaundwa na ilichunguzwa na cag ripoti zikatplewa sema mnatakiwa kudai utekelezaji wa hiyo ripoti maana kuna madudu mengi yalibainika
 
Kuna rafiki yangu Arusha ananiambia wao hata T shirt hawajapata.
 
Kwan lazima kujiunga
Bora hata wewe umeingia kwa namna nzuri kuliko wale wanaokurupuka.

Jamaa wa Msovero kwa kukujibu swali lako tu ni kwamba kujiunga ni hiari (si lazima) indirectly ila pia kujiunga ni lazima (si hiari) directly

Ukijiunga (kwa kuthibitisha mwenyewe) basi utakatwa asilimia 2 na utakuwa unapewa kapelo na tisheti kila mwaka. Pia majanga ya kesi kubwakubwa wanakusaidia saidia kisheria

Lakini

Usipojiunga (kwa kukataa kujithibitisha) basi hutaona tisheti wala kofia wala nini... cha kusikitisha ni kwamba ile asilimia mbili ipo palepale kwahiyo utakatwa kama kawa kama dawa (as usual as normal)

Baada ya hapo niingie kwenye hoja...
Kilio hiki naungana nacho japo nitakuwa tofauti kidogo.

Serikali ina vyombo vyake ambavyo inavitumia kuwakamua (ni hivyo hivyo kuwakamua na wala siyo kuwakwamua) wananchi wake kwa kigezo cha (madai ya) maendeleo

Vyombo hivyo vipo kila sekta (taasisi) na vinaact kuwa pamoja na wananchi katika taasisi hizo ila ikitokea wananchi wanamaindi sana basi sasa ndiyo serikali itafanya kuingilia kati kwa jili ya kupooza na wakati huo ikiandaa (au pengine imeshaandaa) namna ya kuwazunguka tena

Nitatoa mifano hapa
1.CCM
2.CHADEMA
(samahani watu wa siasa)
3.BAKWATA
4.CWT
 
Walimu mnajiona ndio watumishi pekeenu kwenye nchi hii
 
Back
Top Bottom