Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
Chadema , badala ya kuanza kufarakana , mngeaanza kujipanga kuongeza idadi ya ya wabunge . Muda uliyobaki siyo mrefu. Tazameni na angalieni ni majimbo gani mna possibility ya kuleta opposition kali (mfano siyo kusimamisha mgombea against Nimrod Mkono).
Mkiaanza kuleta makundi sasa hivi , hata wakati wa uchaguzi hamtasaidiana. Mfano mzuri ni NCCR. Kwa mawazo yangu, haya makundi ni ya kujipanga kufaidi/kugawana ruzuku/donations/misaada ya Chama.
Mkifarakana , hata hizo za fedha hamtapata. Idadi ya wabunge itapungua na hasa zaidi heshima ya chama.
Umoja ni Nguvu
 
Mimi naona Zitto anatuchanganya tusubiri mkurugenzi wa Uchaguzi aliyesimamia atoe tamko vinginevyo nikutaka kulikologa na jazba za siasa!
 
Zitto pole sana nakuambia tu move foward kuwatetea wananchi ukiwa humo humo chadema
 
Nakuunga mkono mkuu .Kuna wabaya ambao wanaleta shida kwenye Chama na wanaleta issues kati ya Zitto na Chadema .

Kweli mkuu Lunyungu naona baada ya uchaguzi CHADEMA wanatakiwa kufanya ukarabati mkubwa ndani ya chama maana imesha jihidhilisha wazi kuna watu pale CHADEMA wapo kwa ajili ya matumbo yao na si kichama na mshikamano maana majungu,fitna na chuki wanazo zijenga ni hatari sana kwa muhimili wa chama wanaweza kujikuta chama kinameguka na kuwa na pande 2 kwakweli wazee inatakiwa wawe makini na hili ni bora wale wanachama ambao wanatishia uhai wa chama kwa kupika majungu wakaitwa na kupewa onyo kali haswa hawa akina Mnyika na Mrema na wengineo maana muda si mrefu wanaweza wakajikuta wametengeza kambi 2 hatari kumbuka tunaelekea uchaguzi mkuu sasa kukiwa na kambi 2 maana muungano na mshikamano hauta kuwepo endapo chama kitaendelea kuruhusu majungu na fitna ziiendelee ndani ya chama. Kinacho takiwa nikukemea ikiwezekana kufukuza kabisa hao wanachama njaa na uchwala.
 
Masikini Tanzania, mategemeo yote sasa yanakaribia sifuri. Mafisadi, anzeni kujipanga tena upya kwani sasa ni nafasi kwenu kujineemesha nyie na muwapendao. Bila shaka sasa mtakuwa na nafasi ya kufungua account hadi japani, kwani hakuna tena wa kuwaulizeni. NEC imewafunga midomo kina Sitta et. al., wakati nao kina Mbowe na Zitto wameamua kijimaliza wenyewe.

Maskini Tanzania uliyejaliwa kila kilicho chema na muumba, simuoni wa kukuokoa. Inasikitisha na kukatisha tamaa sana.
 
zitto kuja kutoa majibu hapa hujasaidia, ulichofanya ni kuonyesha chadema imeoza kiasi gani na ina ukosefu wa demokrasia tu.

Umejitoa kugombea uenyekiti ili kuunda umoja wa chama, hichi ulokiandika hapa ni kuvuruga chama na kutoa siri za ndani nje (masuala ya ukaguzi wa pesa wa CAG)

Itabidi uniwie radhi mheshimiwa, lakini katika huu mtafaruku uliojitokeza chadema na wewe ume play ur part tena kubwa mno.
 
Kuna wat nawajua kwa tabia pale Chadema ambao wako open sana sana .Kafulia Oops Kafulila anajua kwa nini yuko Chedama mara nyingi nimesema naye , Kitila uwezo wake na uwazi wake , Zitto , Mtemelwa .Chadema kwa wenye majungu kwa Mtemelwa watachoka .I know the man long time ago hakika hataki mambo ya gizani .Nina wasi wasi na baadhi ya vijana pale .Kazi hii Mbowe utalazimishwa kuchukua uamuzi mto na mchungu lakini lazima ufanye mageuzi chama chetu .Kilianzishwa na wachache kwa kubezwa na wananchi wengi lakini leo Chama kinakuwa na nimekuwa Chama chetu na wala si chenu tena .

Imani kwa Chadema bado kubwa , mitikisiko ni kawaida ila majungu haya hao wenye nayo waende kwa Mrema anawafaa hakika .Kijana lazima awe focussed na si kuendeleza majungu na chuki.Siasa hizo ni siasa njaa .

Mbowe pangua sasa kurugenzi hizo zikamatwe na watu wapya ndiyo heshima ya Chama bwana .Yes there is nothing for life .Muda ni huu and let others learn as well .
 
Baada ya kumlazimisha zitto asigombee uenyekiti wa CHADEMA bila sababu za msingi eti chama kitapasuka..
leo hii WAZEE hao hao wametoa mpya kwa kuufuta uchaguzi wa baraza la vijana la CHADEMA (BAVICHA)
sasa ndugu zangu hawa wazee ndio katiba yao au?
kama hari ikiendelea kuwa hivi,hii ni hatari sana kwa ukuaji wa mageuzi nchini

tarehe yako ya kujiunga na data unazotoa na wasiwasi nawewe si mtu mwema hatakidogo!!ni mvurugaji may be we sio kingunge ngombale mwiru wewe?au hajakutuma?wana JF jihadharini na huyu mtu hana la maana
 
Kwanza Pole Mh. Zitto kwa kashikashi zote hizo,

Hivi ukiwa kama Kiongozi Mkuu kwenye Ukatibu Mkuu Makamu hivi huoni kuwa umeingilia huo uchaguzi kwa kusema wewe mwenyewe kuwa ulifanya kampeni wazi wazi kwa vijana hawa wadogo huoni kuwa ukutenda kosa??

Mh Zitto! kwenye kipindi kama hiki kizito kwa chama kwanini usiwe na moyo kama wa mwenyekiti wako Mbowe ukakaa kimya kwa masrahi ya chama kwanza, unapoanza kusema mambo ya Fedha (CAG) huoni kuwa hapo kuna mushkeli,

Pia kuja hapa kwenye JF forum kumwaga razi lote hilo ambalo kuna utitiri wa wanaCCM kibao, huoni kuwa unavujisha siri??

Mimi sina chama ila picha unayoonyesha ni ile ya mapindikizi ya CCM tuliyozoea kuona!!!

Wewe sema tu unachangia whether una chama au la siyo la muhimu hapa. Yawezekana una chama sisi tutajuaje!!
 
mh,mimi chokaa kabisa,CHADEMA?mwenyekiti MBOWE huyu mmemuweka agombee upresident?hivi mko serious na hayo mageuzi?mbowe mimi simkubali hata kwa virungu kwanza ni dikteta waulize waliofanya nae kazi pale club,na ana historia chafu sana hata yeye anajijua leo iweje agombee urais?pili yeye,baba mkwe wake,wajomba na wanafamilia wao ndio viongozi wa hicho chama,haya na leo napata kali zaidi zitto nae na mamaake ndani,hiki chama nadhani ni saccos kama nnavyokumbuka kuna mtu alisema humu,na angalia sasa nilianza kushawishika kama zitto angegombea uenyekiti nimpe kura yangu lakini sasa mmh!inabidi nijikalie tuu niendelee na shida zangu bongo hakuna mageuzi wala demokrasia,nyie endeleeni na majungu wenzenu nyumba ya pili wanachekelea tu,kwani mvurugano wenu ndo unaowapa wao uhakika wa kututawala maisha.chao

Du!! ahaa ahaa leo nimeifaidi JF kweli!! sina mbavu!
 
Masikini Tanzania, mategemeo yote sasa yanakaribia sifuri. Mafisadi, anzeni kujipanga tena upya kwani sasa ni nafasi kwenu kujineemesha nyie na muwapendao. Bila shaka sasa mtakuwa na nafasi ya kufungua account hadi japani, kwani hakuna tena wa kuwaulizeni. NEC imewafunga midomo kina Sitta et. al., wakati nao kina Mbowe na Zitto wameamua kijimaliza wenyewe.

Maskini Tanzania uliyejaliwa kila kilicho chema na muumba, simuoni wa kukuokoa. Inasikitisha na kukatisha tamaa sana.


Pole sana ndugu yangu. Naelewa feelings zako na za wengine humu ndani. Ninawahakikishia kuwa tutainuka, tutajipakusa vumbi na kukimbia tena pamoja. Mchakato huu waweza kuwa na matokeo ya kukikuza na kukikomaza chama sana. Tunajifunza katika changamoto hizi. Hatuwezi kukubali kuingia katika historia ya kuua CHADEMA. Kuna masuala fulani fulani ya msingi kabisa kuhusu mahusiano yetu na marafiki zetu ambayo lazima tuyashughulikie asap.

Deep in my heart i believe truth will prevail and the party will come up strong.
 
This is part of spinning. Uwongo, uzushi nk. Tatizo wanaopanga haya wanasahau kuwa tuliyapanga wote dhidi ya marehemu Chacha Wangwe. Unatengeneza uwongo, unausambaza, na hatimaye wewe mwenyewe unauamini kuwa ni kweli.

Kama kuna kitu kilimuuma marehemu wangwe na alikufa nacho ni kile cha kumsema kuwa alikuwa anatumiwa na mafisadi. Namshukuru Mungu kuwa nilimwomba radhi Chacha kabla na baada ya kifo chake siku ya postmorterm kwa kumzushia uwongo.

Asha ni mmoja wa wenzangu tulioshiriki kumtenda Chacha. Wanatumia mtindo ule ule na wanapita njia zile zile. Rashidi wa Kuli alisema, YANA MWISHO HAYA!

Asha, (ninakujua wewe ni nani) kuwa mkweli wa nafsi yako! Utalipwa hapa hapa duniani kwa uzushi wako na wenzako.

To put record clear - Kasisiko sio ndugu yangu wa damu. Ni mwenyekiti wangu tu wa Mkoa Kigoma. Pili, Baregu hajahudhuria kikao hata kimoja cha wazee toka ajue ukweli wa mambo.
Tatu, chama jana kimechagua rasmi Baraza la Wazee na mgombea aliyekuwa ananiunga mkono waziwazi ameshinda. Inakuwaje bado vikao vya wazee vya chama vinaendeshwa na Mtei na Ndesamburo?

Pili, vyombo vyote vya habari vilikuwapo katika hotuba ya Mtei. Imekuwaje NIPASHE peke yake ndio ione alisema kuna ufisadi kwenye chaguzi za chama? Mhariri mtendaji wa Nipashe ni jesse kwayu kutoka Machame. Mmiliki wa Nipashe ni Reginald Mengi kutoka Machame.

Spinns sio sustainable. Acheni tujenge chama chetu.
Mkuu Zitto, hakika hii inakuondolea sifa ya Kugombea Uenyekiti automatic yaani hufai!..maelezo yako ni dhahiri yanaonyesha wazi huna Hekima wala Busara kuongoza chama, kifupi hujakomaa kisiasa kabisaaa. Una papara, mwenye hasira na mwepesi kuropoka..Mkuu hukutakiwa kabisa kubwabwaja ovyo hapa kijiweni maneno haya kwani yanazidi kukufunga wewe ikiwa umeshakubali kujitoa ktk kugombea.

Maneno haya yalitakiwa kutangulia na hasa siku ya kikao cha chama. Na nakuomba sana ktk mkutano mkuu wa chama hii September, zungumza yote yaliyoko moyoni mwako, kuwa muwazi, mkweli na bayana tuhoji utendaji kazi wa hao wazee ama watu ambao unawafahamu kuhusika na mbinu hizi chafu za kupakaza.

Kulitumia jina la wangwe na uchafu wote mlofanya dhidi yake hakika umenichefua kichizi yaani kumbe kweli Zitto mlimfanyia Wangwe roho mbaya makusudi?..Hukuona ubaya wa kutenda ulotenda Ukajisafisha hadharani hadi siku ambayo umetendewa wewe ndipo unakuja na habari hizi za Wangwe tena ktk gazeti!..

Well itakuwa vizuri ukimalizia kabisa kutufahamisha maanake hakuna kitu ambacho sisi wananchi tunataka kuelewa zaidi ya Kifo CHA WANGWE kama kuna mkono wa mtu..Ikiwa wewe mkweli na unataka tukuamini basi tueleze yote mlomtendea Marehemu Wangwe ambayo wewe mwenyewe unakiri na ulikwenda simama mbele ya maiti na Kutubu..What real happen? wewe mwenyewe pamoja na Bi Asha ,mlifanya nini au mlicheza part gani mkuu come clean leo hii hapa hapa JF.

Duh, ama kweli mkuu wangu najua ulikuwa na haki ya kugombea kiti hicho lakini leo hii na maelezo haya yaonyesha wazi kwamba hufai kabisa... Na wala usije fikiria kuwa Wangwe alikuwa mtu mzuri vile vile..ila kwa walalahoi wasojua kwamba a sneetch ni Liability ktk taasisi yoyote na hafai kabisa..isipokuwa kwetu sisi Ndivyo Tulivyo (Watumwa wa akili), kumbe ktk jumuiya kama zetu nchi za nje watu hawa hamalizwa vibaya vibaya na hawapokelewi mahala popote.

Kifupi Zitto hakuna sifa hata kidogo unapokipaka chama chako na sidhani hata ukiondoka ama kwenda chama chochote utapokelewa kwa mikono miwili, laa utatumiwa tu na hakuna mtu wala chama kitakachokuamini. Watu kama Wangwe na wewe ni wa kuogopwa na kukaliwa mbali sana na sii kwa sababu unasema ukweli wako ila Mropokaji ni Liabiility ktk chama..Usifikirie unajenga mkuu wangu yaani duh! ama kweli Umri ni moja ya kigezo kikubwa sana ktk CV ya mtu..
 
Last edited:
yale yale!

politics za Tanzania ni kama vichekesho vya "Mr Bean"

tunafaidi nini kwa Mh Zitto "kumwaga radhi"? kwa mtizamo wangu Zitto anajaribu kuelezea "hisia" zake baada ya "kushawishiwa" kujitoa ugombe "Uenyekiti" BILA RIDHAA yake!

kwanini amekubali kujitoa, hiyo tutajua mbele ya safari (for sure)!

katika mwendelezo huo huo ameamua kumpigia kampeni "waziwazi" Kafulila ila angalau apata aueni baada ya "machungu" ya "kulazimishwa" kutogombea uenyekiti wa CHADEMA.

Ni lini itafika nchi hii itakapokuwa na "wananchi"? Kwa mtizamo wangu wa-Tz naona tunaendesha mambo kama vile tupo njiani/safarini kwenda kuishi kwenye "nchi" nyingine.

Sikuweza kufikiri kuwa hadi kufikia uchaguzi wa 2010 Tanzania itakuwa na chama kimoja cha siasa! Kila kukicha vyama vya "siasa" vinazidi kudhoofu (CD4 count inapungua dramatically) na Chama tawala kinazidi kunawili!

Aaaaaaaaaaaahg! You can take an African from the Bush....
 
Mkuu Zitto, hakika hii inakuondolea sifa ya Kugombea Uenyekiti automatic yaani hufai!..maelezo yako ni dhahiri yanaonyesha wazi huna Hekima wala Busara kuongoza chama, kifupi hujakomaa kisiasa kabisaaa. Una papara, mwenye hasira na mwepesi kuropoka..Mkuu hukutakiwa kabisa kubwabwaja ovyo hapa kijiweni maneno haya kwani yanazidi kukufunga wewe ikiwa umeshakubali kujitoa ktk kugombea.
Kwangu network imekatika katika ubongo... Sielewi nini kinaendelea mkuu Mkandara!
 
Mimi sichukulii kinachotokea CHADEMA kama ni mpasuko, vituko vyote, vitimbi, kuteteana , majungu, fitina na kupigiana debe ni sehemu ya UCHAGUZI na DEMOKRASIA. Kila chama duniani inapofika wakati wa uchaguzi hali inakuwa kama hii iliyotokea CHADEMA sasa hivi. CHADEMA will emerge even stronger as a result of this process.
 
Mimi niliweka wazi msimamo wangu wa kumwunga mkono kafulila. Wakurugenzi wa Makao makuu ya chama kuanzia Katibu Mkuu mpaka wakurugenzi kama John Mnyika, John Mrema na hata maafisa kama Halima Mdee

Mhe Zitto, hapa ndo maana nikasema wewe kwa uenyekiti bado. Hasa hapo nilipobold. Nafikiri unafahamu vema nafasi yake kwenye jamii ilihali si zaidi ya CHADEMA. Go slowly, akifyatuka wataamini kuwa wewe ndo chanzo cha matatizo na no body will help you. We still need you na tutaendelea kukuunga mkono japo si kwa yote.
Hawa wanaogopa uwezo wa Kafulila wa kukataa kutumika na kuwa independent katika maamuzi yake.

Ukiwa kiongozi lazima utumike, and you can not be independent Zitto. Amua basi kuwa mwanachama wa kawaida. Naheshimu uliwashukuru akina Chenge simply kwa kuwatumikia wanakigoma BUT sio mimi. Mimi huku namuangalia Maghufuli brother. Unapokuwa kiongozi lazima ukubali kutumika na wengi wape kama kuna manufaa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom