Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
Kweli Mkuu, CHADEMA wameharibu mambo kweli kweli safari hii, ila tuelekezane kidogo hapo Mkubwa: Obama hakusema tujifunze kuwekeza kwenye "siasa safi." Obama alisema tuwekeze kwenye kujenga "taasisi imara."

Akimaanisha - na aliorodhesha na kuanisha anachomaanisha - mabunge huru, vyombo vya dola vilivyo safi (polisi wasiokula rushwa, akatoa mfano), mahakama na vyombo vya habari huru, asasi za kiraia zenye nguvu; kifupi taasisi zilizojengwa katika misingi ya, na zinazodumisha, demokrasia.

Kinachofanyika CHADEMA kwa sasa sio kwamba ni kuwekeza katika watu, bali kinaweza kuwa ndio hiyo struggle ya kujenga taasisi za kidemokrasia. Dr. Slaa (Mb.) anapobatilisha matokeo ya uchaguzi, Zitto K. (Mb) anamwambia mbona ni Kamati Kuu ndio ina mamlaka hayo na si wewe? Mbona katibu umejiamulia kutotangaza matokeo kivyako, kwani katiba inasemaje? Kwa hiyo Zitto yuko sawa kwa hilo ( japo anakosea anapolumbana na kunyosheana vidole na wenzake bila tact, akiwemo mwenyekiti wake) alichojaribu kukifanya kinaendana na alivyoshauri rais wa Marekani akiwa Accra, tuwekeze kwenye misingi ya taasisi za kidemokrasia, kufuata utawala wa sheria, Katiba, sio fikra za Katibu wala "siasa safi" za mwenyekiti!
Inapaswa kuwa makini sana katika wakati huu na pia sioni sababu ya kufanya hivi mambo kama haya bwana. lakini yote lazima watu tuyajue na tuchukue hatua haraka sana
 
Tatizo ndugu yangu ni kwamba kama una mambo au jambo la kujibu toka kwa wapinzani wako kuna taratibu fulani za kufuata na sio kama hivi za kuja hapa JF na kuongea na kuandika mambo ya jikoni na kutoa upenyo kwa Wapinzani wako kukusema na kukuadhibu mwakani. CHADEMA wao ndio wanasimamia. na tena kama kuna mtu amedhulumiwa haki yake kama hivi basi kuna mamlaka kamili ya kutoa hukumu na sio kuja na kusema huku JF. Sasa sisi tulikuwa tunamuona Zitto kama Mentor yetu, kweli tunazidi kupunguza imani na mambo yanatokea kwake ikiwa yeye ndio mdau mkuu wa CHAMA.


Mkuu wao ndio wameanza kuja hapa jf,wao ndio hawakufuata taratibu ,kwanini hawakumuita zitti huko kwenye ze said utaratibu wa chama na kumweleza hayo mambo yake ya kifisadi??

Rudi nyuma kidogo kasome post kuanzia mwanzo Zitto amemtaja memba humu na kusema anamfahamu kuwa ni nani huko chadema ,ndipo zitto naye akanza kushusha bakola.

Waambie kwanza hao chadema wafuate utaratibu.Mkuu nimekuuliza kosa la zitto ni kutumia humu jina lake halisi.?
 
Mkuu wao ndio wameanza kuja hapa jf,wao ndio hawakufuata taratibu ,kwanini hawakumuita zitti huko kwenye ze said utaratibu wa chama na kumweleza hayo mambo yake ya kifisadi??

Rudi nyuma kidogo kasome post kuanzia mwanzo Zitto amemtaja memba humu na kusema anamfahamu kuwa ni nani huko chadema ,ndipo zitto naye akanza kushusha bakola.

Waambie kwanza hao chadema wafuate utaratibu.Mkuu nimekuuliza kosa la zitto ni kutumia humu jina lake halisi.?
Hata kama angetimia jina la vichochoroni But the way uandishi wake ulivyo tungejua kabisa kuwa ni yeye. Hivyo Mimi kikubwa nasema kuwa yeye ni kiongozi mkubwa ndani ya CHADEMa na hivyo wanavyoboronga wote wanashiriki na mambo yaliyoandika hapa angepaswa kuyasema ndani na sio kuyamwaga hapa. Sisi hutuwezi kushuhudia CHADEMa ikipelekwa kama hivi wanavyotaka kwenda na kuomba huruma toka wa watu
 
Ndugu zangu,

Katika kipindi hiki sikutaka kabisa kuingia na kujibu hoja yeyote ndani ya JF kuhusiana na uchaguzi wa vijana Taifa. Hata hivyo mtaniwia radhi kujibu hili ili kuweka rekodi sahihi kutokana na upotoshaji ambao unafanyika kwa makusudi kabisa ili kushusha heshima yangu katika jamii.

Moja, mimi ni mumbe wa Baraza la Vijana la CHADEMA kwa nafasi yangu ya kuwa mjumbe wa Kamati Kuu wa kuchaguliwa kuwakilisha vijana na nikiwa Mbunge mwenye umri wa ujana (miaka 33). Hivyo kushiriki kwangu kwenye vikao ni jambo la kawaida kabisa kwani nina haki ya kupiga kura. Vile vile nina haki ya kuamua mgombea gani wa kumuunga mkono katika uchaguzi. Niseme waziwazi kuwa David Kafulila ndiye mgombea niliyemwunga mkono na kumfanyia kampeni waziwazi bila kificho chochote kile. Hii inatokana na tabia yangu ya kutokuwa mnafiki. Nilimwunga mkono David Kafulila na alishinda kwa kupata kura 99 dhidi ya kura 73 ambazo alipata mgombea mwingine John Heche ambaye alikuwa anaungwa mono na kundi lililonipinga kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa.
Huyu aliyeandika post hii ni mmoja wa vijana wa makao makuu ya CHADEMA ambaye amekuwa akinipinga siku zote kwa chuki tu ya kuwa mimi nimepaata umaarufu wa kisiasa kuliko yeye na kundi lake.

Mama yangu mzazi ni mwanachadema. Ni kiongozi mwandamizi wa CHADEMA kutoka mkoa wa Kigoma na amekuwa msaada mkubwa wa chama katika Manispaa ya Kigoma. Ninaomba sana masuala yangu ya kisiasa na mahasimu wangu wasimhusishe mama yangu mzazi. Ninaomba sana sana mumuweke mama yangu pembeni. Mwandishi wa post hii tafadhali naomba usimhusishe mama yangu na tofauti zetu za kisiasa. Ninaomba sana hili liheshimiwe.

Pili, ni dhahiri kulikuwa kuna makundi katika uchaguzi wa BAVICHA. Mimi niliweka wazi msimamo wangu wa kumwunga mkono kafulila. Wakurugenzi wa Makao makuu ya chama kuanzia Katibu Mkuu mpaka wakurugenzi kama John Mnyika, John Mrema na hata maafisa kama Halima Mdee walikuwa wanampinga David Kafulila. Hawa wanaogopa uwezo wa Kafulila wa kukataa kutumika na kuwa independent katika maamuzi yake.
Hii sio mara ya kwanza kwa Kafulila kuzuiwa haki yake. Kijana huyu alipitishwa kugombea Ukurugenzi wa vijana na jina lake kwenda katika Kamati Kuu. Ajenda ya uteuzi wake ikasitishwa baada ya kuhofia kuwa atashinda. Mtindo huo huo wameutumia sasa kufuta uchaguzi na kuupeleka mbele mpaka baada ya miezi 6. Mimi nimekataa

1. Uchaguzi umefanyika.
2. Matokeo hayakutangazwa
3. Hakuna aliyekata rufaa

Hivyo, wazee wanapata wapi 'locus' ya kufuta uchaguzi?

Hata hivyo wenye mamlaka ya kufuta uchaguzi ni Kamati Kuu ya chama maana kuna taratibu za rufaa ndani ya chama chetu. Nimetaka Kamati Kuu iitishwe ili taratibu zifuatwe.

Huyu mtu aliyeleta post hii hapa anataka kuspin ili kupinda ukweli bila aibu.

David Kafulila kashinda round ya kwanza zaidi ya 50%. Wamekataa kutangaza matokeo na kuleta fujo kwenye mkutano.

Kuna tuhuma dhidi yangu kuwa nimetoa rushwa. Huku ni kutapatapa kwani tuhuma hizi zinatolewa bila ushahidi. Hivi huyu mwandishi na akili zake timamu anaweza kuweka akilini kwake kuwa mimi naweza kutoa rushwa hadharani? Eti nimevuta kiti na kuita watu kutoa rushwa. Bila adabu anamhusisha mama yangu mzazi.

Mama yangu ana maamuzi yake binafsi na mfano dhahiri ni uchaguzi wa chaha wangwe ambapo mimi nilimwunga mkono arfi na yeye akamwunga mkono Chacha wangwe waziwazi na bila kificho.

Uchaguzi wa vijana haukua na rushwa. Uchaguzi wa vijana wa chadema umefanyika kwa amani kabisa na matokeo hayakutangazwa kwa kuwa mgombea 'wao' hakushinda.

Wanasema eti Mtemelwa aliyekuwa ananiunga mkono alishindwa Temeke. Hawasemi watu waliowatuma kwa kutumia fedha za chama kugombea mikoa 15 na kutupwa chini na watu wanaoniunga mkono. Ukiwemo mkoa wa Dodoma na Shinyanga ambao walitumwa wakurugenzi wa chama kama Benson Kigaila na Erasto Tumbo na kushindwa. Habarindiyohiyo nakuomba ukumbuke kuwa baada ya uchaguzi kinachofuata ni ukaguzi wa fedha za chama katika kipindi hiki na jinsi zilivyotumika. Nashukuru Mungu kuwa ukaguzi huo sasa utafanywa na CAG

Katika spirit ya umoja na mshikamano wa chama tutamaliza suala hili katika Kamati Kuu ya chama.

Ninaomba sana vijana wa Makao Makuu - hasa Mrema, Mnyika na wengineo waache spinning za kipumbavu ambazo hazijengi umoja na mshikamano wa chama. Waache kuchafua jina langu. Wakumbuke kuwa kuna maisha mbele yetu na kuna kazi ya kujenga chama chetu.

Vijana hawa wakumbuke kuwa majungu hulipwa hapa hapa duniani. Wasubiri nao watakuwa wabunge na watapata ajenda zao za kuwafanya kuwa maarufu.

Wakumbuke pia mimi na Mbowe tunafahamiana kabla yao na tutakaporekebisha tofauti zetu na kugundua wapambe nuksi watakuwa kwenye aibu kubwa. Dunia hadaa!


Haya ambayo nimeyaandika hapa JF nimewaambia vijana hawa 'face to face' ili waache uwongo, uzandiki, majungu, fitna na chuki.

Kafulila kashinda uenyekiti wa vijana. Mpeni ushindi wake. Msibake demokrosia.

Poleni wana JF. Haya hayakuwa ya hapa lakini imebidi. Mwenyekuelewa kaelewa.

Dah! jamani? si tulisema? mkafikiri tuna chuki,sasa hiyo ndo chadema chama m-badala.
Maelezo ya kamanda Zitto yanaeka wazi kuwa chadema :
- Rushwa- kwenye uchaguzi na inaonekana na hata chaguzi za nyuma.

- Democras- Zitto kaenguliwa,kafulia ndo huyo hapewi ushindi wake tena kwa mara ya pili.

- Ufisadi- hapo Zitto alipowaonya kuwa ukimaliza uchaguzi kuna ukaguzi wa mahesabu tena unafanywa na CAG.

- Udicteta- Kiongozi anatoa maaumuzi peke yake,kwa mfano hapo imeonesha dr slaa,na kulazimishana kujiondoa ktk chaguzi,kunyimwa ushindi.

- Makundi- hapo tumeona watu wanavotuhumiana hadharani kabisa,sasa haya ya juu,jee ya ndani.

- Maslahi binafsi- Hapo tumeona jinsi kila moja anavojitetea kwa maslahi yake badala ya chama,na wengine kusema wanang'ara zaidi kuliko wengine

- Siri- Chama hakina siri,watu wanaropoka tu,utafikiri hakuna uongozi ndani ya chama au hakuna kanuni madhubuti.

- Katiba- Katiba haifuatwi kabisa,kila mmoja anaamua vile ambavyo wanaona bora kwao,na hasa hili kundi la kina Nyere wa pili,kina Mtei..

- Majungu- chama kimejaa majungu mpaka viongozi wa juu,inaonesha wazi viongozi ni dhaifu mno na kunaonesha kama viongozi hawajakomaa kielimu kutokana na hili.

JAMANI,JAMANI CHADEMA NDO HII. Sijui wapi tunakwenda. Naona Lwakatare simsikii?
 
Kubalini makosa yenu, jifunzeni kujisahihisha halafu muanze upya na sio kutaka kushambulia mliowkosea ili kuhalalisha makosa mliyoyafanya na mnaendelea kuyafanya kama spining hii mliyoleta hapa

omarilyas

Nd. Omarilyas,

Nimekuwa na wewe tokea hii saga hapa imeanza mpaka ilikofikia. Nashukuru kwa kunijibu yote nimeyaelewa ila kuna vitu vingi vinahitaji majibu na wewe huwezi kujibu viko zaidi ya uwezo wako ila unadandia!
1. Kuhusu Dowans + Mh. Zitto + RA
2. Mh. Zitto kujaza fomu za kugombea Uenyekiti akiwa Airport ile haraka haraka (kujitofautisha na viongozi wenzake yaani bila {team work}
3. Mambo ya Kumuua Wangwe
4. Kuja JF kutoa siri zote za chama na kupiga kampeni waziwazi (BAVACHA) akiwa kiongozi wa ngazi za juu

Huyu Mheshimiwa amekuwa kwenye uongozi tokea nyuma ghafla ndo uchaga/wazee ameuona sasa hivi? ndo pesa zinaliwa?

Mr. Omarilyas nadhani unakumbuka Mr. Msabaha kule ZNZ usanii wake wa kutekwa mpaka alipoibukia unajua! basi picha ndo hii!
 
Hata kama angetimia jina la vichochoroni But the way uandishi wake ulivyo tungejua kabisa kuwa ni yeye. Hivyo Mimi kikubwa nasema kuwa yeye ni kiongozi mkubwa ndani ya CHADEMa na hivyo wanavyoboronga wote wanashiriki na mambo yaliyoandika hapa angepaswa kuyasema ndani na sio kuyamwaga hapa. Sisi hutuwezi kushuhudia CHADEMa ikipelekwa kama hivi wanavyotaka kwenda na kuomba huruma toka wa watu

hoja yangu mbona hao walioanza hawakuyapeleka huko ndani ya chama,na huyo mzee mtei kapanda public ama hilo nalo ni gumu kuliona.?

jf ni chombo cha habari kama kilivyo chombo chochote ambacho mtei alipanda nacho hewani, na afterall sio zito alianza kuleta haya mambo hapa jf na badala yake unamshauri ayapeleke huko kwa ambao wao ndio hao walioanza kuyaleta hapa jf.

Mkuu sikuelewi una maanisha nini,naomba ufafanuzi zaidi.
 
hawa jamaa kwa kweli wako poa sana,ni chama ambacho kwa kweli hata wengine ambao tunaona siasa ni chafu tunaweza tukajiunga nao.
Kuweni makini chadema,jiepusheni na mamluki.

wish you all the best chadema
 
hoja yangu mbona hao walioanza hawakuyapeleka huko ndani ya chama,na huyo mzee mtei kapanda public ama hilo nalo ni gumu kuliona.?

jf ni chombo cha habari kama kilivyo chombo chochote ambacho mtei alipanda nacho hewani, na afterall sio zito alianza kuleta haya mambo hapa jf na badala yake unamshauri ayapeleke huko kwa ambao wao ndio hao walioanza kuyaleta hapa jf.

Mkuu sikuelewi una maanisha nini,naomba ufafanuzi zaidi.
tutataka wakaee ndani na waongee na sio kuja hapa kuandika kama hivi
 
Kwanza Pole Mh. Zitto kwa kashikashi zote hizo,

Hivi ukiwa kama Kiongozi Mkuu kwenye Ukatibu Mkuu Makamu hivi huoni kuwa umeingilia huo uchaguzi kwa kusema wewe mwenyewe kuwa ulifanya kampeni wazi wazi kwa vijana hawa wadogo huoni kuwa ukutenda kosa??

Mh Zitto! kwenye kipindi kama hiki kizito kwa chama kwanini usiwe na moyo kama wa mwenyekiti wako Mbowe ukakaa kimya kwa masrahi ya chama kwanza, unapoanza kusema mambo ya Fedha (CAG) huoni kuwa hapo kuna mushkeli,

Pia kuja hapa kwenye JF forum kumwaga razi lote hilo ambalo kuna utitiri wa wanaCCM kibao, huoni kuwa unavujisha siri??

Mimi sina chama ila picha unayoonyesha ni ile ya mapindikizi ya CCM tuliyozoea kuona!!!

Nadhani wazee wa chadema waliliona hili. Kijana bado hajakomaa na hivyo wasingeweza kumwamini kumpa chama akiongoze (hata kama ana umaarufu!).
 
Ndugu zangu,

Katika kipindi hiki sikutaka kabisa kuingia na kujibu hoja yeyote ndani ya JF kuhusiana na uchaguzi wa vijana Taifa. Hata hivyo mtaniwia radhi kujibu hili ili kuweka rekodi sahihi kutokana na upotoshaji ambao unafanyika kwa makusudi kabisa ili kushusha heshima yangu katika jamii.

Moja, mimi ni mumbe wa Baraza la Vijana la CHADEMA kwa nafasi yangu ya kuwa mjumbe wa Kamati Kuu wa kuchaguliwa kuwakilisha vijana na nikiwa Mbunge mwenye umri wa ujana (miaka 33). Hivyo kushiriki kwangu kwenye vikao ni jambo la kawaida kabisa kwani nina haki ya kupiga kura. Vile vile nina haki ya kuamua mgombea gani wa kumuunga mkono katika uchaguzi. Niseme waziwazi kuwa David Kafulila ndiye mgombea niliyemwunga mkono na kumfanyia kampeni waziwazi bila kificho chochote kile. Hii inatokana na tabia yangu ya kutokuwa mnafiki. Nilimwunga mkono David Kafulila na alishinda kwa kupata kura 99 dhidi ya kura 73 ambazo alipata mgombea mwingine John Heche ambaye alikuwa anaungwa mono na kundi lililonipinga kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa.
Huyu aliyeandika post hii ni mmoja wa vijana wa makao makuu ya CHADEMA ambaye amekuwa akinipinga siku zote kwa chuki tu ya kuwa mimi nimepaata umaarufu wa kisiasa kuliko yeye na kundi lake.

Mama yangu mzazi ni mwanachadema. Ni kiongozi mwandamizi wa CHADEMA kutoka mkoa wa Kigoma na amekuwa msaada mkubwa wa chama katika Manispaa ya Kigoma. Ninaomba sana masuala yangu ya kisiasa na mahasimu wangu wasimhusishe mama yangu mzazi. Ninaomba sana sana mumuweke mama yangu pembeni. Mwandishi wa post hii tafadhali naomba usimhusishe mama yangu na tofauti zetu za kisiasa. Ninaomba sana hili liheshimiwe.

Pili, ni dhahiri kulikuwa kuna makundi katika uchaguzi wa BAVICHA. Mimi niliweka wazi msimamo wangu wa kumwunga mkono kafulila. Wakurugenzi wa Makao makuu ya chama kuanzia Katibu Mkuu mpaka wakurugenzi kama John Mnyika, John Mrema na hata maafisa kama Halima Mdee walikuwa wanampinga David Kafulila. Hawa wanaogopa uwezo wa Kafulila wa kukataa kutumika na kuwa independent katika maamuzi yake.
Hii sio mara ya kwanza kwa Kafulila kuzuiwa haki yake. Kijana huyu alipitishwa kugombea Ukurugenzi wa vijana na jina lake kwenda katika Kamati Kuu. Ajenda ya uteuzi wake ikasitishwa baada ya kuhofia kuwa atashinda. Mtindo huo huo wameutumia sasa kufuta uchaguzi na kuupeleka mbele mpaka baada ya miezi 6. Mimi nimekataa

1. Uchaguzi umefanyika.
2. Matokeo hayakutangazwa
3. Hakuna aliyekata rufaa

Hivyo, wazee wanapata wapi 'locus' ya kufuta uchaguzi?

Hata hivyo wenye mamlaka ya kufuta uchaguzi ni Kamati Kuu ya chama maana kuna taratibu za rufaa ndani ya chama chetu. Nimetaka Kamati Kuu iitishwe ili taratibu zifuatwe.

Huyu mtu aliyeleta post hii hapa anataka kuspin ili kupinda ukweli bila aibu.

David Kafulila kashinda round ya kwanza zaidi ya 50%. Wamekataa kutangaza matokeo na kuleta fujo kwenye mkutano.

Kuna tuhuma dhidi yangu kuwa nimetoa rushwa. Huku ni kutapatapa kwani tuhuma hizi zinatolewa bila ushahidi. Hivi huyu mwandishi na akili zake timamu anaweza kuweka akilini kwake kuwa mimi naweza kutoa rushwa hadharani? Eti nimevuta kiti na kuita watu kutoa rushwa. Bila adabu anamhusisha mama yangu mzazi.

Mama yangu ana maamuzi yake binafsi na mfano dhahiri ni uchaguzi wa chaha wangwe ambapo mimi nilimwunga mkono arfi na yeye akamwunga mkono Chacha wangwe waziwazi na bila kificho.

Uchaguzi wa vijana haukua na rushwa. Uchaguzi wa vijana wa chadema umefanyika kwa amani kabisa na matokeo hayakutangazwa kwa kuwa mgombea 'wao' hakushinda.

Wanasema eti Mtemelwa aliyekuwa ananiunga mkono alishindwa Temeke. Hawasemi watu waliowatuma kwa kutumia fedha za chama kugombea mikoa 15 na kutupwa chini na watu wanaoniunga mkono. Ukiwemo mkoa wa Dodoma na Shinyanga ambao walitumwa wakurugenzi wa chama kama Benson Kigaila na Erasto Tumbo na kushindwa. Habarindiyohiyo nakuomba ukumbuke kuwa baada ya uchaguzi kinachofuata ni ukaguzi wa fedha za chama katika kipindi hiki na jinsi zilivyotumika. Nashukuru Mungu kuwa ukaguzi huo sasa utafanywa na CAG

Katika spirit ya umoja na mshikamano wa chama tutamaliza suala hili katika Kamati Kuu ya chama.

Ninaomba sana vijana wa Makao Makuu - hasa Mrema, Mnyika na wengineo waache spinning za kipumbavu ambazo hazijengi umoja na mshikamano wa chama. Waache kuchafua jina langu. Wakumbuke kuwa kuna maisha mbele yetu na kuna kazi ya kujenga chama chetu.

Vijana hawa wakumbuke kuwa majungu hulipwa hapa hapa duniani. Wasubiri nao watakuwa wabunge na watapata ajenda zao za kuwafanya kuwa maarufu.

Wakumbuke pia mimi na Mbowe tunafahamiana kabla yao na tutakaporekebisha tofauti zetu na kugundua wapambe nuksi watakuwa kwenye aibu kubwa. Dunia hadaa!


Haya ambayo nimeyaandika hapa JF nimewaambia vijana hawa 'face to face' ili waache uwongo, uzandiki, majungu, fitna na chuki.

Kafulila kashinda uenyekiti wa vijana. Mpeni ushindi wake. Msibake demokrosia.

Poleni wana JF. Haya hayakuwa ya hapa lakini imebidi. Mwenyekuelewa kaelewa.

Kaka kama mambo ndiyo haya, kama ndivyo mnavyojibizana kwenye vyombo vya habari, nasikia harufu ya ile NCCR ya Lyatonga Mrema! Panapofuka moshi pana moto kaka, hapo kwenu mkichelewachelewa yatakuwa masizi!
 
Nadhani wazee wa chadema waliliona hili. Kijana bado hajakomaa na hivyo wasingeweza kumwamini kumpa chama akiongoze (hata kama ana umaarufu!).
Mimi Nasema kuwa Zitto ni mwanasiasa mzuri but sasa amelewa sifa na bado kuongoza CHADEMA ila huko mbele kama akijirekebisha basi itakuwa neema kwake,
 
This is part of spinning. Uwongo, uzushi nk. Tatizo wanaopanga haya wanasahau kuwa tuliyapanga wote dhidi ya marehemu Chacha Wangwe. Unatengeneza uwongo, unausambaza, na hatimaye wewe mwenyewe unauamini kuwa ni kweli.

Kama kuna kitu kilimuuma marehemu wangwe na alikufa nacho ni kile cha kumsema kuwa alikuwa anatumiwa na mafisadi. Namshukuru Mungu kuwa nilimwomba radhi Chacha kabla na baada ya kifo chake siku ya postmorterm kwa kumzushia uwongo.

Asha ni mmoja wa wenzangu tulioshiriki kumtenda Chacha. Wanatumia mtindo ule ule na wanapita njia zile zile. Rashidi wa Kuli alisema, YANA MWISHO HAYA!

Asha, (ninakujua wewe ni nani) kuwa mkweli wa nafsi yako! Utalipwa hapa hapa duniani kwa uzushi wako na wenzako.

To put record clear - Kasisiko sio ndugu yangu wa damu. Ni mwenyekiti wangu tu wa Mkoa Kigoma. Pili, Baregu hajahudhuria kikao hata kimoja cha wazee toka ajue ukweli wa mambo.
Tatu, chama jana kimechagua rasmi Baraza la Wazee na mgombea aliyekuwa ananiunga mkono waziwazi ameshinda. Inakuwaje bado vikao vya wazee vya chama vinaendeshwa na Mtei na Ndesamburo?

Pili, vyombo vyote vya habari vilikuwapo katika hotuba ya Mtei. Imekuwaje NIPASHE peke yake ndio ione alisema kuna ufisadi kwenye chaguzi za chama? Mhariri mtendaji wa Nipashe ni jesse kwayu kutoka Machame. Mmiliki wa Nipashe ni Reginald Mengi kutoka Machame.

Spinns sio sustainable. Acheni tujenge chama chetu.

Kaka Zitto nakata tamaa sasa! Hata wewe ulishiriki kumtenda Chacha Wangwe? Na ungamo hili limekutoka katika mwezi huu mtukufu nina uhakika ni kweli umeshiriki kumfanyia ubaya Chacha kama ulivyokiri mwenyewe. Kama ulivyokiri mwenyewe, Mwenyezi Mungu akujalie msamaha kwa toba yako katika mwezi huu mtukufu.

Lakini nimekata tamaa kabisa na CHADEMA yenu.
 
Mama Zitto afyatuka, uchaguzi Chadema wafutwa

Mwiba naomba ukiwa una quote gazeti basi tuletee na jina la gazeti ili tuchambue ni gazeti la nani tafadhali. Samahani ingawa wewe humu ni mzoefu ila ni angalizo.
 
Zitto, acha kuandika uongo na kuaminisha umma juu ya matokeo ya vijana .
Matokeo na ambayo ulikuwa nayo wewe kwani ulikuwa meza kuu na mimi sikuwepo meza kuu ni haya;
David Kafulila = 99
John Heche =83
Dady Igogo= 11
Julieth Rushuli= 11.

jumla zilikuwa kura 204.

Idadi ya wajumbe halali walikuwa ni 164.

Naomba uweke rekodi sahihi na ukijua kuwa kusema ukweli daima ndio njia ya kuweza kujenga, umelaumu sana Mrema na Mnyika hata unafikia mahali pa kudanganya.

Waseminari wana kauli moja kuwa ukweli ni mmoja na haugawanyiki.

naomba niishie hapo kwa leo na nitakujua kujibu mengine yote dhidi yangu siku zijazo .

Nawatakia mjadala mwema.
 
Zitto, acha kuandika uongo na kuaminisha umma juu ya matokeo ya vijana .
Matokeo na ambayo ulikuwa nayo wewe kwani ulikuwa meza kuu na mimi sikuwepo meza kuu ni haya;
David Kafulila = 99
John Heche =83
Dady Igogo= 11
Julieth Rushuli= 11.

jumla zilikuwa kura 204.

Idadi ya wajumbe halali walikuwa ni 164.

Naomba uweke rekodi sahihi na ukijua kuwa kusema ukweli daima ndio njia ya kuweza kujenga, umelaumu sana Mrema na Mnyika hata unafikia mahali pa kudanganya.

Waseminari wana kauli moja kuwa ukweli ni mmoja na haugawanyiki.

naomba niishie hapo kwa leo na nitakujua kujibu mengine yote dhidi yangu siku zijazo .

Nawatakia mjadala mwema.
Ndio maana mimi napata shida sana kuona hali kama hii kutoka kwa Zitto na Kundi lake. Hivyo yeye badala ya kusimamia na kufanya kuwa makini na karibu sana na viongozi wake wa karibu na kufanya mambo ya ndani ya chama na siyo humo ndani JF. sisi kama Wasau hali hii inatuudhi sana na kutufanya kuchanganyikiwa hata kumuumiza roho zetu
 
uchoma kisu, uchaguzi vijana waahirishwa

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na maendeleo Dkt Willibrod Slaa akizungumza na waandishi wa habari akiwa pamoja na Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe kuhusu muelekeo wa uchaguzi wa baraza la vijana Taifa.
Na Waandishi Wetu
HALI ya kisiasa ndani ya Chadema imezidi kuchafuka baada ya uchaguzi wa Baraza la Vijana Taifa (Bavicha) kuahirishwa kwa miezi sita, huku mmoja wa wagombea wa nafasi hiyo (jina tunalo) akitishia kumchoma kisu mwanachama anayeaminika kuwa kambi ya naibu katibu mkuu, Zitto Kabwe.

Wakati hatma ya uchaguzi huo ikiwa bado njia panda, mizengwe imezidi kutikisa uchaguzi wa Jumuiya ya Wanawake baada ya mmoja wa wagombea anayeaminika kuwa upande wa Zitto kunusuruka kung'olewa.

Joto zaidi linaloonyesha hali tete ndani ya Chadema, lilipandishwa na hatua iliyotangazwa jana mchana na katibu mkuu, Dk Wilbrod Slaa ya kuahirisha uchaguzi huo hatua ambayo ilipingwa na Zitto na msemaji wa chama hicho David Kafulila ambao wanataka kutangazwa kwanza kwa matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika juzi na kuitishwa kikao cha dharura cha Kamati Kuu (CC), ambacho inasemekana kinafanyika leo.

Wagombea waliokuwa wakiwania nafasi ya uenyekiti wa Bavicha ni John Heche, Dadi Igogo na David Kafulila ambaye licha ya kuwa ofisa habari wa chama hicho, anatarajiwa kuwania ubunge Jimbo la Kigoma Kusini mwaka 2010.

Akitangaza kuahirishwa kwa uchaguzi huo jana, Dk Willibrod Slaa alisema uchaguzi huo utafanyika ndani ya miezi sita ijayo.

“Mimi kama katibu nimeshauriana na kamati ya wazee ya chama nikiongozwa na Mzee (Edwin) Mtei, Bob Makani na Balozi (Christopher) Ngaiza tumeubatilisha uchaguzi huo, hivyo utafanyika ndani ya miezi sita ijayo,” alisema Slaa.

“Tumeamua hivi kwa sababu kwanza kufanya uchaguzi ni gharama, tunatumia karibia Sh50 milioni ambazo zinaweza kujenga zahanati moja. Jamani hapa tutawaeleza nini Watanzania.

“Wajumbe walidai kuwa uchaguzi ulijaa rushwa, lakini niliwambia waandike malalamiko kwa maandishi na ujumbe mfupi na wamenipatia nitayafanyia kazi na yatatolewa maamuzi na vyombo husika.”

Lakini Zitto alipinga uamuzi huo akisema katibu mkuu hana mamlaka ya kutoa tangazo hilo na kwamba nanlaka hayo ni Kamati Kuu (CC).

"Lakini pia, chombo pekee chenye uwezo wa kufanya uamuzi huo ni Kamati Kuu, sasa inakuaje chombo kingine kichukue uamuzi tena bila matokeo kutangazwa wala mgombea kukata rufaa," alisema Zitto.

Alifafanua kuwa uamuzi huo umetokana na baadhi ya watu kukataa matokeo hayo baada ya kuweka mbele maslahi binafsi badala ya maslahi ya chama kwa kuwa jambo la msingi katika suala hilo ni matokeo hayo kutangazwa kwanza kabla ya kuahirisha uchaguzi.

"Jambo la kwanza ni kutangaza matokeo na baadaye kama kuna mgombea alikuwa akipinga, anaweza kukata rufaa, lakini matokeo hayajatangazwa wala hakuna aliyekata rufaa," alifafanua Zitto.

Kutokana na utashi wa katiba, Zitto alisema tayari amemwomba katibu mkuu kuitisha mkutano wa CC kujadili suala hilo.

"Nimemwomba Dk Slaa aitishe kikao cha Kamati Kuu tujadili hii hali maana kama viongozi hatutakuwa na busara na chama kitavurugika," alionya.

Alipoulizwa nini mustakabali wa Chadema kutokana na matukio hayo ya vurugu yanayotikisa chama, alijibu: "Viongozi tusipotumia busara chama kitavurugika, lakini tukitumia busara na kuweka maslahi ya chama mbele, tutaweza kutatua haya mambo kwa urahisi."

Zitto alihoji: "Kwanini wazee wasitumie busara kama walizotumia kuniomba mimi nijitoe kwa kutaka wagombea wengine wajitoe au wakubali matokeo kwa kumwachia Kafulila?

"Tukiwa na busara; tukiheshimu demokrasia, tutaweza kuvuka salama. Naamini hilo tu ndiyo suluhisho la kukivusha chama salama."

Naye Kafulila alipinga uamuzi wa kuahirisha uchaguzi kabla ya kutangaza matokeo akisema anataka kutangazwa kwanza kwa matokeo ambayo anaamini, yalimpa ushindi.

Akizungumza na gazeti hili jana, Kafulila alisema haoni sababu ya kutotangazwa kwa matokeo hayo ambayo anaamini alishinda licha ya kutokubalika na sehemu kubwa ya wajumbe wa sekretarieti na wabunge wa viti maalum.

"Ukiangalia hata hayo mambo ya karatasi kuongezeka, utaona labda ulikuwa ni mpango maalumu wa kumwangusha mtu fulani, lakini imeshindikana," aliongeza.

"Kwa kifupi, sikubaliani na uamuzi huo ninachotaka kwanza matokeo yatangazwe na pia baraza halina mamlaka hayo. Hiyo ni kazi ya Kamati Kuu."

Habari zinadai kuwa tangu John Mnyika kuondoka kwenye wadhifa wa uenyekiti wa vijana wa Chadema, kumekuwa na mkakati wa kumdhibiti Kafulila unaofanywa na baadhi ya vigogo wa Chadema kutokana na mgombea huyo kuonekana mwiba kwao.

Kafulila anasemekana kuwa ni mtu anayepinga waziwazi mambo yanayoendeshwa kinyume na taratibu na amekuwa hahofii viongozi wa juu yake kueleza msimamo wake.

Wakati hayo yakiendelea, vurugu zaidi zimezidi kutikisa chama hicho na jana zilifikia katika hatua ya mgombea mmoja wa nafasi ya uenyekiti wa vijana kutaka kumchoma kisu mwanachama ambaye alikuwa akimtetea Zitto Kabwe asitukanwe na mgombea huyo.

Kabla ya kufikia hatua ya kutishiana visu, mgombea huyo alikuwa akibishana na baadhi ya wafuasi wa Kafulila kwenye ofisi za makao makuu ya Chadema zilizo Kinondoni jijini Dar es salaam.

Wakati Mwananchi inafika kwenye ofisi hizo majira ya saa 7:00, vurugu zilikuwa zimeshapoa tangu saa 5:00, lakini wanachama walikuwa wamekaa kwenye vikundi wakijadili matukio mbalimbali ya uchaguzi.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, mgombea huyo na mwanachama mmoja anayedaiwa kuwa anamuunga mkono Kafulila, walirushiana ngumi kwanza na baadaye ndipo mgombea huyo alipotoa kisu na kumtishia.

Mashuhuda hao walidai kwamba mara baada ya mgombea huyo kutoa kisu, wanachama wengine waliokuwa karibu waliingilia kati na kumtoa eneo hilo.

Mwanachama anayedaiwa kutishiwa kisu aliiambia Mwananchi kuwa alikuwa akimsihi mgombea huyo kuacha kumsema vibaya Zitto kwa kuwa malalamiko yote ya uchaguzi wa juzi yako ngazi za juu za chama hicho.

Mwanachama huyo alifafanua kwamba baada ya kumwambia mgombea huyo maneno hayo, alipandisha ghadhabu zaidi na kuanza kutukana.

“Sasa mimi nilivyoona anamtukana Zitto, nilimwambia aache lakini hakusikia; alikuwa anasema Zitto wako na Kafulila walishirikiana kumwibia kura. Kutokana na kuendelea kuongea ovyo, tulishikana na alivyoona muziki ni mnene alinitolea kisu na kutaka kunichoma,” alidai.

Katika hatua nyingine, Dk Slaa juzi alilazimika kurudi katika ukumbi wa uchaguzi wa Bavicha mnamo saa 6:20 usiku ili kutuliza ghasia zilizoibuliwa na wajumbe mara baada ya kupata habari kuwa kura 20 ziliongezeka katika nafasi ya mwenyekiti.

Wajumbe hao ambao walionekana kuwa upande wa mgombea wa nafasi hiyo, John Heche ambaye ni diwani wa Tarime Mjini, walipinga matokeo kabla hayajatangazwa hali iliyomlazimu msimamizi wa uchaguzi huo, Charles Mwera, ambaye pia ni mbunge wa Tarime, kutoyatangaza.

Dk Slaa, ambaye aliondoka kwenye ukumbi huo juzi saa 7:00 mchana, alirejea kwa mara ya pili saa 6:20 usiku, vurugu zikiendelea baada ya Heche kumpiga ngumi mbili ofisa wa kurugenzi ya uchaguzi ya Chadema, Ali Chitandana na kumlazimu kufanya kazi kubwa kuzituliza.

“Jamani wajumbe nawaomba muwe watulivu kila kitu kilichotokea nimepewa taarifa na Mnyika, kwa hiyo kama kuna mtu ana malalamiko ayaandike na kuyawasilisha makao makuu ya chama kesho (jana) asubuhi ili niyafanyie kazi,” alisema Dk Slaa.

Katika hatua nyingine, wajumbe hao walimweleza wazi Dk Slaa kuwa hawajalipwa fedha zao za posho hali iliyomlazimu katibu huyo mkuu kumwagiza Mtunza Fedha kuwalipa wajumbe hao kutoka mikoa mbalimbali nchini usiku huohuo.

“Wewe Mtunza Fedha walipe wajumbe posho zao; jamani nimeshamwagiza atawalipa wote ila wale ambao wameshakata tiketi kwa ajili ya kusafiri watarudishiwa fedha zao kesho (jana) kwa sababu hamuwezi kuondoka kwa kuwa uchaguzi huu unaweza kurudiwa, lakini yote yatajulikana mara baada ya viongozi kukutana,” alisema Dk Slaa.

“Kwa kweli, nimesikitika sana hiki kitendo kilichotokea leo ni aibu kwa chama. Hapa wapinzani na magazeti yatapata pa kusemea.

Hiki chama ni cha demokrasia; nahitaji kujua kila kitu kilichotokea ili vifanyiwe maamuzi na yeyote atakayebainika kuhusika kwa namna moja au nyingine atachukuliwa hatua kali kwa mujibu wa katiba ya chama.”

Habari hii imeandikwa na Ramadhan Semtawa, Fidelis Butahe, Musa Mkama na Fred Azzah

Hapani shindwa kumuelewa Dr.Slaa uchaguzi unapoalishwa lazima kuwe na sababu na ili sababu ziwepo ni kutaja matokeo ili kutoa nafasi kwa wale wasiokubaliana na matokeo kukata rufaa.Nashindwa kuelewa Mh.Dr.Slaa anaposemo uchaguzi utafanyika katika kipindi cha miezi 6 kwa sababu gharama za uchaguzi ni kubwa 50millioni wananchi hawatatuelewa nikwanini katika kipindi hiki ambapo wajumbe wote wamekusanyika usitafutwe utaratibu wa kurudia uchaguzi huo hii itakua rahisi na kubana matumizi au upepo wa uchaguzi kwa hivi sasa hauko katika muelekeo wa kudi fulani na hilo kundi linategemea ktk kipindi cha miezi 6 litaweza kujipanga.INASIKITISHA MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Ndio maana mimi napata shida sana kuona hali kama hii kutoka kwa Zitto na Kundi lake. Hivyo yeye badala ya kusimamia na kufanya kuwa makini na karibu sana na viongozi wake wa karibu na kufanya mambo ya ndani ya chama na siyo humo ndani JF. sisi kama Wasau hali hii inatuudhi sana na kutufanya kuchanganyikiwa hata kumuumiza roho zetu

Kaka haya mambo yanaoneka ni makubwa sana,na yapo ndani kwa ndani,na inaonekana ilikuwa inasubiri siku tu ifike,na ninavoona bado kuna moto mkubwa uwaka ndani kwa ndani,nakumbuka siku moja kuna mdau mmoja humu aliwahi kuongea kuwa kuna moto mkubwa chini kwa chini ktk chadema lkn mmoja mimi nikamdharau,sasa nauona kumbe ni kweli na kwa hali hii hichi chama sasa kinanitia wasi wasi sana kama kipo kweli kwa ajili ya wananchi
 
Zitto, acha kuandika uongo na kuaminisha umma juu ya matokeo ya vijana .
Matokeo na ambayo ulikuwa nayo wewe kwani ulikuwa meza kuu na mimi sikuwepo meza kuu ni haya;
David Kafulila = 99
John Heche =83
Dady Igogo= 11
Julieth Rushuli= 11.

jumla zilikuwa kura 204.

Idadi ya wajumbe halali walikuwa ni 164.

Naomba uweke rekodi sahihi na ukijua kuwa kusema ukweli daima ndio njia ya kuweza kujenga, umelaumu sana Mrema na Mnyika hata unafikia mahali pa kudanganya.

Waseminari wana kauli moja kuwa ukweli ni mmoja na haugawanyiki.

naomba niishie hapo kwa leo na nitakujua kujibu mengine yote dhidi yangu siku zijazo .

Nawatakia mjadala mwema.

Haya matokeo mgeyatangaza siku hiyo ,na si kuja kuyatangazia jf.

Mliyatangaza haya matokeo siku hiyo?? hapo ndipo tutaanza kushika mwongo.

Hatudanganyiki tena kauli mbiu kuelekea 2010
 
hapa nafikiri kosa kubwa kuliko la wote ni la zitto.
hawezi kutaka tu kugombea uenyekiti bila ya kutoa taarifa za awali ndani ya chama, na nna uhakika kuwa zitto analijua hilo, ila alifanya kwa kusudi labda kuonyesha kuwa chama hakiendeshwi kwa demokrasia na akashindwa kujua impact ya hicho anachokifanya.

on top of that, kaja hapa kaanika siri za chama zote nje, kuanzia ya wangwe, ya CAG sijui na makundi ya watu ndani ya chama, .....nna wasi wasi zitto ana nia ya kuvunja chama na si vyenginenevyo

Nisichoelewa ni kwamba kwanini pale mtu anapokuwa na "siri" za maovu ya serikali au CCM hapa JF tumekuwa na tabia ya kushabikia kwamba hizo sio siri na ni lazima ziwekwe wazi maana hapa we dare to talk openly! Lakini all of the sudden imekuwa opposite kwa sababu Zitto kaleta uozo wa Chadema hapa, tunashabikia kuwa nin siri za chama hatupaswi kujua! It sounds like double standard to me!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom