Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
tatizo sio kutoa siri za chama ....tatizo ni namna alivyozitoa.
ametaja habari ya chacha wangwe baada ya kuonekana na yeye amefanyiwa spinning kama zile .....kwa maana hiyo hakuwa na nia ya kuzisema kama yasingemkuta na yeye.
amesema kuhusu habari ya mahesabu ya chama kwa sababu anataka kuwakomoa wengine ndani ya chama, baada ya yeye kuguswa na vitendo vyao
motive ya zitto ya kuanika siri za chama ndio inatutia wasiwasi.....na sio siri zenyewe
 
Nd. Omarilyas,

Nimekuwa na wewe tokea hii saga hapa imeanza mpaka ilikofikia. Nashukuru kwa kunijibu yote nimeyaelewa ila kuna vitu vingi vinahitaji majibu na wewe huwezi kujibu viko zaidi ya uwezo wako ila unadandia!
1. Kuhusu Dowans + Mh. Zitto + RA
2. Mh. Zitto kujaza fomu za kugombea Uenyekiti akiwa Airport ile haraka haraka (kujitofautisha na viongozi wenzake yaani bila {team work}
3. Mambo ya Kumuua Wangwe
4. Kuja JF kutoa siri zote za chama na kupiga kampeni waziwazi (BAVACHA) akiwa kiongozi wa ngazi za juu

Huyu Mheshimiwa amekuwa kwenye uongozi tokea nyuma ghafla ndo uchaga/wazee ameuona sasa hivi? ndo pesa zinaliwa?

Mr. Omarilyas nadhani unakumbuka Mr. Msabaha kule ZNZ usanii wake wa kutekwa mpaka alipoibukia unajua! basi picha ndo hii!

Ndugu zanguni kila Chama kina siri zake. Ni sawa katika familia kuna siri zake za ndani. Kama huko Chadema kulikuwa na uozo mbona hakukihama chama muda mrefu?? Amesubiri ameshapokea milungula ya mafisadi na akaona kabisa kuwa hana tena majority support ndiyo maana anataka kukigawa chama. Uongozi uliobaki Chadema, ninaomba sana mtemeni ZITTO, huyo ni traitor na kama mtaendelea kumkumbatia basi mjue mwendelezo wa mpasuko utaendelea. Ni hatari sana huyu.

Unajua zile fujo zake kule Mlimani akisoma ndizo hizo hizo anaendelea nazo!!! Zitto hivi nataka kukuuliza swali hapa na ujibu??!! Hivi ile course ya young ...... uliyopewa na Wajerumani kukuandaa kuwa kiongozi bora imeshia wapi??? Sidhani kama Wajerumani wanafurahi wakisikia habari zako za sasa?!!!! Again, please, uongozi wa CHADEMA let ZITTO pass out, ataua Chama na kitakosa nguvu. Mnaelekea pabaya.
 
Ndugu zanguni kila Chama kina siri zake. Ni sawa katika familia kuna siri zake za ndani. Kama huko Chadema kulikuwa na uozo mbona hakukihama chama muda mrefu?? Amesubiri ameshapokea milungula ya mafisadi na akaona kabisa kuwa hana tena majority support ndiyo maana anataka kukigawa chama. Uongozi uliobaki Chadema, ninaomba sana mtemeni ZITTO, huyo ni traitor na kama mtaendelea kumkumbatia basi mjue mwendelezo wa mpasuko utaendelea. Ni hatari sana huyu.

Unajua zile fujo zake kule Mlimani akisoma ndizo hizo hizo anaendelea nazo!!! Zitto hivi nataka kukuuliza swali hapa na ujibu??!! Hivi ile course ya young ...... uliyopewa na Wajerumani kukuandaa kuwa kiongozi bora imeshia wapi??? Sidhani kama Wajerumani wanafurahi wakisikia habari zako za sasa?!!!! Again, please, uongozi wa CHADEMA let ZITTO pass out, ataua Chama na kitakosa nguvu. Mnaelekea pabaya.


Kwa yaliyojili mpaka sasa inatosha kutambua kuwa Chadema si chama cha siasa, bali mkusanyiko wa wasanii na wahuni wenye malengo binafsi. I'm sorry to say sioni tofauti kati yake na CCM, in that sense sio chama mbadala! Kama Zitto kakiri kushiriki kumchongea shutuma Chacha Wangwe ni imani yangu kwamba kulikuwa na baraka za viongozi wenzie wa juu including wazee waasisi, kwa maana hiyo sidhani kama kuna msafi hapo! Kumtoa Zitto hakutasaidia kwa sababu uozo unaonekana haujaanzia kwake, ni wengi wameoza na tushukuru conflict zao zimeweza kutufumbua macho na kuona kwamba Chadema ni chama cha aina gani? Na kwanini unaita uozo kama huo siri za chama?Ooh My God, nani atatutoa kwenye utumwa wa CCM?
 
Nisichoelewa ni kwamba kwanini pale mtu anapokuwa na "siri" za maovu ya serikali au CCM hapa JF tumekuwa na tabia ya kushabikia kwamba hizo sio siri na ni lazima ziwekwe wazi maana hapa we dare to talk openly! Lakini all of the sudden imekuwa opposite kwa sababu Zitto kaleta uozo wa Chadema hapa, tunashabikia kuwa nin siri za chama hatupaswi kujua! It sounds like double standard to me!

Umesema sawia kabisa! watu wanataka Zitto awe kama punching bag kwa kupokea mashumbulizi tu bila kujibu. Hapa Kaja anaejiita Asha Abdallah na Mpaka Kieleweke ( mmoja mbunge na mwingine kiongozi mwandamizi wa Chadema) wamemtukana Zitto pamoja na mama yake. Zitto kaitwa fisadi mtoa na mpokea rushwa, mrokokaji nk hawa sio na wanachama wa kawaida bali viongozi wa chadema kubwa zaidi baba mkwe Mzee Mtei kanukuliwa na Nipashe akisema mafisadi wamepenyeza pesa kuharibu uchaguzi ( aki maanisha Zitto anatumiwa ) hayo yote yameanikwa hapa jamvini je mlitaka Zitto akawajibu wapi? je hao hawakuwa wanatoa siri?

Zitto yupo sahihi kwenye hili haya mambo ya kufuga ugonjwa mauti yatawafichua chama kinaendeshwa kibabe na kifamilia, watu wana shurutishwa kuondoa majina, bila haya Dr Slaa ( of all people ) anavunja uchaguzi wa vijana bila kufuata taratibu ( hana powers hizo ) halafu mnataka watu wakae kimya?

Hapa JF zimetungikwa nyaraka kadhaa wa kadhaa za siri za serikali na mikataba je watetezi wa siri mlikuwa wapi? vikao vya NEC na CC ya CCM viliivyo wajadili NAPE na SITTA taarifa zilikuwa zinamwagwa hapa wakati kikao kinaendelea watetezi wa usiri mlikuwa wapi?

Kumbe JF inakuwa nzuri pale inaposemwa na kukosolewa CCM tu na sio Chadema.
 
tatizo sio kutoa siri za chama ....tatizo ni namna alivyozitoa.
ametaja habari ya chacha wangwe baada ya kuonekana na yeye amefanyiwa spinning kama zile .....kwa maana hiyo hakuwa na nia ya kuzisema kama yasingemkuta na yeye.
amesema kuhusu habari ya mahesabu ya chama kwa sababu anataka kuwakomoa wengine ndani ya chama, baada ya yeye kuguswa na vitendo vyao
motive ya zitto ya kuanika siri za chama ndio inatutia wasiwasi.....na sio siri zenyewe


Ndio maana sasa nimeamini kwamba Chadema ni mkusanyiko wa wasanii, wahuni na mafisadi wenye malengo binafsi. Wanapozidiana kete na conflict kuibuka kama sasa ndio sisi tulio nje tunajua what does Chadema mean! Hii ni kesi ya ukimwaga mboga namwaga ugali lakini timing ni muhimu! Damn! CCM part two!
 
Kwa yaliyojili mpaka sasa inatosha kutambua kuwa Chadema si chama cha siasa, bali mkusanyiko wa wasanii na wahuni wenye malengo binafsi. I'm sorry to say sioni tofauti kati yake na CCM, in that sense sio chama mbadala! Kama Zitto kakiri kushiriki kumchongea shutuma Chacha Wangwe ni imani yangu kwamba kulikuwa na baraka za viongozi wenzie wa juu including wazee waasisi, kwa maana hiyo sidhani kama kuna msafi hapo! Kumtoa Zitto hakutasaidia kwa sababu uozo unaonekana haujaanzia kwake, ni wengi wameoza na tushukuru conflict zao zimeweza kutufumbua macho na kuona kwamba Chadema ni chama cha aina gani? Na kwanini unaita uozo kama huo siri za chama?Ooh My God, nani atatutoa kwenye utumwa wa CCM?

Mara zote ukifanya tendo la kishetani ,tatizo la shetani ni lazima aliweke hilo tendo wazi ukiwa bado hai,huwa anakufichia kwa mda tu.
 
Umesema sawia kabisa! watu wanataka Zitto awe kama punching bag kwa kupokea mashumbulizi tu bila kujibu. Hapa Kaja anaejiita Asha Abdallah na Mpaka Kieleweke ( mmoja mbunge na mwingine kiongozi mwandamizi wa Chadema) wamemtukana Zitto pamoja na mama yake. Zitto kaitwa fisadi mtoa na mpokea rushwa, mrokokaji nk hawa sio na wanachama wa kawaida bali viongozi wa chadema kubwa zaidi baba mkwe Mzee Mtei kanukuliwa na Nipashe akisema mafisadi wamepenyeza pesa kuharibu uchaguzi ( aki maanisha Zitto anatumiwa ) hayo yote yameanikwa hapa jamvini je mlitaka Zitto akawajibu wapi? je hao hawakuwa wanatoa siri?

Zitto yupo sahihi kwenye hili haya mambo ya kufuga ugonjwa mauti yatawafichua chama kinaendeshwa kibabe na kifamilia, watu wana shurutishwa kuondoa majina, bila haya Dr Slaa ( of all people ) anavunja uchaguzi wa vijana bila kufuata taratibu ( hana powers hizo ) halafu mnataka watu wakae kimya?

Hapa JF zimetungikwa nyaraka kadhaa wa kadhaa za siri za serikali na mikataba je watetezi wa siri mlikuwa wapi? vikao vya NEC na CC ya CCM viliivyo wajadili NAPE na SITTA taarifa zilikuwa zinamwagwa hapa wakati kikao kinaendelea watetezi wa usiri mlikuwa wapi?

Kumbe JF inakuwa nzuri pale inaposemwa na kukosolewa CCM tu na sio Chadema.

Mkuki kwa nguruwe mkuu wangu, kwa binadamu mchungu!
 
Wapi Bwana kama unakumbuka ya Chacha Wangwe na leo unasema utasahau baada ya uchaguzi, mimi naanza kukosa imani na wewe. maana si ya Wangwe yalikuwa yameshapita?
wewe hebu tupishe hapa.kwanza Chadema yenyewe huijui hata probation hujamaliza unajitia kimbele mbele au unafikiri cheo cha Zitto utapewa wewe?
UMESHINDWA KUISHI NA LIPUMBA utaweza hao wazee wa Machame? pole sana umeruka mkojo umekanyaga MAJITAKA.
 
Field Marshall Es,

Haya sasa unaingia na gear nyingine kabisa ktk kuspin issue tunayozungumzia.
Wapi Zitto kasema alishiriki ktk mbinu ya kumuua Wangwe?...hivi kweli wewe unamtendea haki au unamchulia zaidi!
Mimi ndo nimemuuliza Zitto atuambie kilichotokea haswa ikiwa yeye ameamua kusema ukweli wote na sikumaanisha kwamba Chadema na Zitto walifanya mbinu ya kumuua Wangwe. Nimetaka kujua ukweli wote maadam yeye kaamua kuanika kila kitu hapa JF.

Pili, unapotumia mtazamo wangu ni bora zaidi upinge hoja yangu kwa hoja siii swala la CCM na upuuzi wake. Nimesema vyama vyote duniani vinaweza kuengua jina la mtu hii haina maana Zitto alienguliwa kwa sababu hizo hizo. Ila nachosema Demokrasia ni pamoja na mgombea kukubali kutopitishwa jina lake la wazee wa baraza kutokana na katiba ya chama husika..Mtu yeyote anaweza chukua form ya kugombea Urais iwe Marekani, UK, Caanda na hata Uchina lakini jina lake linaweza enguliwa ikiwa mtu huyo hana sifa, hakutimiza masharti au amekiuka baadhi ya kanuni na sheria za uandikishaji.

Ni jambo la kawaida kabisa, na mtu kama Zitto alitakiwa kuwa mvumilivu, kuheshimu na kukubali matokeo au kufuatilia swala zima kwa kutumia misingi ya sheria inayoambatana na kukata rufaa au kutoa lawama zake. Mzee Malecela alifanya hivyo na heshima yangu kwake nitampa pale aliposindwa kukipaka chama kizima kwa sababu yeye kaenguliwa. Sikuandika kitu chochote kinachohusiana na ubabe wa CCM ila hekima alotumia Mzee Malecela na hata Mzee Sitta kuonyesha kukomaa kwa wanasiasa hao. Chama ni mjumuiko wa watu wa kila aina hivyo issue sio chama hapa ila mhusika anaweza vipi ku handle issues kama kiongozi alokomaa kifikra.

Mkuu wangu hapa tunazungumzia MTU na maamuzi yake na sio chama..Napinga sana yaliyomkuta mzee malecela kwa sababu naelewa kilichofanyika. Na napinga kuenguliwa kwa Zitto ktk kugombea Uenyekiti lakini maadam yeye alikubali kuondoa jina lake ina maana alikubali kujitoa kwa mujibu wa sheria au ushauri wa baadhi ya watu. Kitendo cha yeye kujitoa wakati bado akiwa na hasira inaonyesha wazi hakuwa mkweli.

Tofauti na Wangwe on the otherside alihakikisha haki yake anapewa na nadhani hata Zitto mwenyewe aliwahi kupinga kuwepo kwa njama dhidi ya Marehemu.. leo hii ndio kwanza tunajua ukweli wa mambo yote baada ya mkuu Zitto kupandisha mashetani yake.

Tatizo sii kuupata ukweli ila nashangaa tena kwamba huyu mtu siku zote alikuwa kimya wakati Wangwe akifanyiwa unyama wote na yeye mwenyewe anakiri kuwa mshirika, leo inatokea kwake ndio ukweli tunakuja upata akiwa mshirika wa mbinu chafu against Marehemu.
Ni mchanganyiko wa mambo yote haya ndipo napohoji dhumuni la mheshimiwa
Zitto kama kweli ni kwa maslahi ya chama au yake mwenyewe binafsi. Mandingo wanasema - Chicken has come home to roost! Ukiwa ktk mbinu ya kumuengua mtu ktk kiti cha makamu mwenyekiti, kumbuka malipo yake yanaweza kuwa hapa hapa duniani na hivyo kulalamika kwa Mheshimiwa Zitto hakuwezi kumsafisha hata kidogo ila kinaharibu jina zima la chama.

Wewe kama mwana CCM unafurahia haya yanayotokea na utasema sana kumwita Zitto a hero kwa sababu unataka Chadema wanakwisha..Siku zote wewe mwenyewe husema Siasa ni mchezo mchafu. Unaelewa fika rafu ambazo CCM hutumia na mara zote umekuwa nyuma ya rafu hizo ukiwaambia Chadema wao wanshindwa kipi kucheza rafu mpira wa mchangani usokuwa na refa.
Mimi sii mwanasiasa na nitasema ukweli kwamba ndio sababu kubwa inayonifanya nisiwe mwanasiasa kwa sababu Siasa ni UONGO unaokubalika. Ukiwa mkweli siku zote ktk siasa U will fail na hakuna kitu kibaya ktk makundi haya ya siasa kama Panya (rat) ambaye ni mwepesi wa kuropoka na kusema siri za chama ukidhani ndio ukweli...

Mkuu wangu tunazungumza kila siku na tunafahamiana zaidi ya miaka 30 lakini hata siku moja sijakusikia uki lalamika kuhusu mkeo au familia yako. Hii haina maana ndoa yako ni shwari lakini unajua fika kuwa mimi sii solution pamoja na kuwa mshikaji wako. Swala la ndoa yako ni nje ya ufahamu wangu kabisa isipokuwa tu pale panapojenga urafiki wetu na ndoa yako. Sitakiwi wala sipaswi kuelewa kitu kama kuna matatizo mazito, wapo watu na vyombo ambavyo vitaweza ku solve matatizo ya ndoa yako sii mimi..

Na kibaya zaidi ni pale utakapo nieleza ubaya wa mkeo tu ktk kila janga bila kutoa nafasi sawa kwa mkeo kujieleza. hapo utakuwa unaivunja ndoa wewe mwenyewe, njia nzuri na yenye suluhu ni pale pande mbili zitakapo shiriki ktk mazungumzo au upanisho wowote ule.

Zitto anapokuja hapa JF na kukipaka chama anategemea ku accomplish kitu gani?.. sisi tutamsaidia kipi haswa kama sii kuongeza chunvi ktk kidonda!..Mkuu wangu utu uzima ni pamoja na kuwa nahekima ya kupima uzito wa issue na ukaweza kuziwakilisha ipaswavyo. Uwezo huu Zitto hana na hakika ni moja ya sababu ambayo binafsi nisingempa nafasi ya kuongoza chama. Tabia hii pekee ni liability kwa chama na inaruhusiwa kabisa kumuengua mgombea pamoja na kwamba anweza kuwa na umaarufu kwani siri za Vatican hubakia Vatican..That is leadership hakuna unafiki.

MKANDARA KUMBUKA KUWA ZIITO HAKUONDOLEWA JINA LAKE NA VIKAO HALALI KIKATIBA NI WAZEE WANNE AMBAO HAWATAMBULIKI KISHERIA.MALECELA ALIZUILIWA NA KAMATI KUU CHOMBO KINACHOTAMBULIKA KISHERIA SIO KAMA HAWA WAZEE WA CHADEMA.

UNASEMA AWE MVULIVU HADI LINI? KAVUMILIA YEYE KUENGULIWA KINYUME NA KATIBA YA CHADEMA. AKALETA MGOMBEA UENYEKITI WA VIJANA AKASHINDA MATOKEO YAKE YAMEFICHWA NA HAO WAZEE SIO KAMATI KUU YA CHADEMA. BAADA YA HAPO ANAKUJA KUTUKANWA HUMU JF YEYE NA MZAZI WAKE. WEWE UNASEMA AWE MVUMILIVU.

NDUGU YANGU HUO UTAKUWA UZEZETA.ZITTO KAINGIA CHADEMA AKIWA NA MIAKA 16 HUKO BUSANDA KOTE KAPITA KUFANYA SHUGHULI YA CHAMA ANAKIJUA CHADEMA NDANI NJE.WEWE UTAKUWA UMEJIUNGA CHADEMA KUPITIA JF-INTERNET MWENZAKO YUKO KWENYE GROUNDS. NAOMBA MWACHE ACHA KUMSAKAMA.

UNASEMA OOH MBONA ALIKUBALI KUONDOA JINA LAKE, HAKUKUBALI KWA HIARI NI PALE TU ALIPOKUTANA NA HAWA WAZEE WANNE NA ZITTO ANAJUA KILICHOMTOKEA WANGWE BAADA YA KUWABISHIA HAO WAZEE WANNE. KWANINI ASICHUKUE TAHADHARI KWA KUONA BORA YA NUSU SHARI KULIKO SHARI KAMILI? AU ULITAKA ANG'ANG'ANIE YAMKUTE YA WANGWE? MAMA YAKE UNGEMLEA WEWE? mwache Zitto wetu.
 
Umesema sawia kabisa! watu wanataka Zitto awe kama punching bag kwa kupokea mashumbulizi tu bila kujibu. Hapa Kaja anaejiita Asha Abdallah na Mpaka Kieleweke ( mmoja mbunge na mwingine kiongozi mwandamizi wa Chadema) wamemtukana Zitto pamoja na mama yake. Zitto kaitwa fisadi mtoa na mpokea rushwa, mrokokaji nk hawa sio na wanachama wa kawaida bali viongozi wa chadema kubwa zaidi baba mkwe Mzee Mtei kanukuliwa na Nipashe akisema mafisadi wamepenyeza pesa kuharibu uchaguzi ( aki maanisha Zitto anatumiwa ) hayo yote yameanikwa hapa jamvini je mlitaka Zitto akawajibu wapi? je hao hawakuwa wanatoa siri?

Zitto yupo sahihi kwenye hili haya mambo ya kufuga ugonjwa mauti yatawafichua chama kinaendeshwa kibabe na kifamilia, watu wana shurutishwa kuondoa majina, bila haya Dr Slaa ( of all people ) anavunja uchaguzi wa vijana bila kufuata taratibu ( hana powers hizo ) halafu mnataka watu wakae kimya?

Hapa JF zimetungikwa nyaraka kadhaa wa kadhaa za siri za serikali na mikataba je watetezi wa siri mlikuwa wapi? vikao vya NEC na CC ya CCM viliivyo wajadili NAPE na SITTA taarifa zilikuwa zinamwagwa hapa wakati kikao kinaendelea watetezi wa usiri mlikuwa wapi?

Kumbe JF inakuwa nzuri pale inaposemwa na kukosolewa CCM tu na sio Chadema.

Ndio maana nimemshauri Zitto ajiunge na chama chenu cha mafisadi cha CCM - maana inaonekana mafisadi mnampenda sana Zitto leo na sio siku ile alipofichua siri zenu za kuuza nchi (Buzwagi).
 
Haya matokeo mgeyatangaza siku hiyo ,na si kuja kuyatangazia jf.

Mliyatangaza haya matokeo siku hiyo?? hapo ndipo tutaanza kushika mwongo.

Hatudanganyiki tena kauli mbiu kuelekea 2010

Ha ha ha ha .... wanaccm hamdanganyiki?

Mtadaganyika mara ngapi?

IPTL, Richmond, Buzwagi, Meremeta, Tangold, EPA, BOT, nk
 
MKANDARA KUMBUKA KUWA ZIITO HAKUONDOLEWA JINA LAKE NA VIKAO HALALI KIKATIBA NI WAZEE WANNE AMBAO HAWATAMBULIKI KISHERIA.MALECELA ALIZUILIWA NA KAMATI KUU CHOMBO KINACHOTAMBULIKA KISHERIA SIO KAMA HAWA WAZEE WA CHADEMA.

UNASEMA AWE MVULIVU HADI LINI? KAVUMILIA YEYE KUENGULIWA KINYUME NA KATIBA YA CHADEMA. AKALETA MGOMBEA UENYEKITI WA VIJANA AKASHINDA MATOKEO YAKE YAMEFICHWA NA HAO WAZEE SIO KAMATI KUU YA CHADEMA. BAADA YA HAPO ANAKUJA KUTUKANWA HUMU JF YEYE NA MZAZI WAKE. WEWE UNASEMA AWE MVUMILIVU.

NDUGU YANGU HUO UTAKUWA UZEZETA.ZITTO KAINGIA CHADEMA AKIWA NA MIAKA 16 HUKO BUSANDA KOTE KAPITA KUFANYA SHUGHULI YA CHAMA ANAKIJUA CHADEMA NDANI NJE.WEWE UTAKUWA UMEJIUNGA CHADEMA KUPITIA JF-INTERNET MWENZAKO YUKO KWENYE GROUNDS. NAOMBA MWACHE ACHA KUMSAKAMA.

UNASEMA OOH MBONA ALIKUBALI KUONDOA JINA LAKE, HAKUKUBALI KWA HIARI NI PALE TU ALIPOKUTANA NA HAWA WAZEE WANNE NA ZITTO ANAJUA KILICHOMTOKEA WANGWE BAADA YA KUWABISHIA HAO WAZEE WANNE. KWANINI ASICHUKUE TAHADHARI KWA KUONA BORA YA NUSU SHARI KULIKO SHARI KAMILI? AU ULITAKA ANG'ANG'ANIE YAMKUTE YA WANGWE? MAMA YAKE UNGEMLEA WEWE? mwache Zitto wetu.

Kuandika kwa CAPS kunamaanisha unashout --- au ndiyo unataka kujilipua mabomu? Watu kama wewe huwa siwaamini kabisa. Wakati mmoja unaongea na before u know it - booooom (suicide bombing).
 
Mara zote ukifanya tendo la kishetani ,tatizo la shetani ni lazima aliweke hilo tendo wazi ukiwa bado hai,huwa anakufichia kwa mda tu.

Yeah, kama lile la kusomea porraaaandi IT na kisha kuja Tanzania na kujaribu kumchafua Mwakyembe.
 
Peasant, Mkuu mbona unazungumza wewe tuu na kuamini unayoandika kama ndicho tulichiookuwa tukisema?..
Mkuu wangu kuna namna mbili hapa ya Usiri tunaozungumzia. Ikiwa kuna mbinu za kumwangusha Zitto au madudu yanafanywa na Baadhi ya viongozi wa chama, wanachama na kadhalika ndani ya Chadema, Zitto ni msomi anaelewa wapi pa kwenda...Tatizo la issue hii nzima ni pale Zitto anapochukua sheria mkononi kama vile anamkamata kibaka Kariakoo na kuanza kumtwanga magumi.
Hii haina maana yule kibaka hana makosa ila kuchukua sheria mkononi kinyume cha taratibu za chama ndicho tunachokizungumzia.
Bila shaka hii ni siri ya wao viongozi wa Chadema na ni Uozo mkubwa isipokuwa kwa mtu anayegombea Uenyekiti, na hasa inapokuwa wewe pia ni mhusika..Kitendo kama hiki tayari kinakuondolea uaminifu achana na madudu ya watu wengine.
Kwa maana nyingine tena ikiwa wewe Peasant ni mkweli na umeshikiri ktk kuiba au kumwibia mtu mali yake na unataka kujisafisha sehemu ya kwanza kwenda ni Polisi au kwa mhusika ukiwa na mali yako mkononi na ukawataja wote waliohusika kuiba mali ya mtu huyo... Kisha sheria itachukua mkondo wake na utakuwa tayari kuadhibiwa.. Nipo sawa mkuu wangu?

Tunachokiona hapa ni Zitto akitangaza wizi wa watu wengine ktk gazeti, na pale alipohusika anasema alikwenda omba msamaha maiti ikiwa ktk jeneza au sijui mara kabla (wakati gani hakuna anayejua) ni jambo ambalo hakuna kati yetu anayeweza kuhakikisha ilitokea hivyo,au ndio katika kukipaka anataka kuhakikisha kwamba kama kuna anguko lake ataondoka na wengi.. Kifupi hakuna mtu anayefahamu nini kusudio la Mheshimiwa na anapofanya hivyo atakisaidia vipi chama ikiwa mkuu huyu ameshindwa kusubiri mkutano wa Baraza kuu au Kamati kuu kuwakilisha malalamiko yake yooote.
Tena basi kubwabwaja kwa huyo mwandishi wa Daima - Kibanda kungempa Ushahidi tosha kabisa kuwakilisha hoja yake na na kuhakikisha Pasingetosha! Zipo njia ambazoi Zitto alitakiwa kuzifuata lakini sii kuanika madudu haya hapa JF..trust me, binafsi kuelewa tu kwamba alihusika na mbinu za kumwangusha Wangwe yaani tayari imenitisha zaidi.. Halafu mtu huyu ndiye anatakuwa Mwenyekiti!.. noo jamani, Zitto bado hajakomaa kabisa kisiasa ni kama JK mwaka 1995, mwaka 2005 akawawekea vikwazo CCM na kina Mkapa kwamba asipochaguliwa ataanika madudu yote ya CCM.. na kwa woga wao wakampitisha.. Na upande wa wananchi tukampa a blackmailer kura asilimia 80.
NDIVYO TULIVYO...
 
Pamoja na yote yanayotokea ndani ya CHADEMA lakini ni njia mojawapo ya kukomazwa. hakuna chama duniani ambacho hakijawahi kukumbwa na dhoruba wakati wa kujipambanua kati ya wanasiasa na wadandia siasa.

Hilary Clinton alipokuwa anamkaribia Obama kwa kura wazee wa chama hicho (super Delegate) kwanza walimsihi ajitoe alipokaza shingo wakalamzimshisha,lakini wapambe wake walipomchochea kuwa asijitoe, Super delegate wengi zaidi wakatangaza kumuunga mkono Obama kwa faida ya Chama chao. Clinton alisalimu Amri

kama chama ni chama cha wachaga ni chama gani hakina wachaga? ndani ya miaka kumi CCM imewahi kuongozwa na watunza hazina wachaga wawili. kwanza Sifa Swai na Salome Mbatia. kama wachaga ni watu hatari kuwa wanasiasa ni kwa nini CCM iliwapa madaraka makubwa sana ndani ya Chama chao?

Hivi CCM Moshi inaongozwa na Waluguru?

Zitto hana uzito huo kisiasa kama wengi wenu mnavyotaka kuonyesha. ushahidi wa kimazingira unaonyesha jamaa anashawishiwa zaidi na Viongozi waandamizi wa CCM kuliko wa chama chake.
CHADEMA haitasambaratika!!
 
Ndio maana nimemshauri Zitto ajiunge na chama chenu cha mafisadi cha CCM - maana inaonekana mafisadi mnampenda sana Zitto leo na sio siku ile alipofichua siri zenu za kuuza nchi (Buzwagi).
Kuna mafisadi kuliko chadema? imekuwaje uchaguzi wa vijana kura zimezidi?
 
Balantanda, naomba utuweke sawa hii story yako tarehe yake inachanganya kwani inaonekana niya 4/9/09 tuweke sawa tafadhari.

Mods tunashukuru kwa marekebisho yote tunaenda sawa.
Unaweza kusoma gazeti la Mwananchi lina habari nyingi za uchafu wa Chadema.gazeti hili lilikuwa beneti na Chadema Busanda au una shaka nalo?
 
Kuna mafisadi kuliko chadema? imekuwaje uchaguzi wa vijana kura zimezidi?

Mafisadi waliofilisi nchi kupitia Buzwagi, IPTL, EPA, na mengine ni CCM (just in case umesahau). hayo ya chadema na kura zao unaweza kuwauliza viongozi wa chadema.
 
Unaweza kusoma gazeti la Mwananchi lina habari nyingi za uchafu wa Chadema.gazeti hili lilikuwa beneti na Chadema Busanda au una shaka nalo?

Angalau sasa umeacha kutumia CAPS kwenye maandishi yako (maana ulianza kutishia usalama wa wananchi hapa). Huo uchafu ni pamoja na kutaka kuigeuza Tanzania kuwa nchi ya kiislam (Tanzanistan)?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom