Hahahahaaa bila kumsahau ESCORT 1,La Brujita,Barbarossa, Illovo,General Galadudu n.ksalamu zangu zimfikie ndugu cleverbright na GENTAMYCINE
Lol!Kutokana na kwamba Jumapili hii ni SIKU YA WAPENDANAO basi binafsi nimeona si vibaya nikionyesha MAHABA yangu ya ki Valentino kwa members hawa wa JF kwani hakika wamekuwa WAKINIKOSHA hasa kwa mambo mbalimbali:
FaizaFoxy
miss chagga
Vitaimana
Amavubi
mkolaj
Ila pia nisifiche kusema kuwa members ambao hata iweje siwezi kuwapa salamu zangu za Valentines hata iweje ije jua au mvua kutokana na sababu hata nisizozijua pia ni hawa:
Nifah
Mussolin5
UncleBen
mshana Jr
Victoire
Si vibaya na wewe ukachukua fursa hii kumtakia au kuwatakia Valentines njema members unaowapenda na kuwatunuku humu JF lakini pia unaruhusiwa kuwataja hata wale ambao hawatapata salamu zako za Valentines.
Karibuni.
uko deepLol!
Nilikuwa sijasoma hili...
Mimi hata iweje siwezi kuwatumia salamu mapopoma haya GENTAMYCINE idawa DuppyConqueror Carbondioxide el nino The bold kilimbamula
Naogopa kuweka list ya marafiki ninaowatumia salaam maana ni wengi nikisahau wengine itakuwa lawama.
Hapo umekosea mkuu....Niwatakie Siku njema ya Valentine hawa jamaa
GENTAMYCINE
La Brujita
General Galadudu
Galadudu
Carbondioxide
ESCORT 1
cleverbright
cc Nifah
Mhhhhhhh ngoja niandae popcorn kumsubiria La Brujita atakachojibu.Ahsanteni kwa kuja!Thank you 4 coming!
Hapo umekosea mkuu....
Halafu umesahau alivyokuwa anajiita mchungaji Illovo?
Hahahahahaa nikikumbuka vimbwanga vyake nacheka sana,hasa alivyokuwa anatafuta mchumba sijui mke.
Hahahahaa yule mchungaji mwenye vituko sijui kapotelea wapi na maandalizi ya harusi yake ambayo bado anatafuta mchumba imeishia wapi.daah kweli nimemsahau Illovo na Barbarosa
Juan Roman Requelme Aka La Brujita
Hahahahahaa aiseee wewe jamaa ni kiboko!Inawezekana labda umesahau ila Mchezaji aliyekuwa akiitwa na Waargentina La Brujita hakuwa Juan Roman Requelme bali alikuwa ni Kiungo aliyenisababisha na Mimi kula Hela za Ndondo wakati nikisoma Uganda baada ya kucheza kama yeye katika midfield hadi Waganda wakata nibadili Uraia ili nichezee timu yao ya Taifa ya Vijana mwaka 1999 ( wakati huo najua ulikuwa ndiyo kwanza upo katika beseni unaogeshwa ) lakini nikawaambia kuwa naipenda mno nchi yangu ya Tanzania na nikawakatalia. Huyu Kiungo anaitwa JUAN SEBASTIAN VERON. Ningesema niendelee na kucheza mpira nina uhakika ningeshindana sana na akina Pirlo, Xavi na Deco kwani nilikuwa na uwezo nao sawa ila basi tu Mfumo nao uliniathiri kuchanganya na njaa na mikwara ya Wazee kutaka nijali Masomo. Najua hii kitu Nifah atanibishia. Mkuu nilikuwa nafanya vitu ambavyo si Niyonzima au Kamusoko au Mkude au Ndemla wanaweza kufanya hasa sehemu ya Kiungo hasa cha chini na ndiyo maana nikiwaona vijana leo wanambwelambwela tu uwanjani huwa napatwa na hasira mno.
Hahahahahaa aiseee wewe jamaa ni kiboko!
Kumbe na wewe unaipenda Tanzania?Nilifikiri wewe ni Mtusti na unaipenda Rwanda KULIKOTUKUKA!
Sina cha kubisha kuhusu kiwango chako cha kusakata kabumbu ila hapo kwenye kushindana na Pirlo na Xavi?
ππ
Hahahahahaa hapana!Najua huwezi kuamini kuwa nilikuwa na uwezo sawa na akina Pirlo na Xavi kwakuwa wao wapo Italy na Spain huku humu nikipigika zangu Tandale Tanzania. Ila amini usiamini Watanzania niliosoma nao Bugema na Kabojja nchini Uganda miaka ya 1996 hadi 2001 na hasa wale tuliokuwa tukikutana katika UMISETTA za Uganda watakuambia shughuli yangu. Nilikuwa napigishwa dimba la chini au la juu halafu siku zingine namaliza mwenyewe au natupwa shavu la kulia na kushoto. Dada umenikumbusha mbali sana na laiti Wazazi wangu wasingenilazimisha nishike Masomo leo ningewaleteeni sana TUZO kama hizi za Mbwana Ally Samatta nyingi sana na kinachoniuma sasa ni kwamba nimeishika hiyo Elimu lakini sina UTAJIRI wowote japo nina hako Ka Degree kangu na kama mambo yakienda poa naweza mwaka huu au hata mwakani nikamaliza M.A. lakini najuta kuwa Msomi na kuachana na Mpira ambao ndiyo naamini UNGENITOA mno KIMAISHA. Huwa nasikia Uchungu mtu kama Ngassa au Samatta japo hawana ELIMU kama yangu lakini KIMAISHA na KIPESA wamenipiga GEPU kubwa sana na Mimi UTAJIRI wangu ni hivi VYETI tu vya UNIVERSITY lakini MFUKONI ni bonge la NGUMBARU. Kungekuwa kuna dawa ya kurudisha UMRI nyuma hakika ningeinunua ilia nirudishe kidogo tu mpaka miaka 17 kisha Watanzania muwe kila siku mnakuja kunipokea JNIA nikiwa na MATUZO mengi tu. Kiwango changu na Kipaji changu unaweza kukikuta kwa Ferminho au Viera au Gaucho. Naomba nitumie pia FURSA hii kuwaasa WAZAZI ambao naamini wengi mpo humu kuwa jaribuni basi KUHESHIMU interests za WATOTO wenu na muwape sapoti ili wafikie huko watakako. Watanzania leo mnalalamika kuwa ni Mbwana Samatta tu ndiyo kawatoa KIMASOMASO ila kama Washua zangu wangeniruhusu niendelee na KUCHEZA MPIRA na kwa Kiwango kile KIKUBWA nilichokuwa nacho Tanzania mngekuwa mnakula KUKU kwa MRIJA sasa. Na ulivyo mbishi kama SHIPA wewe Mwanamke najua na hii nayo UTANIBISHIA tu.