Tanzania chini ya CCM imeshindwa kabisa kukibadilisha kilimo cha wananchi wake. Nakiri kusema toka imepata uhuru wake mwaka 1961 imekuwa na wakulima wadogo wadogo wanaolima kwa kutumia jembe la mkono na mbolea ya kubahatisha miaka yote mpaka leo 2023.
Kilimo hicho ni kigumu sana kwani kinategemea mvua ambazo hazina uhakika. Mavuno ya kilimo hicho ni duni sana kiasi ambacho nguvu kubwa inatumika lakini mavuno hafifu na ndio maana watu wengi wanakimbia kilimo.
Tanzania kama tunataka tuondokane na bei ya vyakula kupanda ni lazima tubadili kilimo chetu tunatakiwa tufanye uwekezaji mkubwa kwenye kilimo. Kilimo kiwe cha kibiashara na cha zana za kisasa kama vile matrekta n.K. Badala ya majembe ya mikono.
Bila kufanya hivyo tutakuwa tunadanganyana tunaimba wimbo na kwa sasa kilimo chetu siyo tena uti wa mgongo tena.
Ukubwa wa wa mashamba siyo tija.
Wawekezaji siyo wa kutafuta Tanzania.
Tatizo kilimo kiliwekwa nje ya biashara.
Kilimo kingepewa hadhi ya biashara kingekua na kuboreka chenyewe.
NI TATIZO SANA ,
KULIMA SHAMBA KUBWA SANA
HALAFU KITAALAMU SANA,
HALAFU UKAVUNA SANA,
HALAFU UNAKUWA KWENYE SOKO FINYU SANA,
HALAFU UNAWAZA PA KWENDA KUTUPA MAZAO.
KABLA YA KULIMA CHOCHOTE KAMA HUJUI MAZAO UTAUZA WAPI , NA KWA FAIDA;
BASI KAMA NI GARI
UNAENDESHA,
UKIDHANI UNATUMIA GIA YA KWENDA MBELE,
JUA KUWA UMEINGIZA GIA ( R)
WARUDI NYUMA.
KILIMO KIWE BIASHARA.
NANI anaikumbuka GAPEX ? MUULIZENI METL (MO)
UNAPOKUWA ASALI?
PA KUUZA NI KULE,
UNALIMA ILIKI
SOKO LIKO HUKU
NK,NK,
SASA YAKHE WALIMA MAHINDI WATAKA UKAUZE KENYA?
MAHINDI YAKO FUGIA NG'OMBE MILIONI TANO HALAFU MAZIWA NA NYAMA KAUZE ULAYA NK.
MUIGENI ASASI.
NB UKUBWA WA MASHAMBA NA MATREKTA SIYO TIJA ,
TIJA UNACHOZALISHA
KINA MWISHO MWEMA?