Kuendelea kwa haya matukio. Kanisa Mjitathmini.

Kuendelea kwa haya matukio. Kanisa Mjitathmini.

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Kiukweli inatamausha sana kusikia haya matukio ya mara kwa mara yakijirudia ya unyanyaswaji Watoto na Watu ambao ilitarajiwa kuaminiwa na Jamii.

Hainiingii akilini ni kwa vipi Taasisi yenye Wasomi kushindwa kuweka mifumo ya kudhibitiana wao kwa wao...hivi mnashindwa vipi kutambua Mwenendo wa Mwenzenu anayekengeuka mpaka anafikia kufanya madhara makubwa?.

Hamuoni hii mbali na kuitia doa taasisi bali pia inazusha maswali mengi kwaJamii kufikiri labda yanayofanyika ni sehemu ya shughuli za taasisi hiyo?.

Kama nyie mnashindwa kuwa Viongozi kimbilio, na wa kuaminiwa mnataka Jamii imkimbilie nani sasa?.

Ipo haja kwa Uongozi mzima wa Kanisa kutoka mbele na kujitakasa kwa Jamii kuwa ni kwa nini tuendelee kuwaamini ikiwa Jamii haipo salama mikononi kwao?. Hebu mje na mpango utakaoonesha njia mtakazozitumia kuwahakikishia Jamii usalama wao mikononi kwenu.

Haitoshi tu Kanisa kusema inajitenga na muovu au Mkosaji, ni vyema sasa kusikia uwajibikaji wa Kanisa zima na si kufikiri kwamba kwa kutengana naye tu inatosha kurudisha imani ya Jamii, tofauti na hapo ni sawa tu na kuleta ngonjera zile zile zilizokwishazoeleka.

Au mnataka tufikie mahali Jamii iwasuse?.
 
Bora mitume na manabii walioibuka na maji na mafuta yao kuliko hao viongozi waliokuwa wakali kukemea dhambi siku hizi wanawaza mambo ya siasa tu huku wakiacha kukemea mmomonyoko wa maadili
 
Bora mitume na manabii walioibuka na maji na mafuta yao kuliko hao viongozi waliokuwa wakali kukemea dhambi siku hizi wanawaza mambo ya siasa tu huku wakiacha kukemea mmomonyoko wa maadili
Uwezi mkuta mwamposa au kuhani Musa kweny kashfa Kama hzi

Huwez mkuta mwamposa eti amegegeda watot sijui wahumini hapn uwezi mkuta

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Kiukweli inatamausha sana kusikia haya matukio ya mra kwa mara kwa kunyanyswa Watoto na Watu ambao ilitarajiwa kuaminiwa na Jamii.

Hainiingii akilini ni kwa vipi Taasisi yenye Wasomi kushindwa kuweka mifumo ya kudhibitiana wao kwa wao...hivi mnashindwa vipi kutambua Mwenendo wa Mwenzenu anayekengeuka mpaka anafikia kufanya madhara makubwa?.

Hamuoni hii pamoja na kuitia doa taasisi bali inazusha maswali mengi kwaJamii kufikiri labda yanayofanyika ni sehemu ya shughuli za taasisi yenu?.

Kama nyie mnashindwa kuwa Viongozi wa kuaminiwa mnataka Jamii imkimbile nani?.

Ipo haja kwa Uongozi mzima wa Kanisa kutoka mbele na kujitakasa kwa Jamii kuwa ni kwa nini tuendelee kuwaamini ikiwa Jamii hapo salama mikononi kwao?. mje na mpango utakaoonesha njia mtakazotumia kuwahakikishia Jamii usalama wao mikononi kwenu.

Haitoshi tu Kanisa kujitenga na muovu, ni vyema kusikia uwajibikaji wa Kanisa zima, tofauti na hapo ni sawa na kuleta ngonjera zilizozoeleka.

Au mnataka tufikie mahali Jamii iwasuse?.
Kanisa ni nini ewe mkurupukaji?
 
Unajuaje ? ng'ong'o unamlinda wewe
Yaani hata mke mwenyewe wa huyo Mwamposa (kama yupo), au mke wa huyo Kuhani Mussa wakiona huo ugoro alio uandika huyo jamaa, wanaweza kumchapa hata vibao!

Kama Gwaji Boy alifikia mpaka hatua ya kujirekodi video akikata viuno na kutoa miguno ya kutatanisha! Hivi mtu anapataje ujasiri wa kumuwekea dhamana mwanadamu ambaye anamuona kupitia luninga!! Siku wakipata kashfa hao Manabii wake, sijhi ataficha wapi sura yake.
 
Katika kanisa katoliki kuna vita kubwa ya madaraka na nafasi za kupiga pesa ndo maana wanatengenezeana hizo kesi, kurogana n.k. Wale jamaa ni mafia si mchezo ukizembea wanakufyeka kabisa. Kuna padre mmoja ni alikuwa classmate wangu, msomi na alikuwa akikubarika kwa askofu. Hakumaliza hata mwaka tangu apadrishwe akapata ajali. Namuonea sana huruma huyo Padre kwa zengwe alilotengenezewa.
 
Ahahaahah mamndenyi uwez mkuta mwamposa amegegeda mtot bana

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Mwamposa naye ni kama tu Mtu mwingine yeyote.

Kama vile ambavyo huwezi mdhania yule Daktari wa Hospitali unayotibiwa, au Mwalimu wa shule n.k.

Yote haya ni mpaka tu pale yanapotokea ndio wote sasa tunabaki kushika midomo kwa mshangao.

Haina maana kumshangaa Padri huku ukiona labda afadhali angekuwa Mtu mwingine...hakuna yeyote anayetazamiwa kufanya dhuluma kama hizo kwa Watoto.

Na kikubwa kinachonipa shida ni kuwa Mtuhumiwa huyu anaishi kwenye jumuia inayohusisha Wenzake, tena wengi kama sio wote ni Wasomi hata ani Wanasaikolojia.

Sasa ni kwa vipi wanashindwa kung'amua mwenendo wa kiovu wa anayeishi miongoni mwao?. hakika ni lazima kama Jamii kuilazimisha Taasisi hii kuja mbele na kuuelezea uma mikakati yao ya kuihakikishia Jamii usalama na watuambie ni kwa nini tuendelee kuwaamini.
 
Back
Top Bottom