Kufanya biashara kunafikirisha sana hasa ukiwa na mtaji mdogo unahitaji uwe na back-up usogee

Kufanya biashara kunafikirisha sana hasa ukiwa na mtaji mdogo unahitaji uwe na back-up usogee

Jumanne Mwita

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2014
Posts
530
Reaction score
1,446
Nimekaa nikatafakari sana haya maisha kila biashara nikipanga niifanye naona mtaji haukidhi yaani hautoshi. Naona dhahiri kabisa naenda kuanguka maana life mtaani ndio usiseme hakuna hela na mzunguko umekuwa mdogo sana kwa baadhi ya watu wanaofanya biashara.

Niliwaza nifanye biashara ya Hardware kuja kuuliza mtaji wa kuanza nao nikaona labda barbershop napo kuja kuambiwa mtaji nikasema labda ninunue mazao napo muda wa kusubili besa ikae stoo mwishoe bei ishuke uambulie kuuza kwa hasara yaani kiujumla biashara kwa sasa ni ngumu hasa kama uwe unataka kuanza au unatafuta biashara ya kukulipa hapo hutaweza kama unahela ya mawazo kama mimi.

Kitu nilichojifunza hasa watu wanaofanya biashara wengi wanafanya biashara kama mali kauli unakuta mtu mtaji wake ni 100m mtaji mwingine ni malikauli kama 250m+ hii inamsadia kuzungusha hapa na pale na kumfanya aweze kurudisha kidogokidogo yaani ni kama anamsaidia kumuuzia yule mwenye mtaji wa 250m+ baada ya hapo ataagiza na kupewa mzigo mwingine yaani anafanya kupokea mzigo bila kumalizia malipo baadae atakapo agiza ndio analipa ya nyuma anaendelea muda huo analetewa mwingine hii inawasaidia wengi wafanyabiashara wengi tunaona wanamitaji mikubwa kumbe wanawafanyia wengine kinachombeba ni jina na wateja ambao amejikusanyia hapo anakuwa na uhakika wa kuchukua mzigo na kuuza na kurejesha na kuomba mzigo tena

Mwaka 2019 hadi 2020 nilikuwa Kasulu katika heka heka za utafutaji nilijenga mazoea na jamaa mmoja mfanya biashara aliniamini sana mpaka kufikia kunipa siri hii hata yeye alisema siyo kila mtu namwambia hili ila sababu tumeshibana ngoja ni kwambie.

Aliniambia mengi ila kuna hili aliniambia ukweli kuhusu hicho nilichoelezea hapo juu. Akasema Jumanne unajua sii wote tunamitaji humu mjini sema tunawatu ambao tunafahamiana nao kule mzigo unapozalishwa hivyo wao wanatuamini na kututumia mzigo mimi nalipia usafiri tu. Ila mzigo natumiwa bure, nikiuza narudisha hela yake ile faida naongezea kwenye mtaji ukiisha tena namwambia nashushiwa hapa semi full mkoko napakua mzigo mwingine naweka stoo mtu akija hapa anajua mzigo wote wangu na sifa ananimwagia kumbe haujui nachofanya kwenye biashara.

Sasa wewe mwenzangu na mimi unatanga tanga na mtaji wa million 6 sijui 3 unategemea nani atakuamini akupe mali baadae urejeshe akupe tena mzigo. Hilo ni gumu kama huna connection na tajiri mwenye mtaji, hii nimeitafakali sana leo kila nikigusa namna ya kutoka naona kila njia ngumu yaani life kwa wengine sisi tulikuja kushuhudia ulimwengu baadae tufe tuache lawama hakuna namna maana huna wa kusema hapa nakwama ngoja nikamuone flani hamna ni wewe na roho yako tu.

Ukirudi nyuma wengine wazazi wanategemea utoboe waponee hapo wao walipambana lakini riziki ikawa siyo bahati kwao hivyo tegemeo kubwa limebakia kwa watoto wao na wao wajaribu, na sisi tunajaribu lakini wapi!

Kama unarafiki au ndugu ambae ukimueleza shida yako au changamoto yeyote mnaibeba kama wote basi shukuru sana na ombea M/Mungu asije kutenganisha ukaribu huo au undugu wenu.
 
Akasema Jumanne unajua sii wote tunamitaji humu mjini sema tunawatu ambao tunafahamiana nao kule mzigo unapozalishwa hivyo wao wanatuamini na kututumia mzigo mimi nalipia usafiri tu. Ila mzigo natumiwa bure, nikiuza narudisha hela yake ile faida naongezea kwenye mtaji ukiisha tena namwambia nashushiwa hapa semi full mkoko napakua mzigo mwingine naweka stoo mtu akija hapa anajua mzigo wote wangu na sifa ananimwagia kumbe haujui nachofanya kwenye biashara
Hili ni kweli kabisa kwA maana mama yangu anauza duka la rejareja kipindi anaanza hii biashara alijenga ukaribu na mwenye duka la jumla kiasi anatumiwa mizigo anauza kisha anarudisha hela ya mzigo baada ya kuuza na kupata faida
 
Dah,juzi ndugu yangu katoka kuniambia hii issue.Nikabaki nashangaa."hivi we mkabasia unategemea utajaza lini duka kama Kila siku unaenda kutoa hela cash kwenye maduka ya jumla"Akanishauri tafuta duka ulilozoea wakupe mzigo then waambie baada ya week mbili utawapa pesa Yao.
 
Wenye ndugu wahivi washukuru sana maana ukiwa na ndugu wenye wivu hawataki uwapite ni shida sana
Hey we mkaka mbona kama unajikatisha tamaa mwenyew, acha kuwaza mitaji Anza na ichoicho ulichonacho, apo kwenye hardware ulikua na shingap ambayo uliona haitoshi?

Ngoja nikupe summary kidogo Mimi nimemaliza chuo mwaka Jana nilikua na mil Moja tu kesh na pia Kuna mtu nilikua namdai lak tatu, baada ya kumaliza chuo nikarud Kijijin, sehemu nilipo Kuna Barabara na pia ndio Kijiji kinakua, nilichofanya baada ya kufika nilitafuta wakala wa cement nikaanza kuagiza nilianza na cement 50 tu ambayo haifiki ata milioni, Ile lak tatu nikaangaikia flemu, nilianza mwaka Jana na mpaka Sasa ninauza cement, chokaa, misumari, PVC, sinks na vingine vidogovidogo,

Shida ni kua wewe unaonekana unaogopa kuanza haya maisha yanataka kujiamin sio kufanya tathmin kwa kitu ambacho hujafanya..

Jitaidi pia kufanya biashara kwenye vijiji ambavyo ndio vinakua sio kujazana mijini..
 
Ukianza biashara ikawa inatoka vizuri mzigo hauchukui mda unaagiza tena wale wanaojumuisha wao wenyewe wanaanza kukushawish uchukue mzigo mpya ulipie ukishauza, Aya mambo yote utayakuta ukishaungia kwenye mfumo

Bila ata kujipendekeza kwa supplier wanakutafuta wenyewe, unatakiwa kuingia kwanza kwenye biashara Kila kitu utajifunza uko.
 
Hey we mkaka mbona kama unajikatisha tamaa mwenyew, acha kuwaza mitaji Anza na ichoicho ulichonacho, apo kwenye hardware ulikua na shingap ambayo uliona haitoshi?

Ngoja nikupe summary kidogo Mimi nimemaliza chuo mwaka Jana nilikua na mil Moja tu kesh na pia Kuna mtu nilikua namdai lak tatu, baada ya kumaliza chuo nikarud Kijijin, sehemu nilipo Kuna Barabara na pia ndio Kijiji kinakua, nilichofanya baada ya kufika nilitafuta wakala wa cement nikaanza kuagiza nilianza na cement 50 tu ambayo haifiki ata milioni, Ile lak tatu nikaangaikia flemu, nilianza mwaka Jana na mpaka Sasa ninauza cement, chokaa, misumari, PVC, sinks na vingine vidogovidogo,

Shida ni kua wewe unaonekana unaogopa kuanza haya maisha yanataka kujiamin sio kufanya tathmin kwa kitu ambacho hujafanya..

Jitaidi pia kufanya biashara kwenye vijiji ambavyo ndio vinakua sio kujazana mijini..
Hongera Sana kwa kuthubutu
 
Ukianza biashara ikawa inatoka vizuri mzigo hauchukui mda unaagiza tena wale wanaojumuisha wao wenyewe wanaanza kukushawish uchukue mzigo mpya ulipie ukishauza, Aya mambo yote utayakuta ukishaungia kwenye mfumo

Bila ata kujipendekeza kwa supplier wanakutafuta wenyewe, unatakiwa kuingia kwanza kwenye biashara Kila kitu utajifunza uko.
Nakupongeza sana. Uaminifu ni mtaji wa kwanza. Na ukizidi kukua kuna michongo mingi zaidi itakufuata zaidi ya hayo mambo ya mali kauli. Kuna ruzuku za serikali na mikopo yenye masharti nafuu ambayo ili uipate lazima wenye mamlaka wakuelewe pia. Kina Mo na Bahkresa wanapewagwa sana madili na serikali.
 
Hey we mkaka mbona kama unajikatisha tamaa mwenyew, acha kuwaza mitaji Anza na ichoicho ulichonacho, apo kwenye hardware ulikua na shingap ambayo uliona haitoshi?

Ngoja nikupe summary kidogo Mimi nimemaliza chuo mwaka Jana nilikua na mil Moja tu kesh na pia Kuna mtu nilikua namdai lak tatu, baada ya kumaliza chuo nikarud Kijijin, sehemu nilipo Kuna Barabara na pia ndio Kijiji kinakua, nilichofanya baada ya kufika nilitafuta wakala wa cement nikaanza kuagiza nilianza na cement 50 tu ambayo haifiki ata milioni, Ile lak tatu nikaangaikia flemu, nilianza mwaka Jana na mpaka Sasa ninauza cement, chokaa, misumari, PVC, sinks na vingine vidogovidogo,

Shida ni kua wewe unaonekana unaogopa kuanza haya maisha yanataka kujiamin sio kufanya tathmin kwa kitu ambacho hujafanya..

Jitaidi pia kufanya biashara kwenye vijiji ambavyo ndio vinakua sio kujazana mijini..
Nakazia ujumbe wako mkuu, mleta mada auchukue huu ushauri wako aufanyie kazi
 
Hey we mkaka mbona kama unajikatisha tamaa mwenyew, acha kuwaza mitaji Anza na ichoicho ulichonacho, apo kwenye hardware ulikua na shingap ambayo uliona haitoshi?

Ngoja nikupe summary kidogo Mimi nimemaliza chuo mwaka Jana nilikua na mil Moja tu kesh na pia Kuna mtu nilikua namdai lak tatu, baada ya kumaliza chuo nikarud Kijijin, sehemu nilipo Kuna Barabara na pia ndio Kijiji kinakua, nilichofanya baada ya kufika nilitafuta wakala wa cement nikaanza kuagiza nilianza na cement 50 tu ambayo haifiki ata milioni, Ile lak tatu nikaangaikia flemu, nilianza mwaka Jana na mpaka Sasa ninauza cement, chokaa, misumari, PVC, sinks na vingine vidogovidogo,

Shida ni kua wewe unaonekana unaogopa kuanza haya maisha yanataka kujiamin sio kufanya tathmin kwa kitu ambacho hujafanya..

Jitaidi pia kufanya biashara kwenye vijiji ambavyo ndio vinakua sio kujazana mijini..
Nimekuelewa ingawa wengi tunauoga mno maana ukisema uanze mtaji wenyewe unaona kama hautoshi ila kwa ujumbe huu nimechukua jambo asante sana 🤝🤝
 
Hey we mkaka mbona kama unajikatisha tamaa mwenyew, acha kuwaza mitaji Anza na ichoicho ulichonacho, apo kwenye hardware ulikua na shingap ambayo uliona haitoshi?

Ngoja nikupe summary kidogo Mimi nimemaliza chuo mwaka Jana nilikua na mil Moja tu kesh na pia Kuna mtu nilikua namdai lak tatu, baada ya kumaliza chuo nikarud Kijijin, sehemu nilipo Kuna Barabara na pia ndio Kijiji kinakua, nilichofanya baada ya kufika nilitafuta wakala wa cement nikaanza kuagiza nilianza na cement 50 tu ambayo haifiki ata milioni, Ile lak tatu nikaangaikia flemu, nilianza mwaka Jana na mpaka Sasa ninauza cement, chokaa, misumari, PVC, sinks na vingine vidogovidogo,

Shida ni kua wewe unaonekana unaogopa kuanza haya maisha yanataka kujiamin sio kufanya tathmin kwa kitu ambacho hujafanya..

Jitaidi pia kufanya biashara kwenye vijiji ambavyo ndio vinakua sio kujazana mijini..
Uoga wa kuanza unatukwamisha wengi. Umenifundisha kitu.
 
Nakupongeza sana. Uaminifu ni mtaji wa kwanza. Na ukizidi kukua kuna michongo mingi zaidi itakufuata zaidi ya hayo mambo ya mali kauli. Kuna ruzuku za serikali na mikopo yenye masharti nafuu ambayo ili uipate lazima wenye mamlaka wakuelewe pia. Kina Mo na Bahkresa wanapewagwa sana madili na serikali.
Taasisi gani inatoa hii mikopo?

#YNWA
 
Hey we mkaka mbona kama unajikatisha tamaa mwenyew, acha kuwaza mitaji Anza na ichoicho ulichonacho, apo kwenye hardware ulikua na shingap ambayo uliona haitoshi?

Ngoja nikupe summary kidogo Mimi nimemaliza chuo mwaka Jana nilikua na mil Moja tu kesh na pia Kuna mtu nilikua namdai lak tatu, baada ya kumaliza chuo nikarud Kijijin, sehemu nilipo Kuna Barabara na pia ndio Kijiji kinakua, nilichofanya baada ya kufika nilitafuta wakala wa cement nikaanza kuagiza nilianza na cement 50 tu ambayo haifiki ata milioni, Ile lak tatu nikaangaikia flemu, nilianza mwaka Jana na mpaka Sasa ninauza cement, chokaa, misumari, PVC, sinks na vingine vidogovidogo,

Shida ni kua wewe unaonekana unaogopa kuanza haya maisha yanataka kujiamin sio kufanya tathmin kwa kitu ambacho hujafanya..

Jitaidi pia kufanya biashara kwenye vijiji ambavyo ndio vinakua sio kujazana mijini..
Na mim nikazie hapo aache uogaa hata mim mwaka wa jana nilikuwa na mtaji wa takriban 1•5 million hivi kwenye kuuza spare za pikipik huko vijijin, Basi bhana wakapita wale watu wa masoko wa SLL nikawa nachukua mali kauli Yan hata mzigo wa million mbili. Nilichokuwa nafanya kila wiki baada ya mauzo lazima niende mjini ili nitumie pesa marejesho. Yan nikafanya hivyo mpaka nilipojipata. Namshukuru mungu mtaji wangu unakaribia 12M kwa Sasa. Nilichojifunza sisi vijana tujitahid tuwe waaminifu Ili tuweze kutoboa lakin pia anza ulipo!...
 
Back
Top Bottom