Kufanya biashara kunafikirisha sana hasa ukiwa na mtaji mdogo unahitaji uwe na back-up usogee

Kufanya biashara kunafikirisha sana hasa ukiwa na mtaji mdogo unahitaji uwe na back-up usogee

Na mim nikazie hapo aache uogaa hata mim mwaka wa jana nilikuwa na mtaji wa takriban 1•5 million hivi kwenye kuuza spare za pikipik huko vijijin, Basi bhana wakapita wale watu wa masoko wa SLL nikawa nachukua mali kauli Yan hata mzigo wa million mbili. Nilichokuwa nafanya kila wiki baada ya mauzo lazima niende mjini ili nitumie pesa marejesho. Yan nikafanya hivyo mpaka nilipojipata. Namshukuru mungu mtaji wangu unakaribia 12M kwa Sasa. Nilichojifunza sisi vijana tujitahid tuwe waaminifu Ili tuweze kutoboa lakin pia anza ulipo!...
Uaminifu ndo silaha ya mafanikio..bahati mbaya wabongo uaminifu hatuna na ni ngumu tajiri kukuamini ndo mana wanasemaga matajiri wana roho mbaya kwa watu wanaojitafuta ila ni kwasababu kuna sehem walipigwa kwa watu waliokosa uaminifu wakawa wabinafsi.. unampa mtu mzigo kwa mali kauli anauza hakupi pesa anakimbia au anakulipa kwa kuchelewa mno ili hali ashauza.
 
Nimekaa nikatafakari sana haya maisha kila biashara nikipanga niifanye naona mtaji haukidhi yaani hautoshi. Naona dhahiri kabisa naenda kuanguka maana life mtaani ndio usiseme hakuna hela na mzunguko umekuwa mdogo sana kwa baadhi ya watu wanaofanya biashara.

Niliwaza nifanye biashara ya Hardware kuja kuuliza mtaji wa kuanza nao nikaona labda barbershop napo kuja kuambiwa mtaji nikasema labda ninunue mazao napo muda wa kusubili besa ikae stoo mwishoe bei ishuke uambulie kuuza kwa hasara yaani kiujumla biashara kwa sasa ni ngumu hasa kama uwe unataka kuanza au unatafuta biashara ya kukulipa hapo hutaweza kama unahela ya mawazo kama mimi.

Kitu nilichojifunza hasa watu wanaofanya biashara wengi wanafanya biashara kama mali kauli unakuta mtu mtaji wake ni 100m mtaji mwingine ni malikauli kama 250m+ hii inamsadia kuzungusha hapa na pale na kumfanya aweze kurudisha kidogokidogo yaani ni kama anamsaidia kumuuzia yule mwenye mtaji wa 250m+ baada ya hapo ataagiza na kupewa mzigo mwingine yaani anafanya kupokea mzigo bila kumalizia malipo baadae atakapo agiza ndio analipa ya nyuma anaendelea muda huo analetewa mwingine hii inawasaidia wengi wafanyabiashara wengi tunaona wanamitaji mikubwa kumbe wanawafanyia wengine kinachombeba ni jina na wateja ambao amejikusanyia hapo anakuwa na uhakika wa kuchukua mzigo na kuuza na kurejesha na kuomba mzigo tena

Mwaka 2019 hadi 2020 nilikuwa Kasulu katika heka heka za utafutaji nilijenga mazoea na jamaa mmoja mfanya biashara aliniamini sana mpaka kufikia kunipa siri hii hata yeye alisema siyo kila mtu namwambia hili ila sababu tumeshibana ngoja ni kwambie.

Aliniambia mengi ila kuna hili aliniambia ukweli kuhusu hicho nilichoelezea hapo juu. Akasema Jumanne unajua sii wote tunamitaji humu mjini sema tunawatu ambao tunafahamiana nao kule mzigo unapozalishwa hivyo wao wanatuamini na kututumia mzigo mimi nalipia usafiri tu. Ila mzigo natumiwa bure, nikiuza narudisha hela yake ile faida naongezea kwenye mtaji ukiisha tena namwambia nashushiwa hapa semi full mkoko napakua mzigo mwingine naweka stoo mtu akija hapa anajua mzigo wote wangu na sifa ananimwagia kumbe haujui nachofanya kwenye biashara.

Sasa wewe mwenzangu na mimi unatanga tanga na mtaji wa million 6 sijui 3 unategemea nani atakuamini akupe mali baadae urejeshe akupe tena mzigo. Hilo ni gumu kama huna connection na tajiri mwenye mtaji, hii nimeitafakali sana leo kila nikigusa namna ya kutoka naona kila njia ngumu yaani life kwa wengine sisi tulikuja kushuhudia ulimwengu baadae tufe tuache lawama hakuna namna maana huna wa kusema hapa nakwama ngoja nikamuone flani hamna ni wewe na roho yako tu.

Ukirudi nyuma wengine wazazi wanategemea utoboe waponee hapo wao walipambana lakini riziki ikawa siyo bahati kwao hivyo tegemeo kubwa limebakia kwa watoto wao na wao wajaribu, na sisi tunajaribu lakini wapi!

Kama unarafiki au ndugu ambae ukimueleza shida yako au changamoto yeyote mnaibeba kama wote basi shukuru sana na ombea M/Mungu asije kutenganisha ukaribu huo au undugu wenu.
Ningependa kutia neno hapo. Yote hayo ni ukweli kabisa..Ila naomba nitoe mfano hapa..moja ya biashara yangu ni maziwa...mtaji wangu kusema ukweli ni milioni +,japo hapo mwanzo ulikuwa mdogo sana...kutokana na kuaminika na kudumu kwenye biashara kwa muda mrefu naletewa maziwa na wakulima tena sio kwa kubembeleza..mwanzo nilikuwa nanunua Lita kumi Hadi kumi na Tano. Ila biashara ilianza kukaa sawa nikawa naagiza Lita ishirini ndipo boss mwenye ng'ombe wake aliponiona mm nimteja wake potential na akaanza kunipa maziwa hata kama sinapesa anaamini nitamlipa.baada ya mwezi tulikaa chini tukaweka makubaliano..Mana hata kipindi maziwa ni adimu atatafuta kwa wakulima wengine ili tu nisikose mzigo..sasa imefika hatua napokea mpaka Lita sitini..Mana naanza kuuza jumla kwa wengine wanaofanya biashara..hivyo hiyo m6 ni nyingi sana Ila Anza chini.. biashara ni chain
 
Lengo la biashara ni mauzo.. supplier au manufacturer yeye anachotaka ni bidhas zake ziuzike..kama wewe mfanyabiashara utakuwa na wateja wa uhakika na cash flow nzuri..hata mtaji wako uwe mdogo kiasi gani..jua kuwa lazma uzingatiwe.. biashara ni uwakala.
 
Dah yan nmepata hasira huu uzi member wawili wanasema walianza na mtaji wa Mil 1, hv ni kismati au nishafanya zaidi ya biashara 5 za mtaji wa zaidi ya huo holaa hadi naogopa biashara! ajira nayo miyeyusho kweli. Mtu hupigi hatua
 
Unampa mtu hela ndio anaona shida zake ni kubwa kuliko zako.
Mil 6 uliyonayo ni kubwa sana kama hautajilinganisha na mtu.
Wewe nunua kwa hao wenye mtaji wa kati na uza, faida irudishe kwenye mzunguko na ndani ya miaka mitano utaingia kwenye system na wao wakuunganishe na matajiri.
Maisha ni mipango na sio shortcut.
 
ukiifananisha ukurasa wako wa kwanza kwenye biashara na mwingine aliyeko ukursa wa katikakati utakata tamaa. Anza hayo mengine yatajipa huko mbele
 
K
Dah yan nmepata hasira huu uzi member wawili wanasema walianza na mtaji wa Mil 1, hv ni kismati au nishafanya zaidi ya biashara 5 za mtaji wa zaidi ya huo holaa hadi naogopa biashara! ajira nayo miyeyusho kweli. Mtu hupigi hatua
una kitu hukufanya kwa usahihi
 
Dah yan nmepata hasira huu uzi member wawili wanasema walianza na mtaji wa Mil 1, hv ni kismati au nishafanya zaidi ya biashara 5 za mtaji wa zaidi ya huo holaa hadi naogopa biashara! ajira nayo miyeyusho kweli. Mtu hupigi hatua
Ndugu yangu kila kitu ni mikakati asikwambie mtu, Fanya tafiti sahihi katika hizo biashara unazofanya mfano wateja wako wanahitaji nin? Na maboresha pamoja unbunifu wa hapa na pale, Bila kusahau uaminifu kwa wateja wako na kwa wale utakaochukua mizigo ya jumla kwao!...
..
 
Ndugu yangu kila kitu ni mikakati asikwambie mtu, Fanya tafiti sahihi katika hizo biashara unazofanya mfano wateja wako wanahitaji nin? Na maboresha pamoja unbunifu wa hapa na pale, Bila kusahau uaminifu kwa wateja wako na kwa wale utakaochukua mizigo ya jumla kwao!...
..
Nashkuru Mkuu, 100% 🤝
 
Screenshot_20250112-223137.png
 
BUSINESS BENEFITS MORE THAN EMPLOYMENTS DO/ BIASHARA INA FAIDA ZAIDI YA AJIRA
 
Back
Top Bottom