Kufariki kwa Mwandishi wa Habari Makubo; Je kuna mkono wa mtu?

Kufariki kwa Mwandishi wa Habari Makubo; Je kuna mkono wa mtu?

Poleni sana ndg wa marehemu,Mungu ailaze roho ya Makubo mahala pema peponi,mchango wako na watetezi wengine hautasahaulika milele...kama stan katabalo....wewe ni shujaa wa mapinduzi ya kifikra....
 
Let's put the record very clear. Mwandishi aliyesimama kidete kufichua matatizo na North Mara ni Jacob Mugini wa Daily News. Ilifikia hatua marehemu na mwenzake aittwaye Samson Chacha aka Nyoka, wakamchukia Mugini na hata vkumripoti kwa Teweli Teweli kwamba hakuwaq upande wao.

Mwanzoni alikuwa mwandishi mahiri kwenye miaka ya 2000 hadi 2005 baada ya hapo akawa upande wa Mgodi. Mungu ailaze mahali pema peponi-Amina
 
Mungu ametoa na ametwaa.
Poleni sana wanafamilia ya Makubo
 
Awali - kuna habari kuwa mwandishi wa habari wa Tarime ambaye amehusika sana kwenye kutoa habari za uchafuzi wa mazingira uliofanywa na kampuni za madini tarime amefariki dunia kwa ugonjwa wa moyo (moyo umepasuka).

Update:

Kuna taarifa nilizopata muda mfupi uliopita kuwa familia ya marehemu Makubo inahisi kuwa kuna mkono wa mtu umehusika kwenye kifo cha ghafla na cha mazingira ya kutatanisha cha ndugu yao.

Inasemekana kuwa mazishi hayatafanyika mpaka uchunguzi maalumu ufanyike kuhusu kifo cha Makubo.

Zaidi ya yote - RIP Haruni Makubo.

Watu wa Tarime na watanzania wamepoteza mtu muhimu sana kwenye vita ya kutafuta haki dhidi ya kampuni kubwa la madini.

Mkuu Solomon,

huo uchunguzi umeshafanyika? nini kimepatikana? marehemu amezikwa?

RIP Makubo
 
pole shujaa upumzike kwa amani. Kwani ujasiri ni ghali tukumbuke mwandishi aliyefichua ya Loliondo walimfanyaje. Hii ni serikali ya watawala na sio wanachi.
 
Mwenyezi Mungu atawapa subira familia ya marehemu.
Lakini kwa kawaida huwa tunasema msiba usiwe na maeno maneno, lakini kwa kweli huo utamaduni utatufikisha pabaya huko tuendako. Pamoja na imani kutuambia kwamba kila nafsi itaonya mauti, bado tusikubali kila kitu kipite tu hivi hivi. Lazima tuangalie mapana.


Kwa taarifa rasmi ni kwamba:
-Makubo alikuwa mmoja wa waandishi waliohusika na waliokuwa wakiendelea kuchunguza athari za kemikali mgodini Tarime
-Makubo alikwisha kupata ruzuku ya fedha kutoka Tanzania Media Fund (TMF) kwa ajili ya kufanikisha uchunguzi zaidi kuhusiana na athari hizo na alikuwa ndio kwanza ameanza

Kutokana na hayo, si busara hata kidogo kufungwa midomo kujadili mazingira ya kifo na tahadhari kwa wengine. HILI NI JAMBO LA MUHIMU KABISA SI MZAHA TENA
 
Last edited:
Mwenyezi Mungu atawapa subira familia ya marehemu.
Lakini kwa kawaida huwa tunasema msiba usiwe na maeno maneno, lakini kwa kweli huo utamaduni utatufikisha pabaya huko tuendako. Pamoja na imani kutuambia kwamba kila nafsi itaonya mauti, bado tusikubali kila kitu kipite tu hivi hivi. Lazima tuangalie mapana.


Kwa taarifa rasmi ni kwamba:
-Makubo alikuwa mmoja wa waandishi waliohusika na waliokuwa wakiendelea kuchunguza athari za kemikali mgodini Tarime
-Makubo alikwisha kupata ruzuku ya fedha kutoka Tanzania Media Fund (TMF) kwa ajili ya kufanikisha uchunguzi zaidi kuhusiana na athari hizo na alikuwa ndio kwanza ameanza

Kutokana na hayo, si busara hata kidogo kufungwa midomo kujadili mazingira ya kifo na tahadhari kwa wengine. HILI NI JAMBO LA MUHIMU KABISA SI MZAHA TENA

NI MASIKITIKO! LAKINI TUMUOMBEE KWA MUNGU APATE PUMZIKO LA AMANI:
Kwa Mara ya mwisho wakati marehemu ameugua homa, aliwasiliana uongozi na Mhariri wa Gazeti la kanda ya Ziwa la Matukio Daima akiomba kusaidia kuchapisha habari yake ya UCHUNGUZI JUU YA ATHARI YA SUMU KATIKA MGODI HUO WA NORTH MARA kwani alidai kuwa Alikuwa 'AKIHISI' kuwa huenda chombo alichokuwa akifanyia kazi (HABARI LEO) kulikuwa na mtu ambaye alikuwa na mawasiliano ya karibu kabisa na Ofisa mmoja wa Mgodi aliyemtaja kwa jina la Tewel tewel na kwamba kulikuwa na mkakati wa kuzuia story yake isitumeke gazetini.

MAKUBO alikuwa ni miongoni mwa waandishi wa habari ambao walikuwa katika timu ya waandishi wa habari za uchunguzi wa habari za Migodi nchini ambayo ilianzishwa chini ya shirika la NOrwegian Church mwaka jana.
 
Back
Top Bottom