kufeli kwangu form 4 haimaanishi sina akili

elias godfrey

Member
Joined
Oct 13, 2012
Posts
35
Reaction score
6
mimi ni kijana niliemaliza form 4 last yr na matokeo yamekuja nimefeli vibaya mno i dont know why naamini wa kulaumiwa ni serikali kwa kutosahiisha vizuri halafu wanasema wanaunda tume sasa tume ya nn kila kitu kipo wazi sawa wanasema facebook na twitter ndio zimetufelisha acheni sababu zisizokuwa na msingi kwa mfano me facebook haijanifelisha na hata imenifelisha bac kwa asilimia 10% tu
 

Kwa hiyo unaona sifa kufeli!
 
Dogo hapo hujajitetea lolote. sana sana umetudhihirishia ni jinsi gani 'umefeli' kihalali.
 
Ni kweli kwamba sio wote wanaofeli hawana akili.
Shida huja hapa, je aina ya elimu wanayofunzwa inaeleweka katika fahamu zao?
Sasa ndugu mleta mada ni kwamba kilichokufelisha ni uwezo mdogo wa ubongo wako kuweza kuhifadhi maudhui ya elimu darasa.
 

pole sana dogo kwa kusahihishiwa vibaya!!
 
Una hakika ukipewa mtihani saivi hutozungusha zaidi? Maana elimu ya bongo kukariri kwa ajili ya mitihani hamjambo,mkitoka tu chalii
 

Pole sana,nashindwa nikushauri vipi kwani umekubali mwenyewe umefail vibaya mno sijui vibaya mno inamanisha umepata div zero au?Pia umekekubali mitandao ya kijaa kama imesaidia wewe kufaili ni 10%.
Mini binafsi wakati nasoma sikuwa na mtu aliyekuwa anafuatilia maendeleo yangu ya shule,niliamua kuchagua kusoma hivyo hivyo hata leo pamoja na kuwa na facebook,twitter bado maamuzi ni yako.
Unaweza ukawa member facebook or twitter cha muhimu ni ratiba.Umetenga muda gani kwa siku kwa ajili ya shule yako,kama wewe uko busy na tv,kila kipindi unataka uangalie weekday na marudio yake weekend uangalie ,huoni unajipunguzia muda wa kujisomea?
Tatizo wanafunzi wengi hakuna watu wa kuwashauri na wakiwepo mnawaona wanawashauri mambo ya kizamani na nyie mnataka muende na wakati.
Mi nilitegemea kiwango cha kufaulu kiwe kinongezeka kila mwaka,why?Maswali ,vitabu na material ni yaleyale ni wewe tu mwanafunzi na kichwa chako na muda wako ,tumieni internet kujifunza na siyo kujipoteza.
Mimi nimehifunza mambo mengi kwa njia ya internet,internet si mbaya inategemea unaitumiaje.
Usipende kutafuta mtu wa kumlaumu unaposhindwa katika maisha/shule haisaidii,jiangalie mwenyewe ni wapi uliteleza,naamini jibu unalo labda family issues,au kale kamchumba kalikuzingua sababu ni nyingi.Huwezi soma vizuri kama tumbo halina kitu sijui kama unanielewe.
Mtihani si kipimo tosha cha uwezo wa mtu,hivyo bado unanafasi ya kuprove matokeo uliyo nayo hayakuwakilishi wewe the way you are.
Mi nimefundisha sana mwanafunzi asipoelewa namfahamu on the spot(body language) na hizi tuition zenu za siku hizi mfundishaji mwenyewe alichemka badala ya kuwafundisha mnauziwa notice.Mwalimu mmoja anafundisha tuition masomo zaidi ya matatu huyo mimi siwezi kukushauri usome kwake,mimi naamini maximum mwalimu mmoja ili awe safi masomo yasizidi mawili otherwise atakuwa anawauzia notice.
Usikate tamaa,prove that you deserve more,hizo ni challenge za maisha kaza buti.
 
Kwa hiyo unaona sifa kufeli!

Hujamuelewa si ukae kimya mkuu? Maudhui anayotaka kuonyesha hapa ni kwa jinsi gani serikali inavyodanganya kushuka kwa kiwango cha elimu umesababishwa na mitandao.

Mnajua walianza kufuta michezo mashuleni wakizani ndio kutatua tatizo, jana Chiligati anasema bungeni JK kaongeza shule zimefika 4000 na zote zina wanafunzi kwahiyo zimewapa fursa watoto wengi kuingia sekondari na pia akakiri hakuna wanafunzi katika shule hizi hivyo tumsaidie rais katika hii changamoto. Nilibaki mdomo wazi nakusema haya matokeo wamefaulu sana
 

Pole sana dogo kwa mahasibu yaliokufika. Waswahili wamesema kuteleza sio kuanguka. Ukijipanga vizuri unaweza kujikwamua kutoka kwenye hali hii ya sasa na kuendelea vizuri. Labda hii inaweza kuwa mada itakayofuatilia hii.

Nimefurahishwa na mada yako kwa sababu wewe unaweza kutusaidia sana kujua tatizo hasa liko wapi. Ili tuweze kupata jawabu la haya matokeo mabaya ya sekondari ni muhimu tujue chanzo chake hasa kiko wapi. Najua Waziri mkuu ameunda tume ya uchunguzi na tume nyingine ilikwisha kabidhi ripoti yao 2011 lakini hapa naomba tuanze na wewe, kama mtu wa karibu sana na matokeo ya 2012 (Nyongo mkalia ini). Kama utakubali naomba utueleze yafuatayo, kwa kadri ya uelewa wako, kuhusu shule uliyosoma (unaweza kuitaja hiyo shule ukitaka):

1. Tupe sababu 5 (au zaidi) za udhaifu wa (au tabia za) wanafunzi unazoona zimechangia kuwa na matokeo mabaya.

2. Ni mapungufu gani ya waalimu yaliochangia kuwa na matokeo mabaya.

3. Je mitaala (mlichofundishwa darasani) ilishabihiana na maswali ya mitihani? (jaribu ku-specify kwa kila somo).

4. Ni mazingira gani ya kishule (kama vitabu, maabara, n.k.) yaliochangia matokeo haya mabaya.

5. Ni vitu gani vingine unavyofikiri vikifanywa na serikali, shule, walimu, wazazi, au wanafunzi vitasaidia kuboresha elimu?

Tafadhali tumia muda wa kutosha (usiharakishe kujibu) ili utupe majibu fasaha.

RAI:
Wana JF naomba sana msimhukumu au kumkejeli huyu kijana hapa jamvini. Anahitaji msaada wetu, lakini cha muhimu zaidi ni kwamba sisi tunahitaji msaada wake ili tufahamu hisia na undani wa wanafunzi walioathirika na matokeo haya mabaya.

Natanguliza shukrani zangu.
 

We sasa ndio hujamuelewa.....
 
umesema fb ni 10% sawa
twitter 10%
extreme sms 15%
watsap 20% sababu ya kubembeleza na picha
kuwaza mpenz wako 35%
uvivu kutafuta matilio 5%
walimu 2%
siku ulizodouge 3%
total?
 
kufeli kwako kunamaanisha una akili...
 

Niliposoma heading nilifikili nape ndo anataka kueleza kuhusu kufeli kwake form 4...
 
Hao waliofaulu wamesahihishiwa mitihani yao na alliens kutoka sayari za mbali ama?
 
Muwe mnaanza na 'shakoo'
Kuna mdau jana aliwakumbusha msalimie wakubwa zenu humu jf.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Pole sana mdogo wangu ila hizo 10% ni nyingi sana kwa sababu tukizitoa hizo unaondoka kwenye div 0 uliopata.nakupongeza kama umetambua kwamba kuna 10% umezipoteza kwa uzembe ( japo inawezekana ni zaidi ya 10% ).Hoja yako inaonyesha ulistahili kupata ulichopata hivyo nakushauri jipange upya rekebisha makosa yako .
 

big up sana kwa maelezo yako,huyo kijana akaze buti bado mda ni mwingi!
 
Dogo,soma acha hadithi za jf wala fb!!!!!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…