Si Tanzania pekee
Mjadala kuhusu mitihani hiyo na mfumo wake umeibua taarifa mpya kutoka nje ya nchi, zikibainisha kuwa kilio hicho hakipo tu hapa nchini.
Taarifa ambazo Mwananchi imezipata, zinaonyesha janga kama hilo limeikumba sekta ya sheria Zambia katika mtihani wa uwakili mwaka jana, ambapo mwanafunzi mmoja ndiye aliyefaulu kati ya 395.
Kulingana na maelezo ya Chama cha Wanasheria nchini Zambia (LAZ), anguko kubwa la wanafunzi katika mtihani huo limetokana na umakini wa taasisi inayosimamia kuandaa mawakili mahiri.
Kenya nako, mwaka 2020, Mwanasheria Mkuu wa nchi hiyo, Kihara Kariuki alilazimika kutoa tamko baada ya asilimia 80 ya wanafunzi wa mtihani wa uwakili kufeli.
Katika tamko lake hilo, Kariuki alilinyooshea kidole Baraza la Elimu ya Sheria (CLE) akilituhumu kutunga maswali kinyume na kile walichofundishwa wanafunzi wa taasisi hiyo.
“Kuna haja ya kuoanisha kazi za KSL na CLE… Hii inatokana na kwamba wanafunzi wametahiniwa kwa mambo ambayo hawakufundishwa,” alisema.
Nchini Kenya, baada ya kusomea uwakili katika Shule ya sheria ya taifa hilo (KLS), mtihani kuhusu kilichofundishwa unatungwa na Baraza la Elimu ya Sheria (CLE).
Matokeo hayo yalisababisha Serikali ya nchi hiyo kuunda kamati ya uchunguzi wa kiini cha tatizo na kile kilichoelezwa na Kariuki.
Baada ya uchunguzi, ripoti iliyotolewa ilibainisha kuwa idadi kubwa ya vyuo havikidhi mahitaji ya kitaaluma, ikiwemo rasilimali watu, nyenzo za kusomea na miundombinu.
“Baadhi ya vyuo vya sheria havina hata maktaba au nafasi ya kufanyia kazi,” ilieleza ripoti hiyo.
Mjadala kuhusu mitihani hiyo na mfumo wake umeibua taarifa mpya kutoka nje ya nchi, zikibainisha kuwa kilio hicho hakipo tu hapa nchini.
Taarifa ambazo Mwananchi imezipata, zinaonyesha janga kama hilo limeikumba sekta ya sheria Zambia katika mtihani wa uwakili mwaka jana, ambapo mwanafunzi mmoja ndiye aliyefaulu kati ya 395.
Kulingana na maelezo ya Chama cha Wanasheria nchini Zambia (LAZ), anguko kubwa la wanafunzi katika mtihani huo limetokana na umakini wa taasisi inayosimamia kuandaa mawakili mahiri.
Kenya nako, mwaka 2020, Mwanasheria Mkuu wa nchi hiyo, Kihara Kariuki alilazimika kutoa tamko baada ya asilimia 80 ya wanafunzi wa mtihani wa uwakili kufeli.
Katika tamko lake hilo, Kariuki alilinyooshea kidole Baraza la Elimu ya Sheria (CLE) akilituhumu kutunga maswali kinyume na kile walichofundishwa wanafunzi wa taasisi hiyo.
“Kuna haja ya kuoanisha kazi za KSL na CLE… Hii inatokana na kwamba wanafunzi wametahiniwa kwa mambo ambayo hawakufundishwa,” alisema.
Nchini Kenya, baada ya kusomea uwakili katika Shule ya sheria ya taifa hilo (KLS), mtihani kuhusu kilichofundishwa unatungwa na Baraza la Elimu ya Sheria (CLE).
Matokeo hayo yalisababisha Serikali ya nchi hiyo kuunda kamati ya uchunguzi wa kiini cha tatizo na kile kilichoelezwa na Kariuki.
Baada ya uchunguzi, ripoti iliyotolewa ilibainisha kuwa idadi kubwa ya vyuo havikidhi mahitaji ya kitaaluma, ikiwemo rasilimali watu, nyenzo za kusomea na miundombinu.
“Baadhi ya vyuo vya sheria havina hata maktaba au nafasi ya kufanyia kazi,” ilieleza ripoti hiyo.