Kufeli uwakili kilio Afrika Mashariki

Kufeli uwakili kilio Afrika Mashariki

John7371

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2018
Posts
2,994
Reaction score
6,676
Si Tanzania pekee

Mjadala kuhusu mitihani hiyo na mfumo wake umeibua taarifa mpya kutoka nje ya nchi, zikibainisha kuwa kilio hicho hakipo tu hapa nchini.

Taarifa ambazo Mwananchi imezipata, zinaonyesha janga kama hilo limeikumba sekta ya sheria Zambia katika mtihani wa uwakili mwaka jana, ambapo mwanafunzi mmoja ndiye aliyefaulu kati ya 395.

Kulingana na maelezo ya Chama cha Wanasheria nchini Zambia (LAZ), anguko kubwa la wanafunzi katika mtihani huo limetokana na umakini wa taasisi inayosimamia kuandaa mawakili mahiri.

Kenya nako, mwaka 2020, Mwanasheria Mkuu wa nchi hiyo, Kihara Kariuki alilazimika kutoa tamko baada ya asilimia 80 ya wanafunzi wa mtihani wa uwakili kufeli.

Katika tamko lake hilo, Kariuki alilinyooshea kidole Baraza la Elimu ya Sheria (CLE) akilituhumu kutunga maswali kinyume na kile walichofundishwa wanafunzi wa taasisi hiyo.

“Kuna haja ya kuoanisha kazi za KSL na CLE… Hii inatokana na kwamba wanafunzi wametahiniwa kwa mambo ambayo hawakufundishwa,” alisema.

Nchini Kenya, baada ya kusomea uwakili katika Shule ya sheria ya taifa hilo (KLS), mtihani kuhusu kilichofundishwa unatungwa na Baraza la Elimu ya Sheria (CLE).

Matokeo hayo yalisababisha Serikali ya nchi hiyo kuunda kamati ya uchunguzi wa kiini cha tatizo na kile kilichoelezwa na Kariuki.

Baada ya uchunguzi, ripoti iliyotolewa ilibainisha kuwa idadi kubwa ya vyuo havikidhi mahitaji ya kitaaluma, ikiwemo rasilimali watu, nyenzo za kusomea na miundombinu.

“Baadhi ya vyuo vya sheria havina hata maktaba au nafasi ya kufanyia kazi,” ilieleza ripoti hiyo.
 
Kulingana na ripoti hiyo, kilichojibiwa na wanafunzi katika mtihani wa uwakili ni mithili ya watu wasiowahi kwenda katika darasa la sheria.

“Ni wazi, mafunzo yanaakisi ubora wa huduma za kisheria zinazotolewa na wanafunzi hawa sokoni,” ilieleza ripoti hiyo.

Hata hivyo ilipendekeza kufutwa kwa mitihani ya kuhojiwa (oral examination) na kazi miradi na kuunganishwa katika mbinu za mafunzo ya kozi nzima.

Mapendekezo mengine ni kubadilishwa kwa muundo wa mtihani na kuwekwa muda mrefu zaidi wa mwanafunzi kurudia mitihani, tofauti na ilivyokuwa wakati huo ambapo walirudia kwa miaka mitano pekee.

Vilevile ilibainika wanafunzi wanaosoma katika vyuo vikuu vya umma ndio walioongoza kufeli katika mtihani wa uwakili ikilinganishwa na wale wanaosoma katika vyuo binafsi.

Ripoti ilionyesha kwa mwaka 2016 Chuo Kikuu cha Kenyatta kilikuwa kinaongoza katika hilo ambapo asilimia 30 ya wanafunzi waliofeli walisoma shahada zao chuoni hapo.

Chuo Kikuu cha Moi kilishika nafasi ya pili, ambapo asilimia 22 ya waliofeli walisoma shahada katika chuo hicho na Chuo Kikuu cha Nairobi kikiwa cha tatu baada ya asilimia 20 ya wahitimu wake kufeli.

Kwa ujumla asilimia 79 ya wanafunzi waliofeli mtihani wa uwakili KLS nchini Kenya kwa miaka minane nyuma hadi 2016 walikuwa wametoka katika taasisi za elimu ya juu za umma.
 
Uganda nako shida
Kadhalika, taaluma ya uwakili ni mfupa mgumu nchini Uganda ambako kulingana na matokeo ya mwaka 2019/20, kati ya wanafunzi 1,474 waliofanya mtihani huo 145 sawa na asilimia tisa walifaulu.

Katika orodha hiyo wanafunzi 1,329 waliangukia pua, hali hiyo vilevile iliibua haja ya kufanyika uchunguzi.

Haja hiyo iliibuliwa na Wakili Richard Anguria alipohojiwa na vyombo vya habari, akisema hakuna kinachohalalisha matokeo hayo, hoja ambayo iliungwa mkono na Wakili wa Haki za Binadamu, Nicolas Opiyo. Source-Mwananchi

Tatizo muda
Ukiacha kilio mitihani ya mawakili katika nchi hizo, hapa nchini, juzi usiku ulifanyika mjadala kupitia Space ya mtandao wa Twitter na kukusanya watu zaidi ya 2,000 waliokuwa wanasikiliza au kuzungumzia mitihani hiyo.

Akizungumza katika mjadala huo ulioandaliwa na Mwananchi, Wakili Jebra Kambole alisema mzizi wa tatizo la kufeli katika mtihani wa sheria, haswa kwa Tanzania ni muda mfupi wa masomo katika taasisi ya mafunzo ya uanasheria kwa vitendo.
“Kuna haja ya kuboresha utaratibu kwamba kigezo cha kuingia LST kisiwe kwa kila mwenye ada, kuwepo na mtihani wapewe wanafunzi atakayefaulu ndiyo aingie, lakini kuna haja ya kuongeza muda wa masomo kutoka mwaka mmoja wa sasa,” alisema.
Ndani ya hoja ya ugumu wa kuupata uwakili zimeibuka nyingine lukuki zinazochagiza mzizi wa kufeli kwa wanafunzi wa taaluma hiyo. Source Mwananchi
 
1665817780844.png
 
Back
Top Bottom