"Kufufua" Magari kunapunguza gharama?

Hahahahahahahahahaha,Yani uache kufufua Scania ukanunue Tata?kajifunze Magari bro unatuaibisha...Abood mwenyewe ana Scania Marcopolo Since tunasoma O-level leo tunazeeka bado zinapiga Mzigo...hizo TaTa na Yutong za kichina miaka mi3 tu chali zimechoka watu wanakimbia biashara...ht Diffender huwezi linganisha na magari yenu laini laini ya siku hizi...Acheni kupinga pinga kila kitu tena kwenye vitu msivyo na utaalam navyo
2. Bora utengeneze ulichonacho kikusukume hadi pale utakapopata uwezo wa kununua kingine kuliko ukiache kichakae..
3.Mjini kuna watu kibao wana magari model za 80's n 90' wamenunua Japan huku wanajifanya ni mpya ila serikali ikinunua brand new 90' or 2000 ikafa watu wakaifufua watu mnatia maneno...tieni maneno na zenu
 
Kumaintain gari chakavu ni gharama sana, huo ni uharibifu wa Pesa tu, hizo gharama za kufufua hayo magari angeweza kupata Eicher au TaTa mpya kabisa
Anafufua kwa bajeti ipi?Ni fedha za nani?Tuwe wawazi
 
Anafufua kwa bajeti ipi?Ni fedha za nani?Tuwe wawazi
mzee baba hufuatilii vyombo vya habari?
kukufua magari hayo kampuni ya dar coach wamejitolea buuure ndio maana unaambiwa serikali imeokoa zaidi ya 1B
[emoji3]
 
mzee baba hufuatilii vyombo vya habari?
kukufua magari hayo kampuni ya dar coach wamejitolea buuure ndio maana unaambiwa serikali imeokoa zaidi ya 1B
[emoji3]
Kwa taarifa nilizopata ni kuwa Prof Mbarawa amakataza hilo zoezi.Magari kufufuliwa na wakala wa serikali TAMESA
 
Nilitembelea wilaya Fulani nikakuta wana Ambulance mbovu zaidi ya 4.
Waakati zinahitaji ukarabati mdogo tu. Nao wanalia eti hawana ambulance. Wanataka mpya!

Eboo ...... Badala ya kufufua zile wanasubiri mpya, mbaya zaidi wanasubiri mafungu ya ukarabati wakati wangeweza kuhamasishana zikapatikana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…