Kufuga wamachinga mijini ni sawa na mradi wa kutengeneza mabomu

Kufuga wamachinga mijini ni sawa na mradi wa kutengeneza mabomu

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Iko siku hao tunaowaita machinga watakuja kulikataa hilo jina Na kudai wapewe jina lingine Na wanasiasa. Sasa hivi neno wamachinga linatumika fuko kuukuu kubwa la kuwafichia vijana wasiokuwa Na ajira, wasiokuwa Na pembejeo za kilimo, wasiokuwa na zana za kuvulia wala maeneo ya kuchungia Mifugo. Fuko ambalo wanadhani limejaa kura zao wakati wa uchaguzi.

Lakini vijana wanazidi kumiminika mitaani kutoka vijijini kuja kuungana Na wenzao waliozaliwa mijini kusaka maisha waliyoyakosa huko vijijini. Bila shaka muda sio mrefu nafasi za wazi zitaisha za kutandaza bidhaa, kuegesha bodaboda, za kuoshea magari, za kupigia kiwi, kukaangia chips mijini.

Natabiri siku sio nyingi vita kubwa ya kugombea maeneo ya wazi, kugombea abiria Na wateja itatokea ambayo itawasha moto mitaa Na mali za watu Na viongozi wa kisiasa.

Kama hatutaboresha kilimo, ufugaji, uvuvi, viwanda, uchimbaji Na upatikanaji wa masoko Na mitaji kwa vijana tusijidanganye kwa kuwaacha wamachinga wazagae kila kona wakichafua mazingira Na kuziba njia zote za waenda kwa miguu Na mitaro Na chini ya nyaya za umeme wa msongo mkubwa.
 
Serikali ichukue hatua ya kuwatengea maeneo maalumu yaliyowazi na iwahamishie huko,kama kweli bidhaa zao zina ubora wanunuaji watawafuata huko watakakopangiwa wawepo.
 
Baada ya kuwaacha wamachinga kuuza bidhaa zao usumbufu Tanzania imeingia uchumi wa kati.
 
Wamachinga kuwepo si jambo baya kwani nao wanatengeneza Maisha yao Kiujasiriamali na pia wanakuza Uchumi wetu kwa namna fulani kutokana na Mfumo wa Uchumi uliopo.

Ila tu Serikali (Mamlaka) iwawekee utaratibu Maalum ambao utawawezesha Kufanya Biashara zao bila bughudha za mara kwa mara na kuonekana kuwa ni Takataka katika Mitaa ya Miji yetu mikubwa mbalimbali nchini.

Kinachonisikitisha tu ni kwamba hawa Wamachinga kwa miaka Minne huonekana ni Kero kwa Mamlaka za Kisiasa nchini ila mwaka wa Uchaguzi ukifika tu huonekana ni Lulu, wanadanganywa, wanatumika bila wao Kujua kwa Ujuha wao na Uchaguzi ukimaliza Msoto Kwao na Kudharaulika kunarejea.
 
Pay master wa wizara ya fedha ambaye ni mchaga amekwapua billioni 1.5 ndani ya miezi miwili.
 
Kuna. Mwamba mmoja yy kaweka banda la ofisi ya kinyozi pale AKIBA mkabala na kituo cha mwendo kasi ile ofisi huwa inanichekesha sana kila ninapo pita pale.
 
Wamachinga kuwepo si jambo baya kwani nao wanatengeneza Maisha yao Kiujasiriamali na pia wanakuza Uchumi wetu kwa namna fulani kutokana na Mfumo wa Uchumi uliopo.

Ila tu Serikali ( Mamlaka ) iwawekee utaratibu Maalum ambao utawawezesha Kufanya Biashara zao bila bughudha za mara kwa mara na kuonekana kuwa ni Takataka katika Mitaa ya Miji yetu mikubwa mbalimbali nchini.

Kinachonisikitisha tu ni kwamba hawa Wamachinga kwa miaka Minne huonekana ni Kero kwa Mamlaka za Kisiasa nchini ila mwaka wa Uchaguzi ukifika tu huonekana ni Lulu, wanadanganywa, wanatumika bila wao Kujua kwa Ujuha wao na Uchaguzi ukimaliza Msoto Kwao na Kudharaulika kunarejea.
Sio vibaya kweli watu kujipatia riziki zao, lakini kila shuhuli ni lazima iratibiwe ili isiwe kero kwa wengine. Mfano, mimi ninalipa kodi ambayo inakwenda kutengeneza barabara za kupita magari Na njia za waenda kwa miguu, hivyo sio sawa kama njia yangu ya kupita kwa miguu kwa usalama ikazibwa Na wamachinga ili Mimi nipite barabarani pamoja Na magari. Wamachinga wanasababisha msongamano mkubwa kwenye njia za waenda kwa miguu, masokoni Na hata kwenye vituo vya mabasi Na daladala kiasi cha kusababisha watu kuibiwa, kusukumwa Na abiria kukosa sehemu ya kusubiria magari.

Hii ni kero kwa watu wengine wenye haki zao pia. Machinga wana haki ya kutafuta riziki lakini watu wengine pia wana haki zao pia za kutumia barabara, njia za waenda kwa miguu, kuwa salama Na Mali zao Na kuishi kwenye mazingira safi. Uhuru wako lazima ukomee pale unapoanza Uhuru wa wengine.
 
Iko siku hao tunaowaita machinga watakuja kulikataa hilo jina Na kudai wapewe jina lingine Na wanasiasa. Sasa hivi neno wamachinga linatumika fuko kuukuu kubwa la kuwafichia vijana wasiokuwa Na ajira, wasiokuwa Na pembejeo za kilimo, wasiokuwa na zana za kuvulia wala maeneo ya kuchungia Mifugo. Fuko ambalo wanadhani limejaa kura zao wakati wa uchaguzi.

Lakini vijana wanazidi kumiminika mitaani kutoka vijijini kuja kuungana Na wenzao waliozaliwa mijini kusaka maisha waliyoyakosa huko vijijini. Bila shaka muda sio mrefu nafasi za wazi zitaisha za kutandaza bidhaa, kuegesha bodaboda, za kuoshea magari, za kupigia kiwi, kukaangia chips mijini.

Natabiri siku sio nyingi vita kubwa ya kugombea maeneo ya wazi, kugombea abiria Na wateja itatokea ambayo itawasha moto mitaa Na mali za watu Na viongozi wa kisiasa.

Kama hatutaboresha kilimo, ufugaji, uvuvi, viwanda, uchimbaji Na upatikanaji wa masoko Na mitaji kwa vijana tusijidanganye kwa kuwaacha wamachinga wazagae kila kona wakichafua mazingira Na kuziba njia zote za waenda kwa miguu Na mitaro Na chini ya nyaya za umeme wa msongo mkubwa.
Sio siri machinga ni bomu,we fikiria kila mwaka kwa uchache machinga elfu kumi wanaongezeka Dar ,hilo jiji litawaweka wapi. sasa hivi tayari watu na magari na wafanyabiashara hawana nafasi .miaka mitano ijayo Dar itakuaje!?
 
Back
Top Bottom