Kufunga minyororo magari yanayodaiwa ushuru wa maegesho mijini ni utaratibu wa ovyo kabisa

Kufunga minyororo magari yanayodaiwa ushuru wa maegesho mijini ni utaratibu wa ovyo kabisa

Siamini kabisa kwamba kuna wasomi walikaa sehemu wakajadili na kulipana posho za kikao kwamba:

Magari yanayodaiwa ushuru wa maegesho (parking) Yaanze kufungwa minyororo ili kushinikiza wamiliki kulipia tozo hizo.

Huu ni utaratibu wa hovyo sana

1. Huu utaratibu ni Hovyo kwasababu unatupunguzia wateja sisi wafanyabiashara Kariakoo, Ilala! Sisi wafanyabiashara tunalipia leseni manispaa, tunalipia zimamoto, tunalipia pesa za usafi, tunalipa kodi nyingi tu ili tufanye biashara, Mnapowafungia wateja wetu magari yao mnawatisha kwamba wasije ilala kwamba watakamatwa hili peke yake linatuondolea wateja katika biashara zetu.

2. Jambo jingine la kushangaza hivi nyie wachukua maokoto ya ushuru mmechangia nini kwenye kuwekeza maegesho hadi mchukue ushuru wa maegesho? Magari mengi yanaibiwa kwenye maegesho na ushuru wanalipa, agari yanaibiwa vipuri au taa yakiwa kwenye maegesho huo ushuru mnaolipwa je unafaida gani kwa mwenye chombo kama hamyalindi magari yao wala hamlipi fidia linapotokea janga au uharibifu?

3. Wizara na serikali kwa ujumla mlipopitisha huu utaratibu wa ushuru wa maegesho mlitegemea kwamba hawa wenye magari waendeshe halafu wakapark wapi!?

Gari ileile moja mnaitoza ushuru kibao hamuoni hiyo ni kero jaman
  • gari ileile mnaitoza ushuru wa kuingiza nchini (TRA)
  • Mnaitoza Ushuru wa kutumia barabara (road licence) kwenye kila lita moja ya mafuta mnafyeka sasa mnategemea huyu mtu akapaki porini?
  • Mnamchukua nenda kwa usalama
  • kwenye bima cha kwenu pia kipo na mengine mengi.
Mnataka hawa wenye magari waendeshe magari then wakapark wapi?

Huu utaratibu wa kutoza ushuru maegesho haupaswi kabisa kuwepo, ni utaratibu wa hovyo kabisa.

Mwenye gari katoka zake nyumbani kisitaarabu kufuata huduma kwa mfanya biashara halafu nyie kama serikali mnavalisha watu vibrauzi vya njano kwa kazi ya kufungia wateja wetu magari yao mnataka wateja tupate wapi wakiogopa kuja mijini?

Kwanini mnapenda kuifanya nchi yetu sote iwe kero kwa wengine jamani.

Kweli kabisa kwenye kufunga minyororo inaudhi sana kwa sababu

1: Hakuna mazingira mazuri au maeneno ambayo wametengeneza kama maegesho wao wamebuni kukusanya tu tena hata ukifika unashusha mtu tayari wanapiga picha gari na kukuwekea deni


2: Nilishawahi wapa maoni kwanini wasiwe wanaweka risiti kuonyesha unadaiwa? Kwa nini iwe kama kuviziana? Nitajuaje nadaiwa bila kuwa na taarifa? ndiyo madhara mwisho wanakuja na minyororo kama siyo wizi ni nini?

3: Magari yote huwa yana na namba za wamiliki kwanini wasishirikiane na taasisi husika kama tra kupata namba za wamiliki ili wawe wanatuma taarifa kwenye simu zao?

4: Au waweke mfumo watu wajisajili kwenye simu ili kuwe na notification kwenye simu. Maana tunabanbikiwa sana maegesho na mawakala wao sababu wamewapa target unakuta deni hulijui au unakuta ukifatilia deni la mkoa ambao hujawahi hata kwenda na gari.

5: Masaki wanavizia ofisi za watu kama vile wamejenga parking wao nilishangaa hadi see clif hotel parking zao za nje wamejenga vizuri jamaa wakaingia na mashine zao kulipisha .Kuna kanisa moja lipo sinza tla kkkt tukiwa jumapili tunaenda sali wanakuja hata kama umepaki mbali kwenye ntymba za watu wanapiga picha namba na kuandikiwa deni.

Inaudhi sana sasa firikia haya yote juu unakuta sasa limnyororo na hapo upo na mke na watoto na pesa huna ambayo wanakudai na adhabu juu, kwanza ni kukutukanisha mbele ya familia yako na kukudhalilisha. Dawa kutembea na mkasi wa kukatia mnyororo ndiyo dawa
 
Kweli kabisa kwenye kufunga minyororo inaudhi sana kwa sababu

1: Hakuna mazingira mazuri au maeneno ambayo wametengeneza kama maegesho wao wamebuni kukusanya tu tena hata ukifika unashusha mtu tayari wanapiga picha gari na kukuwekea deni


2: Nilishawahi wapa maoni kwanini wasiwe wanaweka risiti kuonyesha unadaiwa? Kwa nini iwe kama kuviziana? Nitajuaje nadaiwa bila kuwa na taarifa? ndiyo madhara mwisho wanakuja na minyororo kama siyo wizi ni nini?

3: Magari yote huwa yana na namba za wamiliki kwanini wasishirikiane na taasisi husika kama tra kupata namba za wamiliki ili wawe wanatuma taarifa kwenye simu zao?

4: Au waweke mfumo watu wajisajili kwenye simu ili kuwe na notification kwenye simu. Maana tunabanbikiwa sana maegesho na mawakala wao sababu wamewapa target unakuta deni hulijui au unakuta ukifatilia deni la mkoa ambao hujawahi hata kwenda na gari.

5: Masaki wanavizia ofisi za watu kama vile wamejenga parking wao nilishangaa hadi see clif hotel parking zao za nje wamejenga vizuri jamaa wakaingia na mashine zao kulipisha .Kuna kanisa moja lipo sinza tla kkkt tukiwa jumapili tunaenda sali wanakuja hata kama umepaki mbali kwenye ntymba za watu wanapiga picha namba na kuandikiwa deni.

Inaudhi sana sasa firikia haya yote juu unakuta sasa limnyororo na hapo upo na mke na watoto na pesa huna ambayo wanakudai na adhabu juu, kwanza ni kukutukanisha mbele ya familia yako na kukudhalilisha. Dawa kutembea na mkasi wa kukatia mnyororo ndiyo dawa
yaani ni aliyewatuma wafunge minyororo huko shule alikwenda kusomea upumbavu
 
Back
Top Bottom