Uchaguzi 2020 Kufungiwa mgombea kukampeni tumejifunza nini?

Uchaguzi 2020 Kufungiwa mgombea kukampeni tumejifunza nini?

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Mabibi na mabwana heshima kwenu.

Mgombea wa Chadema alifungiwa kukampeni kwa wiki moja kwa makosa ambayo si yeye, chama chake wala wafuasi wake ambao yameweza kuwaingia akilini. Hukumu ya namna hii ina tija gani?

Pana hisia na mwonekano wa wazi kuwa ka uonevu fulani kalipita. Ni kwa sababu kama hizo CDM walisema watasajili malalamiko yao mahakamani kwa kumbukumbu stahiki.

Wapongezwe mgombea yule, Chadema kama chama na wafuasi wao kwa kuamua kupisha shari kwa ile style ya funika kombe badala ya ile ya kata funua.

Siku 7 ndiyo hizo zinayoyoma sasa na tunaelekea kurejea tena majukwaani.

Kama hakuna somo lolote tutakalokuwa tumejifunza sisi sote ikiwamo tume basi aliyeturoga tutatakuwa hatunaye hapa duniani. Kama hali ni hivyo ni suala la muda tu (just a matter of time).

Mtuhumiwa wa tume (na haswa wa yule daktari) katika kipindi hiki cha siku 7 ameendelea kuwa kivutio cha wengi kote alikopita akiwa bila ya ulinzi wowote wa polisi.

Polisi walijaribu kumzuia kwenda mlandizi. Haieleweki ilikuwa kwa manufaa yapi au maelekezo ya nani? Au hata kwa sababu gani?

Mgombea huyu hata baada ya kuzuiliwa kwa saa takribani 8 kiluvya aliporuhusiwa kuendelea, bado amani na utilivu pasipokuwa na polisi vili endelea kutamalaki. Akaenda mlandizi salama, akafanya kilichompeleka kule salama na kurejea salama.

Ni vivyo hivyo kwa mabomu yaliyoshuhudiwa tarime na hata kule ifakara. Ya kiluvya, tarime na ifakara yameonyesha wazi kuwa mleta fujo ni polisi.

Ya kumzuia mgombea kukampeni kulinganisha na mapokezi ya wananchi kwa mgombea huyo nayo yanawanyooshea kidole tume kuwa pana kitu hakiko sawa.

Tume, polisi na mamlaka zote zingatieni sheria zenu ambazo wenyewe ndiyo mmeziweka ili kutodhulumu haki za wengine.

Sheria mpya haziwezi kuongezwa katikati ya mechi. Ni vyema mkajua, wananchi mliowanyima haki zao za kumsikia mgombea wao wakampima wenyewe, hawawezi kuwa na maneno matamu sana kuwahusu nyie.

Enyi tume, itakuwa haiwafikirishi kweli kuwa mnaungwa mkono na chama kimoja ambacho ndicho mnachotuhumiwa kukibeba?

Halahala kabla ya hatari. Wananchi wamevumilia tarime, ifakara, kiluvya na hata sintofahamu hii kumsimamisha mgombea wao kukampeni. Kwa maamuzi na hatua fyongo kama hizi, basi tunakokwenda haihitaji nabii kung'amua kuwa pana hatari mbele yetu inayotujongelea.

Tendeni haki, vinginevyo si muda mrefu kutoka sasa patakuwa na watu ambao wala si wachache watakaotaa hii buruzwa buruzwa isiyokuwa na kichwa wala miguu.

Maendeleo hayana chama!

Ninawasilisha.
 
Kwa uchochezi ule alipaswa afungiwe maisha kushiriki siasa sema kwa sasa ana immunity ya ugombea urais ila uchaguzi ukiisha akijichanganya atajuta .tunamsubilia nje ya uringo
Mabibi na mabwana heshima kwenu.

Mgombea wa Chadema alifungiwa kukampeni kwa wiki moja kwa makosa ambayo si yeye, chama chake wala wafuasi wake ambao yameweza kuwaingia akilini. Hukumu ya namna hii ina tija gani?...
 
Kwa uchochezi ule alipaswa afungiwe maisha kushiriki siasa sema kwa sasa ana immunity ya ugombea urais ila uchaguzi ukiisha akijichanganya atajuta .tunamsubilia nje ya uringo

Kwa Lumumba:

Ukweli = uchochezi
Ukweli = matusi

Ukiwaambia wasema tusi lipi hawana lolote. Wananchi wanaona msidhani wanasubiria tafsiri zenu.

Kama mnataka kujaribu na mumsimamishe tena muone. Ya nini kuandikia mate?
 
Nachokiona ni kuwa mpaka sasa ccm wanaweza fanya chochote na hakuna wa kuwawajibisha kwa lolote.
Hali hii inatia shaka sana juu ya mambo yatakayotendeka baada ya kura kupigwa pasipokuwa na hata mtu mmoja wa kumfunga paka kengele.
Tz hii labda Mungu aje atuokoe kima ajabu kama gambia au malawi ilivyotokea
 
Nachokiona ni kuwa mpaka sasa ccm wanaweza fanya chochote na hakuna wa kuwawajibisha kwa lolote.
Hali hii inatia shaka sana juu ya mambo yatakayotendeka baada ya kura kupigwa pasipokuwa na hata mtu mmoja wa kumfunga paka kengele.
Tz hii labda Mungu aje atuokoe kima ajabu kama gambia au malawi ilivyotokea

Kuna ya limeachiwa Mungu hili mbona limo kwenye artillery range zetu kabisa?
 
Lissu amekuwa kama mgombea wa serikali ya mtaa!

Kwa mtu aliyetamani huyu bwana afe lakini akanusurika, ni wazi kuwa angetamani huyu bwana awe mgombea serikali ya mtaa si zaidi ya hapo. Kwani ni hatari mno kwao anapokuja huku juu!

Msiyempenda kaja na anaitaka ofisi kuu. Sasa ni full kukurupushwa. Kama mapanya tokea mashimoni mwenu!

Dua zenu mbaya kwa Mungu dhidi yake kumchulia wala hazitomfika subhana bali mabaya yote mnayomwombea yatawasibu nyie na wauwaji wenzenu wote mmoja baada ya mwingine!
 
Kwa uchochezi ule alipaswa afungiwe maisha kushiriki siasa sema kwa sasa ana immunity ya ugombea urais ila uchaguzi ukiisha akijichanganya atajuta .tunamsubilia nje ya uringo
Uchochezi upi? Wapi lini? Kuna uchochezi kama wa magufuli kusema kuwa kama hamchagui mbunge diwani wa CCM haleti maendeleo kama kwamba maendeleo ni pesa zake binafsi za mtukufu magufuli,
 
Lissu amekuwa kama mgombea wa serikali ya mtaa!
Kwa ujinga wako unajiona eti na wewe umechangia mada? Watu sample yako ndiyo wameifanya CCM kuchukiwa na watanzania wengi kwa kuwafuga nyie vilaza
 
Back
Top Bottom