Hatahivyo hakuna timu permanent ya taifa. Ikimaliza mechi inavunjika. Nadhan tatizo ni TFF hawako serious na hii timu ya Taifa. Hakuna mipango dhahiri ya maana unaiona inayolenga kuandaa timu ya Taifa kufika mbali katika mashindano mbalimbali (mfano: kufuzu kucheza fainali za Kombe la Afcon, au Kombe la Dunia,etc). Ninachoshuhudia ni kuitwa tu kwa wachezaji kutoka timu mbalimbali waunde timu ya Taifa panapokua na mechi,na shughuli inaishia hapo mechi zikiisha. Hawa wachezaji wanatoka kwenye vilabu vyao,wanakusanyika kwa muda mfupi kulitumikia Taifa lao kisha warudi kwa waajiri wao. Sasa huo muda mfupi wanapokutana wanaenda kukuta mikakati gani imewekwa kimbinu,kimaslahi,kihamasa,kiasi cha kuwafanya wacheze kwa moyo wa kujituma,kutafuta ushindi kwa ajili ya nchi yao? Tunawaandaa vipi na kuwaendeleza vijana wa umri wa miaka 16,18,20 na 23 hasa wale wanaoitwa kwenye timu za Taifa za umri huo wacheze wakijua kuwa wanapikwa kwa ajili ya kuja kutengeneza timu ya Taifa ya wakubwa itakayokua tishio na kufika mbali katika mashindano mbalimbali?Kuna nini ambacho kipo kama motisha kwa sasahivi wachezaji wetu waliopo kwenye ligi za ndani (NBC na ile ya Zanzibar) na wale walioko nje ya nchi watamani au wawe na shauku ya kuitwa kuichezea timu yao ya Taifa? TFF ina mikakati gani ya kueleweka zaidi ya kufukuza kocha timu ikiyumba? TFF hii kazi yake ni kupiga tu faini vilabu kupitia ile kamati yao ya maadili? Ziko wapi programu za maana za kuitengeneza timu ya Taifa?hela za FIFA na za faini zina kazi gani?