Wanafunzi waliofutiwa Matokeo wasiachwe.
Wamepotoshwa na watu wazima waliopewa mamlaka ya kuwalea na kuwasimamia.
Waliohusika wote wachukuliwe Hatua.
Hawa watoto wasiharibiwe maisha kutokana na utashi wa wakuu waliotaka kupata sifa kupitia migongo yao.
Jaribu kujiweka katika nafasi yao, kama ungekuwa wewe unafanya mtihani wa darasa la saba katika mazingira hayo na umri uliokuwa nao wakati huo.
Wasaidieni hao watoto !!!!!!