Kufuzu AFCON-2019: Stars yashindwa kufunga mahesabu mapema! Yakubali kipigo cha goli 1-0 kutoka kwa Lesotho

Viongozi wa TFF tuondoleeni hiyo takataka... hana nia njema na Timu yetu

Ni dhahiri kabisa huyu kocha hatutakii mema sisi watanzania, ambao ni mashabiki wa timu yetu ya Taifa..
Mechi na cape verde alipanga kikosi kibovu tukafungwa.. karudi nyumbani karekebisha kikosi tukashinda..
Leo amekuja kurudia yaleyale.. baada ya kupanga kikosi cha ushindi yeye anapanga kikosi cha majaribio

Huyu kocha hatufai atimuliwe arudi kwao kuuza nyanya
 
Kimahesabu nafasi bado ipo...Uganda anakufa kwa mchina..Cape Verde anamfunga Lesotho..Cameroon ileee
 
Nilishasema timu hio ni presha tuuuu

Ova
 
Naunga mkono hoja
 
Ila nafasi bado ipo
 
Na ajibu hamtaki mzee wa maassistiko
 
Leo Taifa stars inacheza kwa hofu huku wakiwa hawaelewani uwanjani. Kwa mchezo huu lazima wanawaza watazitoa wapi M50 wazirejeshe kwa walipa Kodi?

Poleni Taifa stars poleni Watanzania lakini pia tujifunze kuvumiliana katika machungu tunayopitia
 
Ni lazima tuwafunge Uganda na si kwa kubebwa ili cameroon tukawe kapu la magoli
Ukimfunga uganda umfunge kwa Magoli mengi huku ukiomba Lesotho afungwe au atoe Draw na Cape verde. Kwasababu Lesotho akimfunga Cape verde atafikisha point 8 na sisi tukimfunga Uganda tutakuwa na point 8 hivyo mshindi atakuwa mwenye magoli mengi ambapo Lesotho wana hiyo advantage kwa sasa.

Pia kumbuka ni rahisi sana kwa Lesotho kumfunga Cape verde kuliko Tanzania kumfunga Uganda labda Uganda watuachie makusudi na hii itakuwa dharau kubwa sana.

Cape verde pia sasahivi kapata Matumaini kwasababu Kama akimfunga Lesotho atakuwa na point 7 huku Tanzania kama akidraw au akifungwa yeye atapita. Technically Tanzania hatuna Nafasi ya kusonga Mbele.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…