Kufuzu AFCON 2023 | Taifa Stars 0-2 Algeria | Uwanja wa Benjamin Mkapa

Kufuzu AFCON 2023 | Taifa Stars 0-2 Algeria | Uwanja wa Benjamin Mkapa

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) leo Jumatano ya Juni 8, 2022 kinashuka katika dimba la Benjamin Mkapa kukivurumisha na timu ya Taifa ya Algeria.

Ni fusra kwa Stars kuweka hai ndoto za Nchi kuweza kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) endapo watapata matokeo ya ushindi dhidi ya Algeria baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika mchezo wa kwanza wa kundi F ugenini dhidi ya Niger.

Mchezo hautakuwa rahisi, mchezo unatarajiwa kuwa ni mgumu, lakini la muhimu kwa Taifa Stars ni nidhamu ya mchezo na kufanyia kazi mbinu ya Kocha pamoja na kupambana kwa nguvu zote ndani ya dakika 90 kwenye mchezo huu, hakika watafanikiwa kuwapa furaha Watanzania.

Kila la heri Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Kumbuka mchezo ni kuanzia majira ya saa 1: 00 Usiku kwa saa za Afrika Mashariki na Kati..Usikose Ukaulizia

============================

00' Mpira umeanza Uwanja wa Benjamin Mkapa | Tanzania 0-0 Algeria

05' mchezo wa kasi kiasi mpaka sasa hakuna timu imeona lango la mwenzake.

10' Algeria wanajaribu shambulizi lakini golikipa Manula anatoka na kudaka mpira ule..!

15' Ameinga Zargane upande wa Algeria, ametoka mchezaji jezi namba 14 baada ya kupata rabsha

20' Algeria wanaliandama lango la Tanzania, ila Tanzania upande wa mbele bado hawajafanikiwa kuitia kashi kashi.

Unapigwa mbele kuleee lakini golikipa Manula anatoka na kudaka, Islam alikuwa karibu akivizia.

Faisal anapiga shutii lakini mpira unatoka nje ya lango na kuwa goal kick

30' Hakuna bao, mpira unachezwa katikati ya Uwanja, Tanzania bado hawajapenya ngome ya Algeria

Almanusura Algeria wapate bao kama si uimara wa golikipa Manula huku Samatta naye akikosa nafasi ya kufunga upande wa Tanzania.

35' Faisal anafungua shuti kali, lakini mpira unambabatiza Mandi wa Algeria, ilikuwa nafasi nzuri ya kufunga.

40' baada ya mashambulizi kwa pande zote mbili, mpira umepoa, huku Novatus akiwa chini baada kupata rabsha

Kona inapigwa kuelekea Algeria, inapigwa kulee lakini mpira anao Faisal anajaribu kutafuta nafasiii

45+2' Free Kick kuelekea stars, inapigwa kulee, Mandi anarudisha ndani hatariiiii | Goooooooooaaal, Rami Bensebaini anaipatia Algeria bao la kwanza kwa kichwa baada ya mabeki wa Stars kushindwa kuruka na kuondosha mpira

HT: Tanzania 0-1 Algeria

Kipindi cha pili kimeanza, mabadiliko kwa Tanzania | Ameingia Kibu Denis na ametoka Kibabage

53' Kibu alishakwamisha mpira wavuni, lakini refa anasema Kibu kabla ya kufunga alisukuma, huku Novatus akionyeshwa KADI ya njano

55' Kazi nzuri ya Msuva inashindwa kuzaa bao, namna gani Tanzania hapa.

Mohamed anarukaaaa kichwa lakini mpira unatoka nje, huku Mzamiru akionywa na mwamuzi kwa mchezo mbaya.

61' Faisal anapiga shutii kali sana lakini golikipa wa Algeria anarukaa na kuwa Kona ambayo haikuzaa bao

64' George Mpole na Kelvin John wameingia kuchukua nafasi za Faisal na Msuva

66' Bakar Mwamnyeto anaonyeshwa KADI ya Njano baada kucheza kwa mkono, mpira umechangamka lakini Stars bado hawajaona lango.

72' Rami Bensebaini ametoka na ameingia Touba upande wa Algeria

Ibrahim anapiga shuti, lakini golikipa Manula anapangua na kuwa Kona ambayo haikuzaa bao

80' Algeria wanafanya mabadiliko huku Stars wakishindwa kabisa namna ya kupenya mabeki wa Algeria

Ametoka Novatus na ameingia Abubakar upande wa Tanzania, je yapo Matumaini ya kupata bao? Ngoja Tuone.

87' Kevin John anafanyiwa madhambi eneo, karibu kabisa na box ni nafasi nzuri hii, free Kick, inapigwa kulee lakini golikipa anapangua.

Goooooooooooooaaal Algeria wanapata bao la pili kupitia kwa Mohamed Amoura | Tanzania 0-2 Algeria.

90+4' Matumaini ya kusawazisha yanatoweka hapa, Kibu anapiga Krosi lakini mpira unaokolewa.

Hatari nyingine upande wa Tanzania, lakini mpira unaokolewa, Tanzania wanapata Kona ambayo haikuzaa bao

Naaam mpira Umekwishaaaaaa ambapo Tanzania imelala nyumbani kwa mabao mawili kwa bila.

FT: Tanzania 0-2 Algeria
 
Chonde chonde kocha , wale vijana wa lizungu wa Tanzania, uliochochewa na wachambuzi uchwara kwa kupewa orodha na ligi wanazocheza, hii mechi ni heavy weight usiwaingize kipindi cha kwanza wape hata dakika 5 za mwisho baada ya kuona mwelekeo wa michi
 
FT: Uganda 1-1 Niger.

Game ya pili Uganda wanashindwa kupata ushindi baada ya kupigwa na Algeria 2-0 kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza.
 
Riyad Mahrez leo hayupo dimbani.. Lakini kuna huyu Jamaa Islam Slimani, ni hatari sana yaani..!

Anapaswa kuchungwa, halafu ana vichwa fulani hivi kimo cha mbuzi, mabeki wetu wawe makini.
Twendeni kwa kuwaheshimu tu hawa jamaa na kila mchezaji ajitoe zaidi ya asilimia mia moja! Tukisema tunapishana nao watatuaibisha hapa nyumbani!
MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU IBARIKI TAIFA STARS!
 
Kikosi cha Stars kinachoanza dhidi ya Algeria..!
20220608_181807~2.jpg
 
Kikosi cha Stars kinachoanza dhidi ya Algeria..!View attachment 2254536
Kim naye kwa sasa hana tofauti na hawa waswahili wetu! Yaani uwaache wachezaji wenye nguvu na kasi kama George Mpole, Kelvin John, Kibu Dennis! Halafu unamuanzisha mbele Nickson Kibabage!

Kwa upangaji huu mbovu wa timu, halafu tutarajie matokeo! Labda tushinde kwa bahati.
 
Back
Top Bottom