Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) leo Jumatano ya Juni 8, 2022 kinashuka katika dimba la Benjamin Mkapa kukivurumisha na timu ya Taifa ya Algeria.
Ni fusra kwa Stars kuweka hai ndoto za Nchi kuweza kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) endapo watapata matokeo ya ushindi dhidi ya Algeria baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika mchezo wa kwanza wa kundi F ugenini dhidi ya Niger.
Mchezo hautakuwa rahisi, mchezo unatarajiwa kuwa ni mgumu, lakini la muhimu kwa Taifa Stars ni nidhamu ya mchezo na kufanyia kazi mbinu ya Kocha pamoja na kupambana kwa nguvu zote ndani ya dakika 90 kwenye mchezo huu, hakika watafanikiwa kuwapa furaha Watanzania.
Kila la heri Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Kumbuka mchezo ni kuanzia majira ya saa 1: 00 Usiku kwa saa za Afrika Mashariki na Kati..Usikose Ukaulizia
============================
00' Mpira umeanza Uwanja wa Benjamin Mkapa | Tanzania 0-0 Algeria
05' mchezo wa kasi kiasi mpaka sasa hakuna timu imeona lango la mwenzake.
10' Algeria wanajaribu shambulizi lakini golikipa Manula anatoka na kudaka mpira ule..!
15' Ameinga Zargane upande wa Algeria, ametoka mchezaji jezi namba 14 baada ya kupata rabsha
20' Algeria wanaliandama lango la Tanzania, ila Tanzania upande wa mbele bado hawajafanikiwa kuitia kashi kashi.
Unapigwa mbele kuleee lakini golikipa Manula anatoka na kudaka, Islam alikuwa karibu akivizia.
Faisal anapiga shutii lakini mpira unatoka nje ya lango na kuwa goal kick
30' Hakuna bao, mpira unachezwa katikati ya Uwanja, Tanzania bado hawajapenya ngome ya Algeria
Almanusura Algeria wapate bao kama si uimara wa golikipa Manula huku Samatta naye akikosa nafasi ya kufunga upande wa Tanzania.
35' Faisal anafungua shuti kali, lakini mpira unambabatiza Mandi wa Algeria, ilikuwa nafasi nzuri ya kufunga.
40' baada ya mashambulizi kwa pande zote mbili, mpira umepoa, huku Novatus akiwa chini baada kupata rabsha
Kona inapigwa kuelekea Algeria, inapigwa kulee lakini mpira anao Faisal anajaribu kutafuta nafasiii
45+2' Free Kick kuelekea stars, inapigwa kulee, Mandi anarudisha ndani hatariiiii | Goooooooooaaal, Rami Bensebaini anaipatia Algeria bao la kwanza kwa kichwa baada ya mabeki wa Stars kushindwa kuruka na kuondosha mpira
HT: Tanzania 0-1 Algeria
Kipindi cha pili kimeanza, mabadiliko kwa Tanzania | Ameingia Kibu Denis na ametoka Kibabage
53' Kibu alishakwamisha mpira wavuni, lakini refa anasema Kibu kabla ya kufunga alisukuma, huku Novatus akionyeshwa KADI ya njano
55' Kazi nzuri ya Msuva inashindwa kuzaa bao, namna gani Tanzania hapa.
Mohamed anarukaaaa kichwa lakini mpira unatoka nje, huku Mzamiru akionywa na mwamuzi kwa mchezo mbaya.
61' Faisal anapiga shutii kali sana lakini golikipa wa Algeria anarukaa na kuwa Kona ambayo haikuzaa bao
64' George Mpole na Kelvin John wameingia kuchukua nafasi za Faisal na Msuva
66' Bakar Mwamnyeto anaonyeshwa KADI ya Njano baada kucheza kwa mkono, mpira umechangamka lakini Stars bado hawajaona lango.
72' Rami Bensebaini ametoka na ameingia Touba upande wa Algeria
Ibrahim anapiga shuti, lakini golikipa Manula anapangua na kuwa Kona ambayo haikuzaa bao
80' Algeria wanafanya mabadiliko huku Stars wakishindwa kabisa namna ya kupenya mabeki wa Algeria
Ametoka Novatus na ameingia Abubakar upande wa Tanzania, je yapo Matumaini ya kupata bao? Ngoja Tuone.
87' Kevin John anafanyiwa madhambi eneo, karibu kabisa na box ni nafasi nzuri hii, free Kick, inapigwa kulee lakini golikipa anapangua.
Goooooooooooooaaal Algeria wanapata bao la pili kupitia kwa Mohamed Amoura | Tanzania 0-2 Algeria.
90+4' Matumaini ya kusawazisha yanatoweka hapa, Kibu anapiga Krosi lakini mpira unaokolewa.
Hatari nyingine upande wa Tanzania, lakini mpira unaokolewa, Tanzania wanapata Kona ambayo haikuzaa bao
Naaam mpira Umekwishaaaaaa ambapo Tanzania imelala nyumbani kwa mabao mawili kwa bila.
FT: Tanzania 0-2 Algeria
Ni fusra kwa Stars kuweka hai ndoto za Nchi kuweza kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) endapo watapata matokeo ya ushindi dhidi ya Algeria baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika mchezo wa kwanza wa kundi F ugenini dhidi ya Niger.
Mchezo hautakuwa rahisi, mchezo unatarajiwa kuwa ni mgumu, lakini la muhimu kwa Taifa Stars ni nidhamu ya mchezo na kufanyia kazi mbinu ya Kocha pamoja na kupambana kwa nguvu zote ndani ya dakika 90 kwenye mchezo huu, hakika watafanikiwa kuwapa furaha Watanzania.
Kila la heri Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Kumbuka mchezo ni kuanzia majira ya saa 1: 00 Usiku kwa saa za Afrika Mashariki na Kati..Usikose Ukaulizia
============================
00' Mpira umeanza Uwanja wa Benjamin Mkapa | Tanzania 0-0 Algeria
05' mchezo wa kasi kiasi mpaka sasa hakuna timu imeona lango la mwenzake.
10' Algeria wanajaribu shambulizi lakini golikipa Manula anatoka na kudaka mpira ule..!
15' Ameinga Zargane upande wa Algeria, ametoka mchezaji jezi namba 14 baada ya kupata rabsha
20' Algeria wanaliandama lango la Tanzania, ila Tanzania upande wa mbele bado hawajafanikiwa kuitia kashi kashi.
Unapigwa mbele kuleee lakini golikipa Manula anatoka na kudaka, Islam alikuwa karibu akivizia.
Faisal anapiga shutii lakini mpira unatoka nje ya lango na kuwa goal kick
30' Hakuna bao, mpira unachezwa katikati ya Uwanja, Tanzania bado hawajapenya ngome ya Algeria
Almanusura Algeria wapate bao kama si uimara wa golikipa Manula huku Samatta naye akikosa nafasi ya kufunga upande wa Tanzania.
35' Faisal anafungua shuti kali, lakini mpira unambabatiza Mandi wa Algeria, ilikuwa nafasi nzuri ya kufunga.
40' baada ya mashambulizi kwa pande zote mbili, mpira umepoa, huku Novatus akiwa chini baada kupata rabsha
Kona inapigwa kuelekea Algeria, inapigwa kulee lakini mpira anao Faisal anajaribu kutafuta nafasiii
45+2' Free Kick kuelekea stars, inapigwa kulee, Mandi anarudisha ndani hatariiiii | Goooooooooaaal, Rami Bensebaini anaipatia Algeria bao la kwanza kwa kichwa baada ya mabeki wa Stars kushindwa kuruka na kuondosha mpira
HT: Tanzania 0-1 Algeria
Kipindi cha pili kimeanza, mabadiliko kwa Tanzania | Ameingia Kibu Denis na ametoka Kibabage
53' Kibu alishakwamisha mpira wavuni, lakini refa anasema Kibu kabla ya kufunga alisukuma, huku Novatus akionyeshwa KADI ya njano
55' Kazi nzuri ya Msuva inashindwa kuzaa bao, namna gani Tanzania hapa.
Mohamed anarukaaaa kichwa lakini mpira unatoka nje, huku Mzamiru akionywa na mwamuzi kwa mchezo mbaya.
61' Faisal anapiga shutii kali sana lakini golikipa wa Algeria anarukaa na kuwa Kona ambayo haikuzaa bao
64' George Mpole na Kelvin John wameingia kuchukua nafasi za Faisal na Msuva
66' Bakar Mwamnyeto anaonyeshwa KADI ya Njano baada kucheza kwa mkono, mpira umechangamka lakini Stars bado hawajaona lango.
72' Rami Bensebaini ametoka na ameingia Touba upande wa Algeria
Ibrahim anapiga shuti, lakini golikipa Manula anapangua na kuwa Kona ambayo haikuzaa bao
80' Algeria wanafanya mabadiliko huku Stars wakishindwa kabisa namna ya kupenya mabeki wa Algeria
Ametoka Novatus na ameingia Abubakar upande wa Tanzania, je yapo Matumaini ya kupata bao? Ngoja Tuone.
87' Kevin John anafanyiwa madhambi eneo, karibu kabisa na box ni nafasi nzuri hii, free Kick, inapigwa kulee lakini golikipa anapangua.
Goooooooooooooaaal Algeria wanapata bao la pili kupitia kwa Mohamed Amoura | Tanzania 0-2 Algeria.
90+4' Matumaini ya kusawazisha yanatoweka hapa, Kibu anapiga Krosi lakini mpira unaokolewa.
Hatari nyingine upande wa Tanzania, lakini mpira unaokolewa, Tanzania wanapata Kona ambayo haikuzaa bao
Naaam mpira Umekwishaaaaaa ambapo Tanzania imelala nyumbani kwa mabao mawili kwa bila.
FT: Tanzania 0-2 Algeria