KUFUZU KOMBE LA DUNIA 2018, Novemba 17 2015: Algeria vs Tanzania

Opps sory Ni bichwa la Jiendawazimu... kama lilivyonyolewa na Mr. ''T'' Ulimwengu Thomas waalgeria wamemnyoa vibaya sana...
 
Mimi nasema hivi kuna wengi hawapendi maendeleo yetu kwa nini kila mechi hasa hizi tunazocheza na waarabu lazima ianzie TZ na kumalizia ugenini? Kulikoni. Sijaiangalia hii mechi ziwezi kusema mengi

Kama unajua unajua tu, haijalishi unaanzia wapi, tusitafute sababu, lazima tukubali uwezo wetu bado sana kushindana na timu kama algeria, Shaffi daudi kuna siku alisema ukweli kuwa tusidanganyane hatuna uwezo wa kushindana na timu kubwa kubwa hizi, weee alishambuliwa sana, eti sio mzalendo wa nchi yake!!! Hata leo julio amesema, sasa tunapenda kufarijiana tu, na leo kama wasingeanza ubishoo tungekula 15!!!!.wewe malawi tu kumfunga ni shida unazungumzia algeria!!! Eti hizo ranking za fifa ni namba tu!!!!!
 
Kwa matokeo haya tumepeta faida ya kuongeza watalii na kukuza pato la Taifa. Kila atakayechungulia matokeo ya leo, cha kwanza kuona ni 7-0!!! Kisha atatamani kujua zaidi kuhusu nchi yetu. Atakutana na Kilimanjaro, Serengeti, Ngorongoro nk. Bravo Mkwasa!
 
We ni mkiya eeeh.

Mi ni Simba ila nimesema ninavyodhani ndo ingekuwa, Algeria wamefika sana golini!
Lakini Mkwasa angemuacha Ally Mustafa kwa kuwa sababu kubwa ya Algeria kufika golini sana ni upungufu ktk ulinzi baada ya kadi nyekundu, Mkwasa angeingiza kiungo Mkabaji idadi ya goli zingepungua kidogo!
 
Aibu sana, kwa kuweka rekodi kwa timu yetu tangu tuhaza kushiliki kwenye kufuzu kumbe la dunia. Dah kweli kocha hajiuzulu kabsa. Hapa kazi tu yaan tumefungwa sijui kazi hijafanyika uwanjan.

Makocha Wazawa sioo jamani,bado saaana.

Lazima tupate Kocha Mgeni,makocha wengi waliopita walikuwa wazuri,ila zimeingia fitna za watu wenye kutaka walale kesho waamke wapo Word Cup.

Mkwasa Kuwa muungana kabla hujaumbuka zaidi,Jiuzulu.
Mfumo wako sio,Watanzania hatujafikia level ya kupigwa hivyo,hata droo ya hapa bongo unaona kabisa kwamba jamaa wali relaz saana,ila wangeweza kutuchapa hapa hapa
 
Huyu mtangazaji wa ZBC 2 naye sijuo anajifunza kuhoji mambo ya mpira, mweupe!!! Waliomuona na kumsikia watanielewa!
 
Mi nafurahi tuu, kwamba our great legacy is intranational and intraparty genius in politics, especially the most expensive cheap politics. It will take a decade as long as a decision making process is incapacitated. 7-0 is a number, just like is our annual economic growth rate.
 
Hii timu bado sna ila kwa level yetu tumejitahd sana
Nafasi tulishaipoteza hapa kwetu
 
Au igeuzwe timu ya kucheza kwenye mabonanza..inafuja tu fedha za taifa sioni wanachokifanya.
 
Ati mnasema tumepigwa wiki? Yani wiki hiihii ama?? Hii ngumu kumesa aiseeee!
 
Bora tushiriki mashindano ya machungu duniani labda tunaweza kuchukua kombe..
 

Kweli kabisaa Kamanda.

Bado sana,na kila tukienda mbele hatua moja basi nne tunarudi nyuma kwa fitna.

Mie nasema bado KOCHA MZUNGU ANAHITAJIKA HAPA KWETU.

Sie makocha wetu woote wao wanafundisha Bongo tuuu,tunashindwa hata na wakenya na Waganda wao wanakuja huku kwetu na nchi nyingine za majirani zetu,ila sie hata kuitwa nchi hizo hatuitwi,sasa hapo tu watu hatusomi kwamba bado sana hapa kwetu?
 
Hadi mtakapoacha fitna, majungu, unafiki na kuongea sana. Ifikie mahali siasa iwekwe kando, tuwekeze kwenye michezo.

Wa Tanzania tunaongea kupitiliza, ujuaji mwingi, wengine hawajui kitu lakini uropokaji mwingi kana kwamba tunajua sana. Tusipojitambua hatifiki popote.
 
Na kama ingekuw hivyo,,,, tim kambrazil icngekuwepo saiz
 
Mhhhhhh mimi napita wajameni,nimeshtuka usingizini tu nikasema nichungulie huku.
Mimi sipo.....
 
sihitaji kuona walakusukia.mpira.
na huo uwanja wa taifa bora tukafugie kuku maana tutapata faida.
 
wametupiga wiki waarabu. Halafu ile kamati ya ushindi iliyoundwa ivunjwe maana haijafanya chochote.
HAPA KAZI TU.
 
Hii Ni zawadi kwa jpjm. Ktk miakaa 54 taifaa stars haijawai kuruhusu magoli 7.
 

Hahaha kama yule commentator wa ZBC2 Hassan Mvula anataja Morocco badala ya Algeria...wabongo porojo nyingi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…