Tetesi: Kuhakiki TIN Mamlaka ya Mapato Tanzania ni shilingi 150,000

Mmh
Kuna mtu namjua hajakiki tin..kafika nje ya tra kalipia max malipo..
Kufika ndani kawaambia nimefata stika ....aliyekuwepo akuliza ulishalipa ..ndio...haya nipe risiti akatoa akaprintiwa stika yake..
Hakuamini...hajaulizwa chochote kuhusu uhakiki...
Sas sielewi hawa tra
 
Mkuu vitu vingine kama hivi unamezea tuu, ona sasa ushachafua dimbwi(dindi) wengine tutaogelea wapi
 
Pole sana,mleta mada hapa hujatenda haki na niseme kwa kunukuu maneno yako "tin ya biashara ili uweze kuanza biashara kwa sababu umeshalipia fremu" nikupe elimu kidogo:Tin Kupata pamoja na kuhakiki ni bure ila unapofungua tin ya biashara utafanyiwa assessment na kupewa kadirio la kodi kulingana na biashara yako,na kodi ndogo kabisa ni laki na nusu (150,000) hivyo nijuavyo Mimi umepewa kadirio lakodi ili ulipie na uweze kuanza biashara Mara upatapo leseni.
 
Kaka makadirio ya kodi nilishapewa ambayo ni 106000, wakati wanaendelea na process ndio kuulizwa kwanza ushahakiki tin ikawa bado ndio hapo mtoa huduma akasema ni lazima uhakiki kwanza na ili kuhakiki ulipe 150000 sababu muda umeisha
 
Well said
 
TIN no ni bure na hata zoezi LA uhakiki halilipiwa chochote na ni zoezi endelevu Galina mwisho mm nilienda juzi TRA wakaihakiki nikawauliza mwisho wa zoezi hili ilikuwa ni April mbona bdo linaendelea wakanijibu watu weng bado hawajafanikiwa kuhakiki kutokana na sababu mbalimbali, wengne walikuwepo safarin nje ya nchi so huwezi ukawa na dateline ya uhakik wa TIN no kwa style hii,, na kuhusu malipo hebu muulize vizur Hugo uliyemtuma pengne anatak pesa ya usumbufu
 
Kumbe ndogo, hongera yako wewe unayoiona ndogo
Nilimtuma mtu pia last week akaambiwa....Zoezi la uhakiki lilifungwa mwishoni mwa mwezi wa 4, baada ya hapo kukawekwa fine kwa ambao hawajahakiki, fine ni 10 currency points na kila currency point moja ni TZS 15,000. Kama mtu alikuwa nje ya nchi apeleke ushahidi hatapigwa fine.
 
sasa kama kuna faini itakuwa taabu sana maana wenigine hawakuwepo hapa nchini
kama mimi mkuu.Rafiki yabgu amenishauri nisihakiki niombe upya tuu! kanambia yeye amefainiwa lak 5 na ameshindwa kulipa
 
Kuhakiki TIN kwa laki moja na nusu?nafikili mtakua mmeongea na wale vishoka wajanja wajanja wanashindaga TRA kufukuzia wasiojua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…