Kuhamia Arusha

Sam Seaborn

Member
Joined
Aug 20, 2011
Posts
98
Reaction score
39
Jamani mimi nafkiria kununua shamba ili nihamie Arusha nikaishi kama farmer/settler kule kama wale wa Zimbabwe au Kenya

Je kuna maoni gani? Maeneo gani? nafkiria kununua shamba la eka kama 500 au 1000 hivi....


je kuna sehem ziko green kama hivi?







 
Kama una mtaji wa kutosha hamia tu ila kwa ukubwa huo unaotaka sidhani kama utapata kwa hapa Arusha. Piajiandae kununua heka moja mil 40.

Mimi nakushauri kama unataka kweli kuwa settle hamia Iringa, Njombe hasa Ludewa, Rukwa au Katavi. Huko bado kuna ardhi nzuri kwa kilimo na tena kwa bei nafuu.
 
INAWEZEKANA ,ila lazima uwe na mtaji wa kutosha,Arusha ni mji expensive sana,na uwe tayari kuvamiwa na wameru kama utanunua kwao,kama utaenda mitaa ya wamasai,andaa fensi ndefu ya umeme ili wasiingize mifugo.......kila la kheri....inawezekana.
 
Jamani mimi nafkiria kununua shamba ili nihamie Arusha nikaishi kama farmer/settler kule kama wale wa Zimbabwe au Kenya Je kuna maoni gani? Maeneo gani? nafkiria kununua shamba la eka kama 500 au 1000 hivi....
Naona wote wanakukatisha tamaa lakini wazo lako linawezekana maana kilimo sio mjini.. wamejisahau na kukupa mashaka ya mjini wakati wewe unazungumzia kilimo. Mashamba yapo hasa maeneo ya Kiteto (kuna uhakika wa mvua), Makuyuni (mvua ni haba) na pia unaweza kuelekea Kilimanjaro (West Kilimanjaro) kuna mvua za kutosha na ardhi nzuri ya kilimo lakini tayari inamilikiwa na ma-settler ila wapo wanaouza.. Kazi kwako..
 
Jamani mimi nafkiria kununua shamba ili nihamie Arusha nikaishi kama farmer/settler kule kama wale wa Zimbabwe au Kenya

Je kuna maoni gani? Maeneo gani? nafkiria kununua shamba la eka kama 500 au 1000 hivi....

Nenda maeneo ya barabari ya Moshi - Dar kupitia bagamoyo; Arusha hufiki bei
 



nadhani proximity ya International airport na pia kwa kuwa napenda maisha kama settler Arusha is quite convenient japo kutakuwa more expensive kuliko kwengine.

 
Hizi eka ni mgogoro Arusha labda uwe na mihela ya kutosha.
 
pesa sio tatizo. Tatizo kupata maeneo mazuri ambayo mtu unaweza kuishi comfortable na ukajitegemea kwa kila kitu

ndio maana nikasema think of a settlers life in Kenya, South Africa au Zimbabwe ya zamani

mbio za mjini nishazichoka sasa napanga kudissapear from the scene kabisaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…