MSWATI III
Member
- Nov 16, 2010
- 90
- 63
Hamjamboni mabibi na mabwana na poleni na majukumu ya kujenga nchi yetu. Kama kichwa cha habri kinavyojieleza naomba ushauri juu ya hili swala ya mkopo. Mwaka jana nilichukua mkopo kwenye benki moja hapa DAR. Ndo ulikua mkopo wangu wa kwanza. Hawa jamaa waliniambia kua riba yao ni 19% na nikawa nimechukua mil 6.8 ambayo nitalipa kwa muda wa miaka minne. Tatizo kwenye mkataba wao hawajaandika hio riba na baada ya kuanza kufanya mahesabu vizuri nimegundua kua hawa jamaa wananikata installment kubwa ambayo inaashiria kua riba yao ni kama 41%. Niliwafuata ofisini kwao nikawauliza but majibu niliyopewa sikuridhika nayo. Kwa uelewa wangu, kuna ile universal formula ya kucalculate interest/monthly repayments, ambayo nikiitumia inanipa mahesabu tofauti sana.
Baada ya kufikiria sana, nimeamua nihamishe huu mkopo to a different bank ambyao wana riba nzuri kidogo. Nikishachukua huo mkopo nilipe huu ninaodaiwa then nisepe jumla. Kama kuna mtu mwenye uzoefu na hili swala nitashukuru sana kupata ushauri zaidi juu ya hili. Mbarikiwe sana
Baada ya kufikiria sana, nimeamua nihamishe huu mkopo to a different bank ambyao wana riba nzuri kidogo. Nikishachukua huo mkopo nilipe huu ninaodaiwa then nisepe jumla. Kama kuna mtu mwenye uzoefu na hili swala nitashukuru sana kupata ushauri zaidi juu ya hili. Mbarikiwe sana