Kuhisi dalili za mimba bila kuwa na mimba

OCC Doctors

Senior Member
Joined
Jul 20, 2018
Posts
113
Reaction score
172
'Pseudocyesis' ni muonekano wa dalili zote za ujauzito anazopata mwanamke wakati kiuhalisia hana ujauzito. Mwanamke anaweza kuwa na dalili zote za ujauzito kama kutapika mara kwa mara, shida ya kulala na hata kukosa hedhi lakini vipimo vikaonesha kutokuwepo kwa ujauzito.

Hali hii husababishwa na Tamaa kali ya kuwa mjamzito, kuharibika kwa mimba nyingi, kupoteza mtoto, ugumba, hofu kubwa ya kupata mimba, unyogovu au wasiwasi, jeraha la kihisia, unyanyasaji wa kijinsia na mvurugiko wa vichocheo mwilini (Hormonal imbalance).

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…