Dah nakumbuka siku Moja napokea sim ya jamaa yangu kuhusu hiz mambo sisahau.
Huyu jamaangu alipata sim kwa wadosi wanataka mzigo wa mecury nyekundu na hawajui wanaipata wapi.
Hawa wadosi kwakwel walikua waaminifu sana na walikua na nia ya wanachohitaji, kwaiyo kumpa mchongo jamaangu maana yake wamemuamin na hawezi kuwafanyia UTAPELI.
Jamaangu akanitafuta mm kuniulizia tunapata wapi mecury? naskia Tanga zinapatikana hujawahi kuskia?
Bas baada ya hivyo nikamwmbia hiyo kesi niachie mm naifatilia mapka tupate majibu.
Haikupita siku mbili jibu! likapatikana
ilikua mwaka 2022,Nampigia teacher wangu Pale Kabuku Tanga na muelezea ktk Moja na mbili Mecury inapatikana?
teacher ananiambia ndio ipo, pesa ipo na mwambia pesa sio tatizo, tatizo mzigo tu uwe safi usiwe na mambo mengi.
Bas tukatuma pesa Kwahuyo Babu wamizim elf50, na nauli juu waje dar, kweli bhna jamaa wakaja.
Kukawa kuna mashrt yahpa na pale lakini tulikubaliana nayo il tu Biashara ifanyike kesho Kila mtu afe na chake .
Wakat tunapiga hesabu za kupata, wale mabwege nao wana hesabu zao za kutupata, kwa kweli niwajinga sana.
Nikawapokea,Nikawapeleka Gest na pesa ya kula juu, kumbe wale wajinga usiku ule ule wakahama Ile Gest.
Asubhi naenda kuachukua hawapokei simu,ikabid tumpigie ticha kua jamaa zako vip!? hawapokei sim na Leo ndio siku biashara inatakikana ifanyike.
Hapo wakati huo Wale wadosi tupo nao wamekuja, wapo full wanataka mzigo na tushapoteza gharama nyingi za pesa hasa pia kuakirim wagen wetu.
Wale wajinga wanakuja kumpokea sim ni jion sana ,tunawauliza et wanadai walikua wamefunga Leo ilikua ni zohari
wale wadosi wameondoka bhana tukabakia tupotupo tuu tunafosi mawasiliano na hawa jamaa wapokee sim ila waapi.
Wakawa wadai pesa ya kula kwa mara nyingine na pesa ya Gest ili biashara ifanyike siku ya pili,kwa kweli ilikua ngum ikabidi niwaambie kama biashara haiwez kufanyika Leo nyie rudini.
Tukatapeliwa kwa namna hiyo.