Kampeni zinazidi kushika kasi ambapo kila chama kinachanja mbuga kusaka kura kwa kila namna. Gumzo kubwa lililojili leo ni kauli ya Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ya kuwaasa Wananchi kuichagua CCM kinyume na hapo watapata tabu.
"Mkijidanganya hapa mkachagua wa chama kingine, majuto yake mtayaona, wala siwadanganyi, siwafichi." - Dkt. John Pombe Magufuli
Naweka wazi kauli aliyoitoa Dkt. Magufuli ni sahihi kabisa, twende sawa hapa. Miaka ya 1970's Tanzania ya Nyerere ya TANU na ASP na China ya Mao ya Chama Cha Kikomunisti ilikuwa katika hali sawa ya kiuchumi kutokana na nchi zote kuamini na kusimamia mfumo wa chama kimoja cha kisiasa kushika hatamu ndio maana utawala wa awamu ya kwanza wa Mwalimu Nyerere ulikuwa na mafanikio makubwa sana, shida ilianza tulipoanza kuingiza mifumo ya vyama vingi ambayo ni sera ya ukoloni mambo leo wenye lengo la kutugawa ili waweze kututawala.
Mahali ambapo Wananchi wamechagua Wapinzani pamekuwa na ucheleweshaji wa kimaendeleo. Mathalani tumekuwa na Wabunge wa upinzani ambao asilimia kubwa kazi yao ni kususia vikao na hata kwenye Halmashauri napo pia ni vurugu tupu za kupinga kila kitu.
Tumekuwa na viongozi wa upinzani ambao ajenda yao kuu ni kupinga kila kitu hata bajeti za kuwaletea maendeleo wamekuwa wapingaji. Waliochagua Wapinzani wanayajua majuto haya.
Chama tawala na Chama pinzani kamwe hawawezi kukaa meza moja kujenga Taifa kwa sababu mmoja yupo kimaendeleo, mwingine yupo kupinga maendeleo akiamini ni sehemu ya kumnyima ama kumpunguzia umaarufu wa kisiasa mwenzie.
Vyama vingi vya upinzani bado ni vichanga, havijajiimalisha na kutwa ni kugombana wao kwa wao wakigombea madaraka. Unaweza kuta Mwenyekiti haelewani na Katibu wake, kisa wana makundi ya kimaslahi ya kimadaraka. Muda wa kuwatumikia Wananchi hawana zaidi ya kulumbana wenyewe kwa wenyewe. Waliochagua Wapinzani wanayajua majuto haya.
Kauli ya Dkt. Magufuli si ya vitisho wala ya kibabe bali imejaa upendo wa dhati kwa Watanzania akiwa na lengo la kuwaasa Wananchi kuchagua Watu atakaoweza kuongea nao lugha moja na endapo atakosea yeye kama kiongozi wa chama na Serikali pia ataweza kumwadhibu aliyekosea.
Narudia tena kusema kauli ya Dkt. Magufuli ni sahihi kabisa. Ni afadhali ukosee kuoa au kuolewa kwani unaweza kumuacha mwenzio kuliko kukosea kuchagua kiongozi, majuto yake ni miaka mitano.
Shilatu, E.J
"Mkijidanganya hapa mkachagua wa chama kingine, majuto yake mtayaona, wala siwadanganyi, siwafichi." - Dkt. John Pombe Magufuli
Naweka wazi kauli aliyoitoa Dkt. Magufuli ni sahihi kabisa, twende sawa hapa. Miaka ya 1970's Tanzania ya Nyerere ya TANU na ASP na China ya Mao ya Chama Cha Kikomunisti ilikuwa katika hali sawa ya kiuchumi kutokana na nchi zote kuamini na kusimamia mfumo wa chama kimoja cha kisiasa kushika hatamu ndio maana utawala wa awamu ya kwanza wa Mwalimu Nyerere ulikuwa na mafanikio makubwa sana, shida ilianza tulipoanza kuingiza mifumo ya vyama vingi ambayo ni sera ya ukoloni mambo leo wenye lengo la kutugawa ili waweze kututawala.
Mahali ambapo Wananchi wamechagua Wapinzani pamekuwa na ucheleweshaji wa kimaendeleo. Mathalani tumekuwa na Wabunge wa upinzani ambao asilimia kubwa kazi yao ni kususia vikao na hata kwenye Halmashauri napo pia ni vurugu tupu za kupinga kila kitu.
Tumekuwa na viongozi wa upinzani ambao ajenda yao kuu ni kupinga kila kitu hata bajeti za kuwaletea maendeleo wamekuwa wapingaji. Waliochagua Wapinzani wanayajua majuto haya.
Chama tawala na Chama pinzani kamwe hawawezi kukaa meza moja kujenga Taifa kwa sababu mmoja yupo kimaendeleo, mwingine yupo kupinga maendeleo akiamini ni sehemu ya kumnyima ama kumpunguzia umaarufu wa kisiasa mwenzie.
Vyama vingi vya upinzani bado ni vichanga, havijajiimalisha na kutwa ni kugombana wao kwa wao wakigombea madaraka. Unaweza kuta Mwenyekiti haelewani na Katibu wake, kisa wana makundi ya kimaslahi ya kimadaraka. Muda wa kuwatumikia Wananchi hawana zaidi ya kulumbana wenyewe kwa wenyewe. Waliochagua Wapinzani wanayajua majuto haya.
Kauli ya Dkt. Magufuli si ya vitisho wala ya kibabe bali imejaa upendo wa dhati kwa Watanzania akiwa na lengo la kuwaasa Wananchi kuchagua Watu atakaoweza kuongea nao lugha moja na endapo atakosea yeye kama kiongozi wa chama na Serikali pia ataweza kumwadhibu aliyekosea.
Narudia tena kusema kauli ya Dkt. Magufuli ni sahihi kabisa. Ni afadhali ukosee kuoa au kuolewa kwani unaweza kumuacha mwenzio kuliko kukosea kuchagua kiongozi, majuto yake ni miaka mitano.
Shilatu, E.J