Kuibiwa kusikie tu

Kuibiwa kusikie tu

Mkuu ataweka pesa kwenye Busta kwahiyo vibaka hawata weza kumuibia tena, Mimi mfumo wangu wa kuweka pesa natumia aina Mbili moja napenda Busta yenye mifuko ndiyo naitumia kuweka pesa nyingi labda milioni hii ni nzur kama naenda umbali mrefu na natumia daladala za kugombania, Mbinu ya pili natumia begi la mgongoni kuweka pesa ila mabegi yangu yote yana sehemu nyingi ndani zilizo jificha yani nikituma kanichukulie pesa utatafuta utasema hakuna,au nafunga begi na vikufuli vidogo.
Kwenye daladala vibaka ni wengi mida za Asubuhi na jioni tena njia za Tandale uzur, Makumbusho hizi sehemu lazima utunze pesa ndani ya Busta, ni vizur vijana tuache kununua bossa tununua Busta zenye mifuko na zipo Busta nyingine zina mfuko wa nyuma zina kifungo una vaa Busta yako ndani nje uvaa surali imeisha hiyo.
Busta ndio nini? Au ulimaanisha Boxer?

Na hiyo BOSSA? We jamaa mbona unatutafutia dhambi za bure 😂
 
Pole sana mkuu, ila nyie wanaume mnapenda kuweka pesa mfuko wa suruali na unakua umetuna hivi, nashauri kama ukiweka kwenye wallet aisee ishikilie mkononi tu,ikiwa utapanda daladala
 
Siku ya jana niliibiwa pesa ndani ya daladala kiasi cha 350000 yani usiku mzima nimekosa usingizi. Hapa nilipo kichwa kinauma hatari 😭😭
Pole bothi na karibu mjini. siku ingine usitembee na mabunda ya ela keshi kwenye daladala. kuna watu wametumwa ela umu mijini wangekunyonya macho...shauri yako. shukuru haujakabwa.
 
Pole sana mkuu, ukiwa unahela nyingi mfukoni, usipende kusimama kwenye daladala( tafuta siti ukae)
Pia awe anaweka mfuko wa mbele na uwe mrefu, unaobana.

Hela ya nauli aitenge na hela nyingine kubwa, aweke kwenye mfuko mwingine, hii itamsaidia kuepuka kuvuruga hela ambazo amezitunza, kumbuka anaweza kuingiza mkono ili atoe hela kidogo ikasabisha kutoa au kuziweka karibu na kuwa rahisi kuchomolewa na mwizi
 
Asante sana kaka na nimejifunza pakubwa mkuu
Katika ulimwengu huu ambapo huduma za benki na mawakala wako kila kona kiukweli sijawahi kutembea na zaidi ya 50,000 kwa Wallet, kwanza inatuna na kuumiza ukikaa. Malipo mengi natumia lipa namba,na kiukweli faida ni nyingi ukilinganisha na makato ya kutoa hizo fedha. Pole sana ila tubadilike..
 
Nimekumis pia..ulikua wapi?.sikuoni
Nilikua hapa namsikitikia ndugu Antonio...
Heri ya mwaka mpya mtani wangu
Nikiona I'd yako nasikia raha japo ninaumia kuona simba wanatoboa ligi ya mabingwa na ligi kuu 😔😔😔

Anyway usiku mwema mtani 🤗❤️
 
Pia awe anaweka mfuko wa mbele na uwe mrefu, unaobana.

Hela ya nauli aitenge na hela nyingine kubwa, aweke kwenye mfuko mwingine, hii itamsaidia kuepuka kuvuruga hela ambazo amezitunza, kumbuka anaweza kuingiza mkono ili atoe hela kidogo ikasabisha kutoa au kuziweka karibu na kuwa rahisi kuchomolewa na mwizi
Yeah, kuweka hela sehemu moja inaweza kuleta shida kubwa sana, hasa hapa mjini.. ( kulala njaa, kutembea route ndefu kwa sababu ya kuibiwa nauli na n.k)

Ukifeli sana ni bora uweke hela kwenye soksi miguuni 😁, Alafu Yale makadirio ya nauli unaweka mfuko wa kawaida.
 
Hivi Mnaibiwaje...
Au huwa mnaonekana Washamba..!?

Mimi sijawahi na Siji Ibiwa. Neverrr...
 
Back
Top Bottom