Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sawa, kama unasisitiza madamMimi naijua teh teh
Sasa hivi yupo facebook ana share share video za kila lilwayne na kina rihana
Alisema anapumzika ili kushugurikia maswala binafsi pamoja na Masomo , Lkn pia Ktk maisha lzm ufanye mambo kwa vituo na mpango na Sio kufuata mkumbo, baadae unajitathimini kwa kukaa pembeni , Sio siasa tu ila kila unachofanya Ktk maisha, na kuusoma mchezo , wakati mwingine unarudisha mpira kwa kipa ili uanze upya,then unarudi au unabadiri mwelekeo wa maisha!!! Sio Lazima mtu akifanya siasa mpaka azeeke AU afie ktk siasa!!!Dunia hii inahitaji kuishi kwa maarifa Sana na sio idadi ya watu walionyuma yako!!! All in all still unaunga mkono upinzani na maisha yanaenda!!!!
Mtatiro mwansiasa mwepesi sana alikuwa anafanya siasa za kitoto sana kama ukifuatilia siasa zake hakuwa na kitu cha maana alichokuwa anakijua zaidi ya utotoutoto tu.hebu kdg nipone mudi ya wachangiaji nitajijua
Alipalamia jiji atalijua maisha yatamnyosha tu.Jamaa amemaliza Masterz pale Mzumbe ya public administration.kwa sasa amerudi tena Darasani Tumaini university Anasoma Shahada ya sheria
Huyu hapa
Julius S. Mtatiro
RAIS KIKWETE ANASEMA KUANZIA
MWAKA 2016 CCM ITATOA ELIMU YA
SEKONDARI BURE...
Kwa nini aanze kupanga sera za serikali
ijayo wakati yeye atakuwa Msoga, kijijini
kwake? Na kama yeye ni bingwa wa
mipango mbona mwaka huu peke yake
vijana zaidi ya 20,000 wamerudi
majumbani kwao kwa sababu wamekosa
mkopo wa elimu ya juu?
Wakati Rais anasema hayo nimejionea
jana wafanyakazi wa TAZARA wakianza
mgomo kwa sababu hawajalipwa
mishahara ya miezi mitano, wakati huohuo
nimeona walimu Kinondoni wakiandamana
kudai fedha zao.
Badala ya kuanza kufikiri kipropaganda
dhana ya kusomesha sekondari bure
mwaka kesho, kwa nini tusilipe ada za
watoto hawa masikini wa vyuo vikuu
ambao wanahitaji msaada sasa hivi ili
hayo ya mwaka kesho tuyapange wakati
wa kampeni mwezi oktoba 2015?
Vyama vya upinzani viliposema utoaji wa
elimu bure mwaka 2000, 2005 na 2010,
CCM ilisema vinaongopa na haiwezekani
na wananchi waliamini uongo wa CCM.
Hata hiyo elimu ya msingi tu CCM
imeshindwa kutoa bure, michango iliyopo
sasa inazidi ada ya zamani.
Kinachoonekana hapo ni propaganda za
kuanza kuwaweka sawa wananchi kwa
ajili ya uchaguzi wa mwaka.
Si ajabu kuwa, Kinana na Nape
watazunguka nchi nzima katika mikutano
yao ya mwaka huu, wakieleza sera hii ya
elimu ya sekondari ambayo kuitekeleza
hawawezi.
Na hapohapo wanasahau kuwa mambo
mengi yaliyoahidiwa na CCM mwaka 2010
hayajatekelezwa, Mahakama ya kadhi
siioni, waliahidi!
Ni jambo la ajabu mno kukuta kiongozi wa
nchi ambaye anamaliza muda wake
anaanza kupanga ahadi za serikali ijayo,
wakati uongozi wake umeacha majanga
mengi katika nchi huku ukishindwa
kutekeleza ahadi zake nyingi! Sijui
mnanielewa?
J. Mtatiro,
Dar Es Salaam,
11 Januari 2015.
2 hrs · Public
Kuna Sultan Maalim Seif pale. Mkono wako ukionekana kutaka kugusa penye maslahi yake shurti uondolewe.lkn CUF nayo, unamkumbuka Lwakatare?