Kuitwa mwizi na wananchi kuanza kushusha kipigo bila kuhoji ni kukosa ustaarabu jamii za Tanzania Bara, Wengi wamesingiziwa na kuuawa / kupata vilema

Wabongo tuna roho mbaya ila tunajificha kwenye kivuli cha sisi nj wamoja na lugha yetu ya kiswahili.
Kuna demu alikuwa anaongea na jamaa kwao,jamaa ni dereva wa daladala,ghafla demu akapiga kelele za mwizi,raia wakajazana ila sasa kuna watu walikuwa wanamfahamu wakauliza alieita huyu mwizi ni nani,demu akatokea,wakamuuliza huyu si ni jamaa yako iweje umwite mwizi. Demu akabaki anatoa macho tu. Wakamwambia jamaa aondoke na demu akaishia kuoga mvua ya matusi
 
Kwenye hili sakata la kuitia watu neno MWIZI, raia tunaonekana tuna makosa lakini makosa yapo kwa wanaotakiwa kuwajibisha adabu na si wengine ni vyombo vya usalama.

Ukimpeleka Mwizi halisi Polisi hatafanywa kitu badala yake unaweza kugeukwa, sasa kitendo hicho ndipo kinafanya raia wawe wanamalizana nao moja kwa moja.

Na ndipo neno MWIZI likawa linatumika kama silaha rahisi ya kuangamiza hata kwa watu wasiokuwa wezi.

Endapo kama wezi wangekuwa wanakomeshwa kwenye vyombo vya usalama, tungekuwa na ari ya kuwakamata pindi tusikiapo neno mwizi na kuwapeleka polisi hata kama wamesingiziwa na kule polisi wangeenda kuhojiwa na kupata haki zao, lakini hili limekuwa tofauti na kuzaa hizi mambo za kuitiana neno Mwizi.
 
Hivi ujasiri mtu anapata wapi wakufika na kushusha kipigo
 
Nimekumbuka kijijini kwetu miaka kabla ya 2000s wezi walikuwa hawauliwi na raia ilikuwa ni viboko, wanapakwa na tope mwili mzima halafu wanaanza kuzungushwa kijiji kizima kama adhabu
 
Siku ukiibiwa utaona kuita mwizi ni option sahihi pia.

Siku yako ikifika hauwezi kuchomoka regardless ya sababu, sote ni wapita njia
Mi nlikua na mawazo kama yako mkuu lakini mwisho wa siku nikagundua hakuna kitu kinachodhidi thamani ya uhai. Kuna faida nyingi za kumuacha mtu akaishi kuliko kuyachukua maisha yake.

Kwa kesi kama ya Mandojo utagundua angepewa adhabu ya viboko au kupelekwa polisi kusingekuwa na majuto kwa walioshiriki kuondoa uhai wa mtu asiye na hatia. He's gone na hakuwa mwizi kisa tu waliomuua walikuwa na mawazo haya "wewe hujawahi kuibiwa.".

Niwe mkweli tu nikisikia fulani kauwawa kwa kusingizia jambo huwa naumia na inaniharibia siku kabisa.
 
RIP mandojo, ila ukiitiwa mwizi kuchomoka ni ngumu aisee asilimia 90 lazima ufe, omba yasikukute.
 
Siku ukiibiwa utaona kuita mwizi ni option sahihi pia.

Siku yako ikifika hauwezi kuchomoka regardless ya sababu, sote ni wapita njia
Acha ujinga wewe, tatizo sio kuita mwizi, issue ni kupiga mpaka kuua bila ushahidi wowote zaidi ya kuita mwizi, angalia Kuna siku wewe au mtu wako wa karibu watawaita wezi kwa kukusingizia au bahati mbaya tuu ukaishia kupondwa na mawe mpaka ufe, hii tabia lazima ikomeshwe na iwekwe wazi Hilo ni kosa la jinai, polisi uanze kuelimisha watu na ni marufuku kuchukua Sheria mkononi
 
Sikubaliani na kitendo cha kuuawa Mandojo, lakini hali ndio hiyo siku yake ilikuwa imefika.

Mimi nalia na mfumo uliotufikisha hapa kwenye hatua ya kutumia neno MWIZI kama bomu la maangamizi.

Mfumo wa kuadabisha wezi ungekuwa mzuri tungekuwa na shauku, ari ya kuwapeleka wezi kule wakaadabishwe. Lakini kwa kuwa mfumo uko hovyo tumebaki kuamua bora tumalizane nao moja kwa moja.

Ndipo sasa neno MWIZI likaanza kutumika vibaya, yaani ukiitiwa tu mwizi unashambuliwa bila kujali ni kweli au si kweli.
 
Njoo usome reply za huku mwishoni uone nilikuwa namaanisha nini na ujue mtazamo wangu.

Nishaweka reply nyingi njoo zisome
 
Hapo mwenye hatia ni huyo aliye msingizia mwenzake wizi ...inatakiwa na yeye auliwe hadharani
 
Mwenyezi Mungu awalinde ndugu zetu popote wapitapo.

Nchi ya kujichukulia sheria mkononi… kilichomtokea Mandojo ndicho kilichomtokea yule binti aliyebakwa. Kuna watu wanaona kuwa wapo entitled kutoa adhabu kwa wenzao, ni dalili ya kujikatia tamaa kimaisha. Tunaishi na watu ambayo empathy yao iko chini sana.

WaTz kimaadili tuko 0.
 
RIP mandojo, ila ukiitiwa mwizi kuchomoka ni ngumu aisee asilimia 90 lazima ufe, omba yasikukute.
Na hivi umaarufu ulishapotea kizazi cha kuanzia 95 hawamfahamu. i hope hakua anajihusisha na mambo hayo. Sijui story yake imekaaje kiuhalisia, alikua anatoka wapi kwenda wapi anafanya nini eneo gani ikawaje!!
 


Tatizo polisi wapo wanachojali ni siasa tu za chadema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…