Kujiendeleza kimasomo kazini ni suala linalohitaji kuangaliwa vizuri

Kujiendeleza kimasomo kazini ni suala linalohitaji kuangaliwa vizuri

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,151
Reaction score
4,277
Licha ya umuhimu wa kuboresha maarifa kazini bado suala hili limekuwa na ukakasi mwingi kuliko mianya bora ya ufanisi. Licha ya wawakilishi wa mwajiri kuwatatavwatumishi wengi kujiendeleza kwa gharama zao wenyewe kimasomo bado sheria ya kutumikia muda wa daraja la mshahara ni changamoto kwa watumishi wanaojiendeleza.

Hakuna njia nyepesi wala njia rahisi kwani kusoma kwa njia ya masafa marefu ni changamoto na kukaa darasani nako kunaambatan na sheria nyingi zinazombana mtumishi anayejiendeleza. Mathalani kuhudhuria kazini wakati wote wa likizo endapo mwajiri atakuhitaji.

Serikali yetu kama ina nia njema na ubora, tija na na maendeleo endelevu yanayosaidia kuboresa utendaji ni vyema ikiliangalia suala hili kwa makini zaidi.
 
Shida ni nini mkuu? Ukienda masomoni hupandi daraja?
 
Hupandi daraja ndio, huruhusiwi kuhama baada ya masomo mpaka baada ya miaka miwili, pamoja na kwamba unajisomesha, huna ruhusa kusomea kitu kilicho nje ya kada husika

Kwahiyo Kama umeenda kusoma baada ya kutimiza vigezo? Na inachukua muda gani kupanda baada ya masomo?
 
Shida ni nini mkuu? Ukienda masomoni hupandi daraja?
Vigezo vya kupanda daraja inazidi
Hupandi daraja ndio, huruhusiwi kuhama baada ya masomo mpaka baada ya miaka miwili, pamoja na kwamba unajisomesha, huna ruhusa kusomea kitu kilicho nje ya kada husika
Vigezo vinazidi kuwa vigumu...infact ili upande sharti ulitumikie daraja unalovuka kwa angalau miaka 3.( minne 4).
 
Hupandi daraja ndio, huruhusiwi kuhama baada ya masomo mpaka baada ya miaka miwili, pamoja na kwamba unajisomesha, huna ruhusa kusomea kitu kilicho nje ya kada husika
Mkuu hivi daraja unapaswa kulitumikia muda gani baada ya probation period?.
 
Hupandi daraja ndio, huruhusiwi kuhama baada ya masomo mpaka baada ya miaka miwili, pamoja na kwamba unajisomesha, huna ruhusa kusomea kitu kilicho nje ya kada husika
huyo mwajiri anakuonea, anayeruhusiwa kukushikilia ni yule anayekulipia masomo
 
Hupandi daraja ndio, huruhusiwi kuhama baada ya masomo mpaka baada ya miaka miwili, pamoja na kwamba unajisomesha, huna ruhusa kusomea kitu kilicho nje ya kada husika
1. Unapanda vipi daraja wakati hujalifanyia kazi?? Upo masomoni maana yake hautekelezi majukumu ya daraja hilo, ni sahihi kutopandishwa daraja

2. Huruhusiwi kuhama mpaka ipite miaka miwili baada ya kumaliza masomo, ni kwa mujibu wa sheria ipi? Ukiomba ruhusa ya masomo kwa barua, ulitimiza takwa la kisheria. Barua ya mwajiri wako ya kukuruhusu kwenda masomoni ilieleza hilo kuwa hutahama na ikaweka na kifungu cha sheria kuthibitisha hilo? Kama hakuna, unafanyaje kazi kwa maneno ya hewani tu mkuu?

3. Ni sheria na kifungu gani kinachoeleza kuwa mtumishi anapojiendeleza kimasomo hapaswi kusoma nje ya kada yake?? Kwenye ajira kuna kitu inaitwa re-categorization, mtumishi kutoka kada moja kuhamishwa kwenda kada nyingine sababu ana ujuzi wa kada zote mbili, waliweka hiyo re-cat ya nini kama hairuhusiwi mtu kusoma kada tofauti na aliyonayo??

Zingatia:
Mahusiano ya ajira ni ya kisheria, usielekezwe jambo kiholela bila mrejeo wa sheria.
 
Nisadie hapa mkuu, ni kweli ukirudi shule hulipwi mshahra wako.?
1. Unapanda vipi daraja wakati hujalifanyia kazi?? Upo masomoni maana yake hautekelezi majukumu ya daraja hilo, ni sahihi kutopandishwa daraja

2. Huruhusiwi kuhama mpaka ipite miaka miwili baada ya kumaliza masomo, ni kwa mujibu wa sheria ipi? Ukiomba ruhusa ya masomo kwa barua, ulitimiza takwa la kisheria. Barua ya mwajiri wako ya kukuruhusu kwenda masomoni ilieleza hilo kuwa hutahama na ikaweka na kifungu cha sheria kuthibitisha hilo? Kama hakuna, unafanyaje kazi kwa maneno ya hewani tu mkuu?

3. Ni sheria na kifungu gani kinachoeleza kuwa mtumishi anapojiendeleza kimasomo hapaswi kusoma nje ya kada yake?? Kwenye ajira kuna kitu inaitwa re-categorization, mtumishi kutoka kada moja kuhamishwa kwenda kada nyingine sababu ana ujuzi wa kada zote mbili, waliweka hiyo re-cat ya nini kama hairuhusiwi mtu kusoma kada tofauti na aliyonayo??

Zingatia:
Mahusiano ya ajira ni ya kisheria, usielekezwe jambo kiholela bila mrejeo wa sheria.
 
Back
Top Bottom