Kujisahau ni hatari nyingine inayofanya wengi washindwe kutumia mazingira rafiki katika jambo husika

Kujisahau ni hatari nyingine inayofanya wengi washindwe kutumia mazingira rafiki katika jambo husika

Mwanasayansi Kalivubha

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2024
Posts
344
Reaction score
926
Maisha yana Vipindi mbali mbali ambavyo mara chache vinajirudia na hata vikijirudia ni kwa sura na lengo jingine.

Unaweza kurudi kwenye shule yako ya msingi ila sio tena kama mwanafunzi bali utarudi kwa lengo lingine kabisa hivyo kama kuna jambo ulitakiwa ufanye kama mwanafunzi unaweza usilifanye tena kwa sababu huna hiyo hadhi tena japo upo mazingira yale yale.

Ni muhimu tuwe makini na mazingira na urahisi wake kufanya jambo fulani katika kuelekea malengo yetu ili isije kutugharimu kufanya jambo lile lile kwa gharama kubwa ilihali awali kulikuwa na urahisi ila TUKAJISAHAU.


Malengo uliyoshindwa kuyatimiza miaka 30 ukiwa unalipwa mshahara ukitaka uyafanye sass ukiwa mstaafu kuna ugumu utakuwepo tofauti na kama ungeyafanya kabla.

KI UFUPI NI KUJITAHIDI KUJUA NINI UNATAKIWA KUFANYA KATIKA KILA MAZINGIRA KABLA HAYAJAPITA NA KUKUPA UGUMU TENA KULIFANYA JAMBO LILE LILE ILA MAZINGIRA TOFAUTI.

#Mwanasayansi Saul kalivubha
#Fikia Ndoto Zako
 
Doing right thing,with right people,at the right place,at the right time,for the right reasons,to get right results itakuwa ngumu
...
Wakati mwingine inabidi ufanye jambo baya kwa sababu nzuri
 
Back
Top Bottom