Kukaa ndani siku nzima bila kutoka nje

Kukaa ndani siku nzima bila kutoka nje

Habari wakuu Mimi ni kijana wa late 20s ila tangu mdogo nilizoeshwa kukaa ndani tu yaan kwa kifupi wazazi hawakutaka tabia ya kuzuzura sasa mpaka now ni form sixleaver nakaa tu ndani siku nzima mpaka watu wananitania nakaa ndani utafikiri mwali..ushauri wakuu nifanyeje kuondoka hii tabia ya kushinda ndani tu
Acha tabia ya kupanda mnazi kwa mkono mmoja utaacha kukaa ndani
 
Vizuri kama upo hivyo ukijichanganya utaanza tabia mbaya haswa ulevi na uzinzi kama huna ishu kaa ndani au kama unataka kujiweka busy lima bustani ya mbogamboga na maua uwe unamwagilia na kupalilia kila siku
 
Bora wewe hautoki nje.. Mim nilikaa sehemu mwaka mzima bila kujulikana na watu wa maeneo yale... Yaan walikuwa hawajui naishi nyumba ipi, jina langu nk.

Ila ni jambo la kawaida tu.
 
Nilizoea hivyo toka utotoni hadi sasa. Kama sina inshu au siendi kazini huwa niko ndani tu.

Upole wangu na kutopenda makundi hasa ya vijiweni na malezi vilichangia hasa kwa upande wangu.

Siyo ugonjwa dogo.
kuna siku uliwahi niambia tunafanana kitabia'... leo nina sadiki maneno yako
 
Kukaa ndani kama utumbo siwezi abadani...labda kuwe na ishu ya maana!

Halafu mwanaume kukaa ndani dooh! Haileti picha nzuri asee
 
Back
Top Bottom