Kukamatwa Juzi kwa Kato Rasta Muuaji wa Afande Muna Kawe ni jibu tosha kuwa huwezi Kuikimbia popote pale Jamhuri kama ikikutaka

Tena km alishaingia Songea, angezamia matimira, kilagano, muhukuru au mpitimbi, angekamatwaa wapiiii?

Yaan huko angekua kibarua wa mashambani, angetafuta demu na kuoa hapo kijijini, angekaa miaka kadhaa afu angechoropokaa.
 
nasemaje... Natafuna lines natupa kule halafu sim natupa yenyewe tupu bila line then ataokota mtu mwingne ataweka lain zake au tauza kivyovyote! Vipi hapo sijauza msala?
 
Aliishiwa pesa ya matumizi bhana. Ndo maana amedakwaa.
 
Wee km aliingia songea, si angejichanganya kwa watu huko kijijini na kujifanya kibarua wa kulima msimu huu wake kabisa, angedakwa wapii?

Yeye ameshindwa kujiongezaaa. Poleee yake
Lazima uwe mzoefu wa uhalifu kuna wenge pia damu ya mtu.....sio rahisi mnavyofikiria.....vibarua songea huko sio lelemama
 
Mkuu, unazungumzia Tanzania hii hii? Ni wangapi wanajua hata crypto?
 
Unavyoongea kama vile ni kesi ya Kuku pana mtu alienda kukamatwa Athrone Cape Town na kule alipewa kabisa msikiti kama sheihk alikua anatoa sana misaada Cape Town alivyokamatwa watu walidhani kabambikiwa kesi walitaka kuandamana wakaambiwa tarehe aliyofika SA na watu anaoshirikiana nao huko Pakistan ikabidi watulie Bunge la SA liliingilia kati kuwa ahukumiwe SA baadae wakakubaliana apelekwe kwenye Jimbo ambalo wamefuta hukumu ya kunyongwa hadi kufa yupo huko USA kahukumiwa maisha Jela yule Kijana wa Kizanzibar....waliolipua ubalozi wa USA daslm
 
Acha ujuaji WA kijinga , kuna Kato mnyiramba ?
Unajua maana ya kina Kato kwa kihaya na luganda ?
Halafu huyo kijana si alikuwa ameshakamatwa kitambo ?
Si wewe uliwahi kusema humu kuwa ameshakamatwa alipokuwa anaenda kufuatilia pikipiki yake iliyoibiwa huko Mwenge ?
 
Hapa unazungumzia Ma mbele huko siyo bongo

Kwa maana hiyo jamaa kupita mikoa yote hiyo alitembea kwa miguu?
 
Lazima uwe mzoefu wa uhalifu kuna wenge pia damu ya mtu.....sio rahisi mnavyofikiria.....vibarua songea huko sio lelemama
2013 kwetu tulipata kibarua wa shamba, yule bwana kumbe huko kwao aliua jamaa mwenzie wakiwa kibanda umiza huko Tabora,
Yule bwana alikua mtiifu wa kazi za shamba na kuchunga mifugo yetu,

Alikaa pale kijijini had 2016 akaoa na kuanzisha familia yake, 2019 kuna jamaa mnunua mazao kumbe ni wa huko kijijini kwao na anamfahamu, alivyofika kumuona alihamaki, kakuta mwenzake ana mke na mtoto na nyumba yake, kiufupi ana maisha yake,
Yule jamaa ndo akatusimulia pale home, nakumbuka mzee akamuambia yule mgeni asiseme kwa watu, huwezi amini baada ya muda ndugu wa yule kibarua walikuja kule kijijini, navyoongea maisha yake yako pale kijijini ana fuga ng'ombe na mbuzi, kurudi kwao hataki tena, ila ndugu zake ndo wanamtembelea.
 
Hivyo ya kuombwa siku ndio mbaya zaidi maana likimkuta ya yote kati yao ....unawekwa mtu kati.
Mbaya zaidi uwe humfahamu uliyempa simu.
mim nilishaacha haya mambo sim yangu ya mkononi ni yangu mwenyewe litakalotokea kwa matumizi mabaya ya sim yangu, nitawajibika mwenyewe. Hata uje kikongwe unaomba mawasiliano umpgie ndg yako sipo tayari kukupa sim yangu
 
Tunatakiwa tufahamu kuwa duniani kote mhalifu anayetafutwa (hata mimi na wewe ikitokea ,Mungu aepushe ) hukumbwa na vitu viwili vikuu ambavyo ni :

1) Hofu (Fear): ni hali ya wasiwasi inayompata mtu au mnyama mbele ya mwingine au kingine kisichompendeza au kuhatarisha usalama wake.


2) Woga (Paranoia/ Anxiety) (Naomba nirekebishwe): ni tabia ya kupatwa na hofu kupita kiasi inayokuwa ndani ya binadamu juu ya kitu au vitu fulanifulani.

Hivyo vitu viwili hupelekea kufanya makosa ya kimkakati ambayo vyombo vya dola huvitumia kama faida kwao! Ukiwa na hivyo vitu ni lazima narudia tena ni lazima utafanya makosa.

Moja ya mafunzo ya kijasusi na machache kwa vyombo vya dola ni kukuondolea hivyo vitu vikuu viwili na kukupa vitu vipya! Baada ya kuondolewa hivi vitu huwa wanaweza kuhimili hali zote! Mimi na wewe hatuwezi!

Mfano 1: mwangalie Kikwete na marehemu Magufuli reaction zao kuhusu jambo lolote, utagundua mmoja amekasirika mwingine anatabasamu.

Unaweza kuona huyu aliyekasirika ni jasiri kumbe ni kinyume chake! Mwingine ana hisia mwingine anaigiza hisia!

Mfano 2: Mwangalie Putin na Kim wa Korea Kaskazini, namaanisha kampe taarifa Kim kuwa wanajeshi wako 1000 wamekufa halafu nenda kwa Putin kampe hiyo taarifa!

Nb: 1) Hisia hupelekea kufanya makosa!

Nb 2) Mhalifu siku zote huwa mwoga!

Nb 3) Dola halina hisia ila watu wake wana hisia!

Ni mtazamo wangu!


"The escape man is still human, he is still afraid, Fear becomes paranoia, paranoia ultimately psychosis. I bring this up because in one hundred and forty years, the fundamental mind of the escape man has not changed "- FBI Special Agent Alexander Mahone (Prison Break)
 
Kwa hiyo Askari wetu akipata matatizo Askari mwenzao wanaweza kufanya ufuatiliaji ila kwa wananchi story nyingi
 
mim nilishaacha haya mambo sim yangu ya mkononi ni yangu mwenyewe litakalotokea kwa matumizi mabaya ya sim yangu, nitawajibika mwenyewe. Hata uje kikongwe unaomba mawasiliano umpgie ndg yako sipo tayari kukupa sim yangu
Sahihi mkuu
 
Ok. Good to hear this from an expert.
 
Kato sio survivor ni mtoto wa mama tu!
Usikute hapo aliishiwa hela akaanza kulialia kwa ndg jamaa na marafiki ambao tayari simu zao zilikuwa tracked!

Alitakiwa akate mawasiliano na watu wote wa karibu na hata ikitokea dharula ngumu basi angetumia code maalum kuwasiliana kwa namba nyingine pande zote.

Ukifanya uharifu ishi "kigendaeka".
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…