Kukata GOGO!

Kukata GOGO!

Kuna Watu wengi wana mushkila wa Qabz ya tumbo (Constipation) kwa kiswahili kukosa kufanya haja kubwa. Kuna sababu tofauti:

1- Kukosa kunywa maji
2- Kukosa kula kwa wakti
3- Kukosa kula vyakula vya maana
4- Kukosa kwenda chooni wakati unapojihisi unataka kwenda na kujizuia.

Na hii husababisha uvivu na viungo kuuma na pia kujiona saa zote unataka kulala.

VIPI KUJITIBU BILA YA KUTUMIA HALULI

1- Kunywa maji gilasi 8 kwa siku

2- Kula kwa wakti wake.


3- Kula vyakula vya maana sio unaokotea tu.


4- Uwende chooni wakati unapojihisi unataka kwenda na usijizuie.


5- Kunywa maji baina ya kila tonge 2 au 3.


6- Kunywa mafuta ya Halzet (Olive Oil) au kutia kwenye chakula kama salad kila siku inasaidia kulainisha tumbo.


7- Kunywa maji kama gilasi 3 au 4 kisha ukawa unakwenda ukirudi kwa muda wa robo saa au dakika 20.


8- Kuchukua chupa ya Tanuf (litre 1 na nusu) na kutia chumvi kidogo kisha ukaichanganya sawa sawa halafu ukainywa yote kwa pamoja na hii mtu akifanya mwezi mara moja kwani kama haluli.


9-Kila Asubuhi na usiku - gilasi ya maji ya moto moto utachanganya na kijiko kikubwa cha asali na utakunywa.


10-Haba Sawda utasaga na uchanganye na asali na uwe unakula kijiko asubuhi kijiko usiku kila siku.


11- Fruits - Papai , Embe, Machungwa na kama unaweza ule maganda meupe.


12- Kwa watoto wadogo - juice ya chungwa - sukari na maji - asali na maji moto moto.

Fuata ushauri wangu Kisha unipe Feedback


Nitajitahidi mjomba!! Lakini mmh! zingne hapo mbona ngumu, watu wanazifanya kweli!! glass nane kwa siku..... etc, kwa muda gani.
 
Nina wiki jamani sijakata GOGO!!

Asubuhi: Chai na mihogo/chapati etc home.
Mchana: Chips Kitimoto Survey migombani/Chips Makange Rozi garden/Ugali nyama choma pale Hongera.
Usiku:Ugali/wali nyama/maini/mchicha na matunda home mamsap plus Lager moja au mbili hivi kabla ya kulala.

Hivi vitu vyote vimeenda wapi jamani: Nimekula hewa au nina Pepo mie.

Kiafya: Rate ya kwenda Chooni inatakiwa iweje wajameni! Loh!!
kula ukwaju sahani mbili sio juice mumunya na juice ya pera ya azanu
 
Nitajitahidi mjomba!! Lakini mmh! zingne hapo mbona ngumu, watu wanazifanya kweli!! glass nane kwa siku..... etc, kwa muda gani.

DASA, glasi 8 ni chache. glasi 1 = 250 ml au robo lita. kwahiyo glasi 8 sawa sawa na lita 2 tu!, lager 1 ina ujazo wa 500 ml au nusu lita!, ukiambiwa upitie bar fulani kila siku kuna ofa yako ya lager 8 hautasema ni nyingi!, lager 8 ni sawa sawa na lita 4, najuwa wapo wanakunywa lager mpaka kumi na kuendelea kwa siku.

Tunasema unywe glasi 8 yaani lita 2 gawanya mara mara glasi 8 tofauti kwa siku siyo zote kwa pamoja, unaweza kunywa zaidi ya hapo lakini yasizidi lita 3.5 kwa siku. mwili wa binadamu unapopungukiwa maji, hutoa ishara (indicators), tumeziita ishara hizo kuwa ni MAGONJWA. Asilimia 94 ya damu yako ni maji, asilimia 85 ya ubongo wako ni maji, asilimia 75 ya wewe ni maji, you shouldn't have eaten!. Kila siku unatakiwa kunywa maji. tembelea Utangulizi | maajabu ya maji ujifunze zaidi kwanini maji ni uhai.
 
DASA, glasi 8 ni chache. glasi 1 = 250 ml au robo lita. kwahiyo glasi 8 sawa sawa na lita 2 tu!, lager 1 ina ujazo wa 500 ml au nusu lita!, ukiambiwa upitie bar fulani kila siku kuna ofa yako ya lager 8 hautasema ni nyingi!, lager 8 ni sawa sawa na lita 4, najuwa wapo wanakunywa lager mpaka kumi na kuendelea kwa siku.

Tunasema unywe glasi 8 yaani lita 2 gawanya mara mara glasi 8 tofauti kwa siku siyo zote kwa pamoja, unaweza kunywa zaidi ya hapo lakini yasizidi lita 3.5 kwa siku. mwili wa binadamu unapopungukiwa maji, hutoa ishara (indicators), tumeziita ishara hizo kuwa ni MAGONJWA. Asilimia 94 ya damu yako ni maji, asilimia 85 ya ubongo wako ni maji, asilimia 75 ya wewe ni maji, you shouldn't have eaten!. Kila siku unatakiwa kunywa maji. tembelea Utangulizi | maajabu ya maji ujifunze zaidi kwanini maji ni uhai.

Yani ndio nimetoka kulikata sasahivi!! Loh!
 
Nina wiki jamani sijakata GOGO!!

Asubuhi: Chai na mihogo/chapati etc home.
Mchana: Chips Kitimoto Survey migombani/Chips Makange Rozi garden/Ugali nyama choma pale Hongera.
Usiku:Ugali/wali nyama/maini/mchicha na matunda home mamsap plus Lager moja au mbili hivi kabla ya kulala.

Hivi vitu vyote vimeenda wapi jamani: Nimekula hewa au nina Pepo mie.

Kiafya: Rate ya kwenda Chooni inatakiwa iweje wajameni! Loh!!

Mkuu usijari utakuwa na selfcontener tumbon mwako
 
Kwa kifupi unatatizo la kuganda kwa choo,
Tiba tafuta ukwaju kama kilo 1 weka kwenye maji lita 2 baada ya nusu saa anza kuukamua kwa mikono usitumie brenda utapata juice nzito weka asali kupunguza uchachu usiweke sukari kunywa kwa wingi uwezavyo baada ya nusu saa utakata gogo laini sana
Kinga; jitahidi kula chakula mapema kabla ya kulala
Kula matunda ya kutosha au juice za matunda natural siyo artificial
Kwa kuzingatia hayo hutapata tatizo hilo tena.
 
Back
Top Bottom