Kukithiri kwa mateja (Wala madawa ya kulevya) Serikali iwajibike maana ndio inayopelekea tatizo kuwa kubwa zaidi

Kukithiri kwa mateja (Wala madawa ya kulevya) Serikali iwajibike maana ndio inayopelekea tatizo kuwa kubwa zaidi

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Habari!

Twende kwenye hoja.

Mateja au kuongezeka kasi ya matumizi ya madawa ya kulevya serikali ndio chanzo kikuu.

Kwanini niseme serikali ndio chanzo kikuu cha tatizo hili?

Serikali ndio inayokusanya kodi, hizo kodi ndizo hutumika kuwalipa watumishi wa idara ya polisi, TISS, Uhamihaji, Tume ya kudhibiti madawa ya kulevya, PCCB, Mahakama n.k

Serikali imeshindwa kuviongoza vyombo hivi nilivyovitaja juu kukomesha uteja kwa vijana.

Ukifika asubuhi kesho Temeke Hospital utakutana na mateja mamia au maelfu wanapanga foleni kupokea Methodone (Dawa za kuondoka kiu ya uteja wa madawa ya kulevya).

Hivi serikali imeshindwa kudeal na mizizi ya tatizo kiasi hiki mpaka wanadeal na majani(mateja).

Hizi ni akili?

Serikali imeshindwa kuwakamata mateja angalau 5 waonyeshe mtu anayewauzia, kisha huyo mtu aminywe awapeleke kwa dealer mkuu wao?

Kisha dealer mkuu akipatikana na hatia afungwe maisha.

Tatizo hivyo vyombo juu havisimamiwi ipasavyo katika hili, badala yake wanawageuza ma pusher na mabosi wao kama kitega uchumi.
 
Kuna hao nimeona juzi sijui wanachangaya panadol kwenye sigara. Sijui kidonge ganj kile ila cheupe.

Sijui ndio pack mpya ya unga
 
Wakati Mhe. Makonda akiwa RC Dsm alipambana sana na Wauza Dawa za Kulevya, Shisha, Ushoga, Machinga, Utelekezaji watoto, Migogoro ya Ardhi nk na nafuu ilionekana kwa kiasi kikubwa.

Hapa hapa JF, members sie sie tulimnanga saaaaana mwishowe Makonda akaishia kukashfiwa na kukosa Uteuzi moja kwa moja.

Sasa ongezeko la Mateja ni matokeo yetu, tujitafakari kama jamio maaana hatujui ni kipi tunataka Viongozi watufanyie. Akina SHIKUBA mazungu ya Unga Kimataifa yalitiwa ndaniiii lkn tulibeza na kutukana.

Mwenyezi Mungu atusaidie kila aliyebeza jitihada hizo japo apate watoto Mateja wawili na ndugu wengine mateja kama watatu naaamini akili zitatukaa sawa.
 
Wakati Mhe. Makonda akiwa RC Dsm alipambana sana na Wauza Dawa za Kulevya, Shisha, Ushoga, Machinga, Utelekezaji watoto, Migogoro ya Ardhi nk na nafuu ilionekana kwa kiasi kikubwa.
Hapa hapa JF, members sie sie tulimnanga saaaaana mwishowe Makonda akaishia kukashfiwa na kukosa Uteuzi moja kwa moja. Sasa ongezeko la Mateja ni matokeo yetu, tujitafakari kama jamio maaana hatujui ni kipi tunataka Viongozi watufanyie. Akina SHIKUBA mazungu ya Unga Kimataifa yalitiwa ndaniiii lkn tulibeza na kutukana.
Mwenyezi Mungu atusaidie kila aliyebeza jitihada hizo japo apate watoto Mateja wawili na ndugu wengine mateja kama watatu naaamini akili zitatukaa sawa.
Yule alikuwa anatafuta sifa tu hakuwa mzalendo.
Ni mshenzi tu mla rushwa na mwenye kiburi.
Alipata wapi maghorofa, magari ya fahari ya ya kumzawadia mke wake alipofanya happy birthday?
 
Wakati Mhe. Makonda akiwa RC Dsm alipambana sana na Wauza Dawa za Kulevya, Shisha, Ushoga, Machinga, Utelekezaji watoto, Migogoro ya Ardhi nk na nafuu ilionekana kwa kiasi kikubwa.
Hapa hapa JF, members sie sie tulimnanga saaaaana mwishowe Makonda akaishia kukashfiwa na kukosa Uteuzi moja kwa moja. Sasa ongezeko la Mateja ni matokeo yetu, tujitafakari kama jamio maaana hatujui ni kipi tunataka Viongozi watufanyie. Akina SHIKUBA mazungu ya Unga Kimataifa yalitiwa ndaniiii lkn tulibeza na kutukana.
Mwenyezi Mungu atusaidie kila aliyebeza jitihada hizo japo apate watoto Mateja wawili na ndugu wengine mateja kama watatu naaamini akili zitatukaa sawa.
Kama aliachwa Zungu kwenye ile list ya wauza ngada wakubwa basi tulichezewa maigizo tu.
CCM ndio inabeba waasi wote
 
Yule alikuwa anatafuta sifa tu hakuwa mzalendo.
Ni mshenzi tu mla rushwa na mwenye kiburi.
Alipata wapi maghorofa, magari ya fahari ya ya kumzawadia mke wake alipofanya happy birthday?
Kumbe kumkamata SHIKUBA na wauza Unga wengine ni sifa! Basi usiulize mateja kuongezeka mkuu maaana uwepo wa mateja ni sifa pia kwa mtazamo wako.
 
Habari!

Twende kwenye hoja.

Mateja au kuongezeka kasi ya matumizi ya madawa ya kulevya serikali ndio chanzo kikuu.

Kwanini niseme serikali ndio chanzo kikuu cha tatizo hili?

Serikali ndio inayokusanya kodi, hizo kodi ndizo hutumika kuwalipa watumishi wa idara ya polisi, TISS, Uhamihaji, Tume ya kudhibiti madawa ya kulevya, PCCB, Mahakama n.k

Serikali imeshindwa kuviongoza vyombo hivi nilivyovitaja juu kukomesha uteja kwa vijana.

Ukifika asubuhi kesho Temeke Hospital utakutana na mateja mamia au maelfu wanapanga foleni kupokea Methodone (Dawa za kuondoka kiu ya uteja wa madawa ya kulevya).

Hivi serikali imeshindwa kudeal na mizizi ya tatizo kiasi hiki mpaka wanadeal na majani(mateja).

Hizi ni akili?

Serikali imeshindwa kuwakamata mateja angalau 5 waonyeshe mtu anayewauzia, kisha huyo mtu aminywe awapeleke kwa dealer mkuu wao?

Kisha dealer mkuu akipatikana na hatia afungwe maisha.

Tatizo hivyo vyombo juu havisimamiwi ipasavyo katika hili, badala yake wanawageuza ma pusher na mabosi wao kama kitega uchumi.
Nashangaa hata viongozi wa dini wanafumbia pia jambo hili. Mfano pale msikiti wa Temeke Stereo, vijana wana bwia unga hadharani na Waumini wa pale msikitini wanaona mana nwanajaa hadi wengine wako nje. Ibada inaendelea pembeni mita 10 watu wanabwia. Patrol za Polisi kila siku wanapita pale na wanaona, ila wakiambiwa CHADEMA wako hapa dakika sifuri wamefika na kuzoa wote. sasa hawa Polisi kazi yao nini?
 
"Samaki huanza kuoza kichwani".ukiona hivyo ujue Kuna wenye nguvu wanafaidika na hakuna yeyote atathubutu kuingilia.
Mtoa post umekurupuka hujui kua serikal ni pamoja na mwananch so na wewe ukiwepo unatakiwa uwajibikaj uanzie kwako
 
Tatizo ni kuwa hii biashara ni ya kimataifa na inagusa maslahi ya vigogo wakubwa kwenye idara nyeti na kuidhibiti ni ngumu, dunia hadi leo inahangaika

Sent from my SM-J720F using JamiiForums mobile app
 
Ni ngumu sana kuzuia au kupambana na biashara ya madawa ya kulevya hasa ukizingatia “nature” ya biashara hii ni mtumiaji kuhimiza ongezeko la supply .
Yaani hata wakiwa watumiaji wawili ukuaji wa supply uko na guarantee hii inasababisha biashara hii kuwa na uhakika wa kukua .
Hatuwezi kuondoa supply ya “narcotics” au “ilicit” bali ninachofikiri ni nguvu iongezwe kwenye tiba ya waathirika wa matumizi ya dawa za kulevya .
Vituo vya methadone viimarishwe lakini pia vijengewe uwezo wa kuhudumia waraibu wa aina zote yaani hadi sigara ,bangi na pombe .Kama mtu anataka kuacha basi apewe msaada wa kuacha .
 
Back
Top Bottom