KIOO
JF-Expert Member
- Mar 3, 2013
- 6,235
- 5,854
Ukilangua gunia la mpunga shilingi 50,000 na ukaja kuliuza dar shilingi 80,000 hiyo ,hiyo faida ya elfu 30 sio Riba mkuu??
Sio riba mkuu hiyo ni faida kumbuka kuwa hapo umenunua na umekuja kuuza haijalishi umeuza kiasi gani hata ukiuza milioni sio riba.
Kwenye kuuza na kununua kuna makubaliano ya bei husika ya bidhaa, pia kuna kupunguziana bei kama discount yani vile mtakavyokubaliana na mteja.
Halaf pia, hapo kinachotoka ni bidhaa na inayoingia ni pesa ndugu wala sio vitu vinavyofanana ni vitu viwili tofauti kabisa.
Riba ni pale unapotoa kitu halaf baadae ukaja kurudisha au kulipa kwa zaidi ya ile bei au idadi uliyochukua mwanzo, aidha itategemea na pesa itakavyokuwa kwenye soko la dunia nikimaanisha labda wakati nakupa ilikuwa chini then uliponirudishia hela imepanda unaweza kurudisha kutokana na thamani itakavyokuwa wakati huo unarudisha, ila pia inatakiwa kuangalia wakati mnapeana thamani yake ilikuwaje ili mjue mtakaporudishiana itakuwaje.
Na pia, riba hasa ipo katika vitu au mali au bidhaa zinazofanana nikimaanisha nafaka kwa nafaka, dhahabu kwa dhahabu au fedha kwa fedha. Wala sio bidhaa kwa fedha, au nafaka kwa dhahabu laa.
Inaweza kuwa riba katika mfumo huo pindi tu itakapokuwa mwenye mali akasema bwana ee imekaa siku nyingi kwa hiyo kila baada ya siku kadhaa itaongezeka kiasi kadhaa coz umekaa siku nyingi hapo nayo hiyo itakuwa ni riba ndugu yangu. Kama utakuwa hujaelewa sehemu unaweza ukaniuliza tu nikakuelewesha wala usjali ndugu yangu.
Karibu Sana.