na SACCOS wana vibali vya BOT?kukopesha pesa bila kibali cha BOT ni kosa kisheria. Kibali cha bot ni leseni. Wengi wanaofanya hii biashara hawajui hadi siku wameshindwana kulipana na kupelekana polisi ndio wanajua ni haramu.
Hauwezi kupata maendeleo bila kukopa...Mfanyabiashara anaetumia pesa yake kufanya biashara ni mpumbavu...unatakiwa utumie pesa ya kukopa au hisa ..periodBiashara yeyote, ambayo haipo au haina msingi wa kisheria ni kufukuza upepo. Biashara ya kukopesha mahali popote haina mashiko.. Benki unaona wamechemsha, wanabadilisha riba na mambo kadha wa kadha lakini bado itabuma kwa nini... Wanajaribu kuziba jino lililotoboka, lazima litaachia tu..
Kiukweli ni watu wachache sana wanastahili kukopeshwa na wanaostahili na kufaa kukopeshwa , hawahitaji kukopa . Wale wasiostahili kwa kiwango kikubwa ndio wakopaji, na ndio maana kuna shida .. Unaweza kupanua wigo huo , kuingiza makampuni , mataifa Nk.. Biblia inasema mkopaji ni mtumwa wa mkopeshaji, hapo sasa .
Kauze kitimoto basi..!Kwa imani yangu siwezi jaribu hii biashara.
leseni ya BOT inataka uwe na minimum capital milioni 650.....na fee yake ni milioni 10Mkuu. Ni financial/ lending institutions zenye kibali cha BOT pekee ndio zenye haki kisheria kukopesha na kuweka riba. Hapo kwenye mkataba kwakutumia ujanja hua nawashauri wateja wangu nikiwaandikia mkataba... kwa mfano mtu anakuja kumkopa mteja wangu laki moja na mteja wangu anataka faida ya elfu ishirini.. basi namuandikia mkataba ambao unasema mkopaji amekopwa laki na ishirini bila riba na anatakiwa kurudisha pesa hiyo baada ya mwezi ili hali amechukua laki moja. Ukiweka riba asipolipa mkaenda mahakamani , mkopeshaji imekula kwake kwani mkataba huo utakua hauna nguvu kisheria ( null and void from abi initial) .
Ni haramu na ni money loundaringTunaendelea kujikakamua . Tutatoboa tu.
Kuna mtindo ambao ulianza kama masihara huko nyuma lakini sasa umepamba moto sana na unazidi kuota mizizi mno siku zinavyozidi kusogea.
Kukopeshana hela mtaani kwa riba:
Watu wengi saivi wanakopesha na kukopeshwa kwa riba sana mtaani. Unakuta mtu ana shida ya ghafla anaamua kujitia kitanzi anaenda kwa mtu mwenye vihela kidogo kukopa pesa kwa riba kwa muda fulani.
Mfano: Mtu anaenda kukopa laki 1 kwa siku 30 na atarudisha TZS 160.000 (Riba ni TZS 60.000).
Watu wanakopesha unarudisha 60 % kama faida. Kwa mkopeshaji inalipa sana.Kwa mkopeshwaji inakula sana.
Ni biashara halali au haramu?
Maana siku hizi watu wanakopa mtaani zaidi kuliko benki.