Kuku wa kienyeji kuwa wa mayai

Kuku wa kienyeji kuwa wa mayai

Chamume

Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
12
Reaction score
0
Nisaidieni nataka nifanye kuku wa kienyeji wawe wanatoa mayai kila siku ili niyauze je inawezekana?
 
Inawezekana,kinachotakiwa ni matunzo na chakula bora unaweza ukakiandaa mwenyewe kinakua bora zaidi,pia kuwapatia chanjo za magonjwa hatarishi.
 
Inawezekana,kinachotakiwa ni matunzo na chakula bora unaweza ukakiandaa mwenyewe kinakua bora zaidi,pia kuwapatia chanjo za magonjwa hatarishi.

mkuu unaweza kunipa dondoo za uandaaji chakula cha kuku bora. Wakitaga kama wa mayai wanatoa asilimia ngapi?
 
Hapo kwenye kutoa asilimia sijakuelewa,kuhusu uandaaji wa chakula nitakuandikia usijali.
mkuu unaweza kunipa dondoo za uandaaji chakula cha kuku bora. Wakitaga kama wa mayai wanatoa asilimia ngapi?
 
Kitu chochote mi matunzo kama matunzo hakuna basi mazao hakuna"
Muhimu chakula na maji!!
 
Nenda ukagogle ufugaji kuku wa kienyeji,utakuta kuna pamflet moja imeandaliwa na mradi ...nimesahau jina ila kwa msaada wa Swiss Aid for rural Development utapata kila kitu.mimi mwenyewe nilisoma humuhumu na sasa nina kuku wa kienyeji 250 nategemea mwishoni mwa mwezi huu wataanza kutaga.
 
Nenda ukagogle ufugaji kuku wa kienyeji,utakuta kuna pamflet moja imeandaliwa na mradi ...nimesahau jina ila kwa msaada wa Swiss Aid for rural Development utapata kila kitu.mimi mwenyewe nilisoma humuhumu na sasa nina kuku wa kienyeji 250 nategemea mwishoni mwa mwezi huu wataanza kutaga.

Mkuu.
Ni changamoto zipi unakutana nazo katika huo ufugaji?
 
mpaka sasa sijapata changamoto yoyote ambayo ni kubwa ,mm vifaranga nilinunua kutoka kwa kampununi moja inaitwa BenaChicks wako mbagala,walinipa karatasi inayoonyesha maelekezo yote ya utunzaji(kwa maana ya chanjo, na chakula na nimefuatilia maelekezo sijaona shida yoyote) kwa wastani ktk kuku mia vilikufa vifaranga 2.kwa sasa wanamiezi 3 na 2weeks.majogoo yameshaanza kuwika na yana wastani wa 2kg.
 
Hapo kwenye kutoa asilimia sijakuelewa,kuhusu uandaaji wa chakula nitakuandikia usijali.

natanguliza shukran kwa maelekezo ya chakula unayoyaandaa.

Kwa upande wa kuku wafugwapo kama chanzo cha mayai huwa wanakodolea sana wastani wa idadi ya mayai kwa idadi ya kuku, m.f. ukipata mayai 90 kwa kuku 100 ~90%; matunzo ni bora, na ukipata chini ya mayai 75 kwa kuku 100 ~<75%, matunzo ni dhaifu, labda magonjwa yanasumbua kuku, zingatia mfano hapo juu ni kwa kuku wa kisasa, nategemea wa kienyeji watakuwa chini kidogo.
 
Mtakuwa mnazungumzia Chotara, Ila pure Kienyeji haiwezekani wakawa wanataga kila siku ni lazima wafikie mahali wanastop kwa ajili ya kuatamia, hivyo mambo ya kutaga kila siku ni hakuna hata kama utawapatia chakula cha aina gani,
 
Mtakuwa mnazungumzia Chotara, Ila pure Kienyeji haiwezekani wakawa wanataga kila siku ni lazima wafikie mahali wanastop kwa ajili ya kuatamia, hivyo mambo ya kutaga kila siku ni hakuna hata kama utawapatia chakula cha aina gani,

lakini hata kuku wa kisasa kutaga kila siku haiwezekani maana mzunguko ukifika mwisho lazima atastop ndo aanze tena ndio maana hata ukiwa na kuku 100 wa mayai huwezi okota mayai 100 kwa siku
 
lakini hata kuku wa kisasa kutaga kila siku haiwezekani maana mzunguko ukifika mwisho lazima atastop ndo aanze tena ndio maana hata ukiwa na kuku 100 wa mayai huwezi okota mayai 100 kwa siku
sawa ila kumbuka wa kienyeji baada ya mayai kama 12 ni lazima atake kulalia na kumsahaulisha huchukua si chini ya wiki mbili hadi tatu kuanza kutaga tena.
 
Hapana ni siku 3 mpaka 5,unamtoa nje ya banda na kumlisha vizuri baada ya hapo anaanza kutaga.
sawa ila kumbuka wa kienyeji baada ya mayai kama 12 ni lazima atake kulalia na kumsahaulisha huchukua si chini ya wiki mbili hadi tatu kuanza kutaga tena.
 
Kwa alieuliza kuhusu ratio ya chakula unafanya pumba ya mahindi kg 30,mashudu ya alizeti kg 20,uwele/mtama kg20,pumba ya mchele kg20;dagaa wachafu kg5,mifupa kg5,chokaa kg 1(sio lazima),chumvi pakiti moja hiyo ni kwa kilo mia.
 
Kuku wa kienyeji ni wazuri ila pia unaweza kufuga machotara hawana tofauti sana na hao wa kienyeji,machotara weusi mbegu ya ujerumani ni bora zaidi.
 
mpaka sasa sijapata changamoto yoyote ambayo ni kubwa ,mm vifaranga nilinunua kutoka kwa kampununi moja inaitwa BenaChicks wako mbagala,walinipa karatasi inayoonyesha maelekezo yote ya utunzaji(kwa maana ya chanjo, na chakula na nimefuatilia maelekezo sijaona shida yoyote) kwa wastani ktk kuku mia vilikufa vifaranga 2.kwa sasa wanamiezi 3 na 2weeks.majogoo yameshaanza kuwika na yana wastani wa 2kg.

mkuu unauhakika hao ni kuku wa kienyeji original na sio machotara? Ulinnunua kifaranga kimoja kwa tsh ngapi, me nataka kufuga kuku ila sio chotara nataka kienyeji kabisa, maelezo yako yatanisaidia sana tafadhari
 
Kwa alieuliza kuhusu ratio ya chakula unafanya pumba ya mahindi kg 30,mashudu ya alizeti kg 20,uwele/mtama kg20,pumba ya mchele kg20;dagaa wachafu kg5,mifupa kg5,chokaa kg 1(sio lazima),chumvi pakiti moja hiyo ni kwa kilo mia.

nimefurahia mchanganyiko huu, natumai unakupa tija kwenye ufugaji wako.
Naomba niuchukue kama ulivyo nami uninufaishe, ila sijaelewa kwanini unatumia mifupa na chokaa wakati mmoja.

Shukran.
 
Wakuu nashukuru sana kwa maoni yenu nimejifunza kitu kizuri sana hapa
 
Ndio maana nimeandika sio lazima chokaa ila mifupa ni bora zaidi.
nimefurahia mchanganyiko huu, natumai unakupa tija kwenye ufugaji wako.
Naomba niuchukue kama ulivyo nami uninufaishe, ila sijaelewa kwanini unatumia mifupa na chokaa wakati mmoja.

Shukran.
 
Back
Top Bottom