Kukua kwa Uchumi siyo madaraja na miundombinu tu, bali PPP (Purchasing Power Parity)

Kukua kwa Uchumi siyo madaraja na miundombinu tu, bali PPP (Purchasing Power Parity)

Naona mmefunguliwa koki za kufisadi sahizi kimya tu. Mnajipigia mahela kila kona PPP imekuwa ya uhakika LC300 zinanunulika kwa kasi
 
Namshangaa yeyote anayejinasibu kukuza uchumi wakati bado hali ya Watanzania waliowengi ni maskini hawana uwezo wa kununua hata mahitaji muhimu.

PPP ya Tanzania inazidiwa na Kenya, Rwanda, Uganda

Maswali ya Msingi
1. Wangapi wana uwezo wa kufanya mahemezi ya kila siku.

2. Wangapi Waliokuzunguka wana uwezo wa kwenda dukani kununua sukari, Unga, Mchele na Mafuta ya Kula.

3. Wangapi wana uwezo wa kununua hata hayo maji ambayo ni wajibu wa serikali kuyaleta?

Britannica
Kama hawana uwezo wa kununua walime hata mchicha wauze. Watanzania tunajirudisha nyuma kwa kutaka kununua kila kitu. Hii siyo sawa, tunatakiwa tuzalishe ili tuwauzie wengine. Kumpima mtu kwa uwezo wake wa kununua siyo sawa, tupime kwa uwezo wa kuuza.

By the way mimi niliishi kwenye Kijiji ambacho unaweza kukaa wiki mbili tujanunua kitu sababu magimbi, asali, maziwa, mchele mnazalisha wenyewe.
Vingi vinavyotuongezea umaskini Tanzania siyo basic needs bali wants
 
GDP per Capita PPP in Kenya is expected to reach 6008.00 USD by the end of 2024, according to Trading Economics global macro models and analysts expectations. In the long-term, the Kenya GDP per capita PPP is projected to trend around 6344.00 USD in 2025 and 6731.00 USD in 2026, according to our econometric model

GDP per Capita PPP in Tanzania averaged 2459.61 USD from 1990 until 2023, reaching an all time high of 3580.78 USD in 2023 and a record low of 1670.81 USD in 1994. This page provides - Tanzania GDP per capita PPP - actual values, historical data, forecast, chart, statistics, economic calendar and news.
Mkuu hizi taarifa chanzo chake nni?
 
Mama amekuza uchumi wa watu, sasa hivi hata barabarani tunapishana na ndinga zenye namba E za kutosha
Huo ndio umaskini wa kwanza. Hizo ndinga zingekuwa zinazalishwa na KP motors ya Tanzania ingekuwa tofauti
 
Huo ndio umaskini wa kwanza. Hizo ndinga zingekuwa zinazalishwa na KP motors ya Tanzania ingekuwa tofauti
Waziri wa mambo ya fedha ndio kasema tumepiga hatua, hata benki siku hizi foleni zimekuwa nyingi

 
Bahati Mbaya CCM wamejikita kwenye maendeleo ya vitu, na hawataki maendeleo ya watu. Nchi nyingi huwa zina Balance kote kote, China ina Project za kuondoa umasikini vijijini kwa kuwawezesha watu kaunzisha viwanda vidogovidogo na pia ufugaji na kilimo.

Tanzania hilo halipo tuko busy na madaraja.
 
Mama amekuza uchumi wa watu, sasa hivi hata barabarani tunapishana na ndinga zenye namba E za kutosha
Mitumba au unaamnisha Namba E za Serikali? Mitumba tu ni Dalili za Full Umasikini, ni kipimo tosha kabisa, na pia naona mnahamasisha sana Importations
 
Kama hawana uwezo wa kununua walime hata mchicha wauze. Watanzania tunajirudisha nyuma kwa kutaka kununua kila kitu. Hii siyo sawa, tunatakiwa tuzalishe ili tuwauzie wengine. Kumpima mtu kwa uwezo wake wa kununua siyo sawa, tupime kwa uwezo wa kuuza.

By the way mimi niliishi kwenye Kijiji ambacho unaweza kukaa wiki mbili tujanunua kitu sababu magimbi, asali, maziwa, mchele mnazalisha wenyewe.
Vingi vinavyotuongezea umaskini Tanzania siyo basic needs bali wants
Sikilia nenda Fuatilia Mipango ya India au China au nchi zingine za Asia kwenye kuondoa umasikini, China haondoi umasikini kwenye Raia wao kwa kuwajengea Barabara na Madaraja. China anaondoa umasikini wa vipato kwa kuwawezesha Raia wake kuanzisha viwanda vidogo, ufugaji na kilimo.

Tanzania mnadanganywa sana kwamba mkisha wekewa Rami umasikini unaootea wenyewe.
 
Naona mmefunguliwa koki za kufisadi sahizi kimya tu. Mnajipigia mahela kila kona PPP imekuwa ya uhakika LC300 zinanunulika kwa kasi
Screenshot_20240713_232635_com.facebook.katana.jpg
 
Sikilia nenda Fuatilia Mipango ya India au China au nchi zingine za Asia kwenye kuondoa umasikini, China haondoi umasikini kwenye Raia wao kwa kuwajengea Barabara na Madaraja. China anaondoa umasikini wa vipato kwa kuwawezesha Raia wake kuanzisha viwanda vidogo, ufugaji na kilimo.

Tanzania mnadanganywa sana kwamba mkisha wekewa Rami umasikini unaootea wenyewe.
Sasa mkuu Black ulichoandika na nilichoandika kina tofauti gani? Mimi sijaandika mambo ya madaraja au barabara. Mimi nimeandika tunatakiwa kupima kwa wananchi kuongeza uzalishaji! Soma tena mkuu wangu
 
Back
Top Bottom