Kukutana kwangu na "Deep Throat" wa Madina, Handeni 2014

Kukutana kwangu na "Deep Throat" wa Madina, Handeni 2014

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
KUKUTANA KWANGU NA "DEEP THROAT" WA MADINA, HANDENI 2014​

Angalia hiyo picha hapo chini.

Picha hii nimeipiga miaka saba iliyopita siku kama ya leo.

Picha imeanza kwenye ndevu kuja chini hakuna sura. Hivi ndivyo mwenyewe alivyotaka.

Alitaka sura yake isionekane. Kwa nini anajificha?

Huyu bwana kaja nyumbani kwangu mimi simjui lakini yeye ananijua na nilipomuuliza ananijuaje jibu lake lilikuwa, "Nani asiyekujua Sheikh Mohamed?"

"Wewe nani ndugu yangu?"

"Usitake kunijua mimi nimeelekezwa kwako na Waislam ili nikuekeze mambo mazito yaliyowafika ndugu zetu vijiji vya Lalago na Madina Wilaya ya Handeni."

Pale pale mimi nikampa jina ndani ya nafsi yangu nikamwita, "Deep Throat."

Deep Throat ndiye mtu aliyetoa siri ya Watergate iliyomfanya Richard Nixon ajiuzulu urais wa Marekani.

Hili jina lilinijia haraka kwani wakati huyu Deep Throat wangu ananifikia na kuniambia ana habari za Lalago na Madina nchi ilikuwa katika msisimko na taharuki kubwa.

Taarifa zilikuwa zimezagaa nchi nzima kuwa katika baadhi ya vijiji Tanga kuna kambi za ugaidi, zinazomilikiwa na Al Shabab, kuna mahandaki ya vita na silaha za kutungulia ndege.

Deep Throat wangu alikuja kunipa ukweli wa taarifa hizi na akaniambia kuwa yeye ni mmoja wa vijana waliokuwa wanaishi Madina lakini kakimbia huko baada ya kijiji kuvamiwa na kupita operesheni ya kamatakamata wakisakwa magaidi.

Deep Throat wangu akaniambia huko alikotoka ni hatari kuwa na muonekano wa Kiislam hasa kufuga ndevu na kuvaa kanzu fupi.

Akaniambia kuwa mabasi yanasimamishwa njiani na askari ukionekana na muonekano usiofaa unashushwa na kuwekwa chini ya ulinzi.

Deep Throat wangu alinieleza mambo mengi ya mauaji na misikiti kuchomwa moto.

Mwisho wa mazungumzo akaniambia kuwa katumwa kuja kwangu ili nieleze ukweli kupitia kalamu yangu.

Nilimuomba Deep Throat kabla sijanyanyua kalamu yangu kuandika anipatie ushahidi zaidi wa picha na sauti za waathirika wakieleza haya yaliyowafika.

Deep Throat akaniambia Mkuu wa Mkoa wa Tanga Bi. Chiku Galawa amezungumza na wananchi wa Tanga kuhusu hali ya usalama wa mkoa wake kupitia Radio Nur FM, na kaeleza mengi ya kutisha.

Ndipo katika kuagana kwa miadi kuwa atanipatia ushahidi nilioomba nikamuomba nimpige picha.

Deep Throat akaniruhusu kupiga ndevu zake na alipokuwa anaondoka namsindikiza nikaona kanzu yake iko juu ya fundo za miguu.

Screenshot_20210109-224054.jpg
 
Siku mzee Mohamed Said ukiitwa na mola wako msiba wako watajaa Wana jf wengi Sana naomba ikimpendeza mola niione siku hiyo.
 
Mohamed Said,

..nimecheka ulivyompachika mhabarishaji wako jina la " deep throat. "

..hivi unajua " deep throat " alikuja kujitokeza miaka michache kabla ya kifo chake?

..ila wajuvi wa siasa za Wamarekani wanasema identity ya " deep throat " was the best kept secret in Washington.
 
Hilo neno lina maana mbaya sana, hasa kwenye lugha za mtaani US.

Especially kwa mwanaume. Ndiyo maana nilivyosoma heading nikaangalia inatoka jukwaa gani.
 
Kwahiyo unapenda mwenzako afariki kwanza ili upate nafasi ya kuhudhuria mazishi yake?!--- ukianza kufariki wewe je?!!, wote njia yetu ni moja.
Mokaze,
Unadhani nitapata maziko makubwa?

Maziko makubwa yaliyopata kutokea Dar es Salaam ni haya yafuatayo:

Maziko ya Sheikh Idrissa bin Saad, Sheikh Kaluta Amri Abeid, Abdulwahid Sykes, Sheikh Kassim bin Juma, Mzee Kitwana Dau na Sheikh Ilunga Kapungu.
 
Mohamed Said,

..nimecheka ulivyompachika mhabarishaji wako jina la " deep throat. "

..hivi unajua " deep throat " alikuja kujitokeza miaka michache kabla ya kifo chake?

..ila wajuvi wa siasa za Wamarekani wanasema identity ya " deep throat " was the best kept secret in Washington.
JK,
Nimeona na sura ya Deep Throat wakati mgonjwa yuko kitandani.

Huyu jamaa niliona nimpe jina maana ningwemwandikaje katika shajara yangu?

"Midevu," au "Ndevu," sikulipenda.
 
Mokaze,
Unadhani nitapata maziko makubwa?

Maziko makubwa yaliyopata kutokea Dar es Salaam ni haya yafuatayo:

Maziko ya Sheikh Idrissa bin Saad, Sheikh Kaluta Amri Abeid, Abdulwahid Sykes, Sheikh Kassim bin Juma, Mzee Kitwana Dau na Sheikh Ilunga Kapungu.


Mohamed Said umejuaje kwamba hutopata maziko makubwa ilhali hujui kitakachotokea nyuma yako baada ya kifo chako??!
 
Mokaze,
Unadhani nitapata maziko makubwa?

Maziko makubwa yaliyopata kutokea Dar es Salaam ni haya yafuatayo:

Maziko ya Sheikh Idrissa bin Saad, Sheikh Kaluta Amri Abeid, Abdulwahid Sykes, Sheikh Kassim bin Juma, Mzee Kitwana Dau na Sheikh Ilunga Kapungu.
Pyeeeeh.....

Unachekesha sana Mzee Mohamed Said

Hayo ni maziko makubwa kwa mujibu wa msiba uliohudhuria wewe au unayoikumbuka na ni kwa watu wa Imani yako ya kiislam

Au wewe ulishahudhuria mazishi yote ya Dar es salaam na ukagundua hilo?
 
Naona mnakaribisha hisia za kigaidi.
Hakuna nafasi awamu hii muende Mozambique [emoji1174] au mtulie mpaka Hussein Mwinyi aapishwe wa Muungano 2035.
 
Pyeeeeh.....

Unachekesha sana Mzee Mohamed Said

Hayo ni maziko makubwa kwa mujibu wa msiba uliohudhuria wewe au unayoikumbuka na ni kwa watu wa Imani yako ya kiislam

Au wewe ulishahudhuria mazishi yote ya Dar es salaam na ukagundua hilo?
Azarel,
Kuchekeshana ni jambo zuri kwani huingiza furaha moyoni.

Ikiwa unahisi haya hayakuwa maziko makubwa si neno.

Lakini katika maziko ya Abdul Sykes Mwalimu Julius Nyerere alifika nyumbani kwa Mama Abdul Bi. Mruguru bint Mussa Mtaa wa Lindi, Gerezani mapema sana.

Alikaa kwenye jamvi barazani pale pamoja na Ahmed Rashad Ali na watu wengine mashuhuri wa Dar es Salaam ambao wengi wao walimfahamu Nyerere kwa kumuona akiwa na Abdul Sykes.

Vijana wa Usalama siku ile walimwagwa wengi Gerezani nzima kwani ulikuwa wakati wa mgogoro wa East African Muslim Welfare Society (EAMWS).

Kulikuwa na hofu kidogo kuhusu usalama wa Nyerere.

Idara ya Usalama ilishauri Mwalimu asihudhurie mazishi yale.

Rashid Kawawa akapinga vikali akamwambia Mwalimu kuwa watu wasingemjua ila kwa kupokelewa na Abdul na kuishi kwake hadi alipohamia Magomeni Majumba Sita na baina yao kuna hisani kubwa sana kuanzia TAA hadi TANU.

Mwalimu akaambiwa kuwa Chifu Abdallah Said Fundikira wakati ule Mwenyekiti wa East Agrican Airways kaja kutoka Nairobi kuhudhuria maziko ya Abdul na mtaa haupitiki kwa umma uliokusanyika nyumbani kwa Bi. Mluguru.

Mwalimu alihudhuria maziko na akapeleka ng'ombe mzima kama kitoweo.

Mwalimu alitembea kwa miguu kutoka Mtaa wa Lindi hadi Msikiti wa Kitumbini yuko nyuma ya jeneza la Abdul na akasimama nje msikitini anasubiri maiti isaliwe.

Muhindi mmoja mwenye duka karibu na msikiti akachukua kiti kumwekea Mwalimu akae.

Mwalimu alikataa kukaa akabaki amesimama.

Kutoka hapo Mwalimu akalisindikiza jeneza la Abdul Sykes hadi Makaburi ya Kisutu.

Umma uliohudhuria maziko yale ulikuwa haujapata kuonekana Dar es Salaam.
 
Hasa ukiwa na muonekano usiofaa!!
Unamaanisha midevu na kanzu fupi ni muonekano usiofaa Hadi ushushwe kwenye gari?
 
Hasa ukiwa na muonekano usiofaa!!
Unamaanisha midevu na kanzu fupi ni muonekano usiofaa Hadi ushushwe kwenye gari?
Kadhi...
Ukionekana uso umejaza ndevu na kanzu yako fupi wameshakutambua kuwa wewe ni Ansar kwa hiyo unatakiwa kuhojiwa huko uendako Handeni ndiyo makazi yako au unatembelea ndugu na jamaa?

Ikiwa hukai huko nini kinakupeleka na watahitaji kuwajua wenyeji wako.

Hakika kilikuwa kipindi kigumu sana kwa Waislam wa Handeni.
 
Back
Top Bottom