Kwa kuwa hii ni Forum, ngoja tuandike,
Wahenga walisema "Umoja ni Nguvu, Utengano ni Udhaifu". Ifike Wakulima waungane. Hapa nina maanisha Umoja halisi sio umoja wa Vyama vya Ushirika tunavyoviona leo kama vya KCU, NCU, n.k.
Ninaamini Wakulima wodogo wadogo, yaani wenye mitaji midogo wakiungana wanaweza kutetea haki zao, kupambana na utapeli na dharau kubwa inayoendeshwa na Serikali, Madalali wanajiita Wafanyabiashara na Taasisi nyingine nyingi. Hili linawezekana.
Ninaamini Wakulima wa Kati wanaweza kuunda Umoja wao vile vile na kupata manufaa kama niliyoyataja hapo juu.
Sambamba na hao, Wakulima wakubwa, kama wapo, wanaweza kufanya hivyo hivyo.
Kwa Wakulima Wadogo na wa Kati Umoja wao unaweza kuwa katika ngazi ya eneo walilomo, yaani Wilaya hata Mkoa. Hili linawezekana kabisa.
Kama sehemu ya Forum hii, huwa ninatamani sana wenye Ujuzi wa Sheria watueleweshe Sisi Wana-Umma ni Sheria zipi zinatumika kumzuia Mkulima mdogo asiuze Mazao yake nje ya Wilaya/Mkoa wake. Mpango wa Biashara Huria una Mipaka gani, kwa nini Wakulima wawekewe mipaka na vikwazo kibao? :A S confused: