Rafiki yangu kamchukua bajaji anaemtakaga eti ampeleke Tabata Segerea kwa boyfriend bure. Nikamuuliza yani unataka kaka wa watu akupeleke sehemu ya elfu 20 bure kisa tu anakutaka akasema eeeh akome kutongoza asivyoviweza. Nikamwambia aone haya kidogo na huruma maana hiyo unaweza kuta ndo anajazia apeleke hesabu kwa boss akacheka akaondoka tena anasema akifika huko njiani akiona vitu atamwambia amnunulie pia.
Nimumeonea huruma dereva wa watu maskini maana atakua anatumika hivyo hivyo na tamu tamu hatapewa. Kuna watu wakuwalia hela zao hata kama humtaki ila sio dereva wa bajaj halafu hata kumpooza hamna. Ndo maana wanaume huwa wanatuua wakati mwingine wakijua mwanamke anacheat maana wanatafuta kwa nguvu kutuhudumia halafu tunawasaliti.
Wanawake wenzangu ukiona mtu ana kipato chake kidogo na anakipata kwa tabu usile hela yake wapo watu kibao wapigaji na wanafanya kazi nzuri tuwalieni hao.