Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,809
- 15,421
Hivi umeshawahi kuona ndoa ambapo zinafumuka ngumi kati ya ndugu wa mke na wale wa mume, humohumo kwenye nyumba ya wanandoa? Kama hujawahi, una bahati mbaya tu, kwani ni nyingi za kutosha ndoa za aina hiyo.
Ni ndoa ambazo, ndugu wa mume wanatafutana usiku na mchana na wale wa mke. Kila upande unajaribu kutafuta ushindi ili ndiyo uwe unashikilia nyumba kimamlaka. Hawa ndugu wa mume au mke, mara nyingi ni wale wanaoitwa kula-kulala. Au ni wale wanaoamini kwamba, mradi fulani ni ndugu yake anayo haki ya kuvaa nguo yake ya ndani muda wowote akishikwa na hamu ya kufanya hivyo.
Lakini bila shaka ufa ambao umejengwa na wanandoa wenyewe, ndiyo unaoruhusu hali kama hii. Hawa ndugu wanatumia udhaifu huo kupata kile wanachohitaji, siyo kwamba ni kweli wanawapenda hao ndugu zao. Ingekuwa wanapenda, wangewasaidia kuwaunganisha kwa njia mbalimbali.Kwenye nyumba nyingi, ugomvi au mvutano kati ya ndugu wa mume na wale wa mke ni wa chinichini sana, lakini unasaidia kwa nguvu ileile kuvunja uhusiano wa wawili ambao waliapa kwamba, kifo ndicho kitawatengenisha.
Hatimaye kinachowatenganisha siyo kifo, bali ndugu. Mtu unajiuliza, ni kwa faida ya nani na kwa nini ni lazima iwe hivyo.Ndoa inaweza kuwa na matatizo, lakini kuwepo kwa matatizo hakuna maana ya ndugu kuruhusiwa kuiingilia na kuwafanya wanandoa kama wanasesere. Sina maana kwamba, ndugu wasipokuwepo ndoa ndiyo itakuwa nzuri, hapana. Lakini, ninachosema ni kwamba, ndoa ni zao la watu wawili ambao waliamua kwa hiyari yao kulizalisha. Wanapoamua zao hilo liwe ni kondoo na mbwa mwitu wanaonesha ni kwa kiasi gani uwezo wao wa kufikiri ni mdogo sana.
Kama watu bado wanaishi pamoja, bila kujali wanapigana kutwa mara ngapi, wana haki ya kulinda ndoa yao isiingiliwe na watu wengine. Tukumbuke kwamba, kuna watu ambao wako tayari kuuwa mtu ili wapate wanachotaka kutoka kwetu sisi ndugu zao au watoto wao. Kwa sababu hiyo, kwa ushabiki wao, tunaweza kujikuta tukiwauwa wapenzi wetu na hivyo kubadili kabisa historia ya maisha yetu.
Kama tunagombana sana au kama hatuna mawasiliano, tusifanye udhaifu huo ukaonesha ujinga wetu kwa ndugu na jamaa zetu. tugombane, tushindwe kuwasiliana, lakini iwe ni siri yetu.
Ni ndoa ambazo, ndugu wa mume wanatafutana usiku na mchana na wale wa mke. Kila upande unajaribu kutafuta ushindi ili ndiyo uwe unashikilia nyumba kimamlaka. Hawa ndugu wa mume au mke, mara nyingi ni wale wanaoitwa kula-kulala. Au ni wale wanaoamini kwamba, mradi fulani ni ndugu yake anayo haki ya kuvaa nguo yake ya ndani muda wowote akishikwa na hamu ya kufanya hivyo.
Lakini bila shaka ufa ambao umejengwa na wanandoa wenyewe, ndiyo unaoruhusu hali kama hii. Hawa ndugu wanatumia udhaifu huo kupata kile wanachohitaji, siyo kwamba ni kweli wanawapenda hao ndugu zao. Ingekuwa wanapenda, wangewasaidia kuwaunganisha kwa njia mbalimbali.Kwenye nyumba nyingi, ugomvi au mvutano kati ya ndugu wa mume na wale wa mke ni wa chinichini sana, lakini unasaidia kwa nguvu ileile kuvunja uhusiano wa wawili ambao waliapa kwamba, kifo ndicho kitawatengenisha.
Hatimaye kinachowatenganisha siyo kifo, bali ndugu. Mtu unajiuliza, ni kwa faida ya nani na kwa nini ni lazima iwe hivyo.Ndoa inaweza kuwa na matatizo, lakini kuwepo kwa matatizo hakuna maana ya ndugu kuruhusiwa kuiingilia na kuwafanya wanandoa kama wanasesere. Sina maana kwamba, ndugu wasipokuwepo ndoa ndiyo itakuwa nzuri, hapana. Lakini, ninachosema ni kwamba, ndoa ni zao la watu wawili ambao waliamua kwa hiyari yao kulizalisha. Wanapoamua zao hilo liwe ni kondoo na mbwa mwitu wanaonesha ni kwa kiasi gani uwezo wao wa kufikiri ni mdogo sana.
Kama watu bado wanaishi pamoja, bila kujali wanapigana kutwa mara ngapi, wana haki ya kulinda ndoa yao isiingiliwe na watu wengine. Tukumbuke kwamba, kuna watu ambao wako tayari kuuwa mtu ili wapate wanachotaka kutoka kwetu sisi ndugu zao au watoto wao. Kwa sababu hiyo, kwa ushabiki wao, tunaweza kujikuta tukiwauwa wapenzi wetu na hivyo kubadili kabisa historia ya maisha yetu.
Kama tunagombana sana au kama hatuna mawasiliano, tusifanye udhaifu huo ukaonesha ujinga wetu kwa ndugu na jamaa zetu. tugombane, tushindwe kuwasiliana, lakini iwe ni siri yetu.