Sie ni wazee wa vice versa, asubuhi chai vitumbua viwili, mchana na usiku ndipo tunapiga milima ya nguvu haswa kumbe kile cha asubuhi ndio kilitakiwa kiwe cha usiku
Hilo nalielewa mkuu ila kibongobongo ndio tumelelewa hivyo kiasi kwamba imekuwa mazoea ya kunywa chai na andazi 2 au chapati, huwa ninajitahidi weekend maana katikati ya wiki na mishemishe za kuamka asubuhi unakuta hata muda wa kupata heavy breakfast hakuna waandaaji wamechoka na majukumu ya jana yakeweka bajeti yako kubwa asubuhi maana baada ya breakfast ndo kazi nyingi na nzito za maendeleo zinatakiwa zikafanyike na sio mchana wala usiku, usiku unahitaji nguvu kidogo tu ya kupapasiana gizani ambayo itabidi pia uilipe asubuhi utakapoamka kwa msosi wa nguvu. Hebu siku moja nenda kaone breakfast ya mchezaji wa Real Madrid au Wayne Rone utakimbia na hutaamini kama ataumaliza huku wachezaji wetu wakila vitumbua viwili na chapati moja wanayodaiwa na Mwina Kaduguda hadi leo, ha.
kavulata naomba tena maelezo ya hapo uliposema usinywe chai ya maziwa,kwanini tusinywe?
everlenk niwie radhi kwa kuchelewa kukujibu kuhusu chai ya maziwa, sijui kama upo kwenye uzi.
Maziwa Maziwa Maziwa!
Maziwa yana protein ya wanyama ambayo kutokana na mchakato wa umeng'enyaji tumboni tumesema unakinzana kwa kiasi kikubwa na mchakato wa umeng'enyaji wa carbohydrates tumboni pia, hivyo haifai kuchanganya tumboni kwako sukari, chapati/vitumbua/bagia/mkate/tambi (CHO) na maziwa (kwenye chai). Hivyo tunashauriwa maziwa yanywewe kama maziwa kwa wakati wake bila kuongezwa sukari wala akina chapati.
LAKINI pia: maziwa yana Calcium nyingi sana na sukari aina ya lactose nyingi. Kwa asili na kwa maumbile ya Mwenyezi Mungu maziwa ni kwa watoto wachanyanga wa binadamu na wanyama wengine wanaonyonyesha (mamalia). Watoto wachanga wanayo miundombinu madhubuti inayowezesha mtoto kunywa/kunyonya, kumeng'enya, kusaga na kufyonza mwilini protein, sukari (lactose) na mazagazaga yote yaliyomo kwenye maziwa kwa urahisi. Miundombinu hii muhimu kwa usagaji wa maziwa inatoweka polepole kadri umri wa mtu unavyoongezeka. Hivyo, Watu na wanyama wakubwa hawapaswi kunywa maziwa hata kidogo maana miili yao imeshapoteza enzymes muhimu (renin) kwa usagaji maziwa tumboni, hatuwezi kuitumia protein iliyoko kwenye maziwa kama walivyo watoto wachanga. Mfano, kati ya watu wazima 10 watakaokunywa maziwa fresh au chai ya maziwa 6 kati yao huwa wataharisha, tumbo kujaa gesi, kunguruma na kuuma (lactose intolerance) muda mfupi baada ya kunywa maziwa kwasababu ya kukosa mmeng'enyo muhimu unaohitajika kumeng'enya sukari (lactose) iliyomo kwenye maziwa.
Mungu hakutengeneza maziwa kwaajili ya watu mazima ila watoto tu, ndio maana anatukomesha tunaokunywa maziwa ya watoto kwa kuharisha, kujaa gesi tumboni na vidonda vya tumbo kwa kunywa maziwa. Wako watu wazembe wanaokunywa maziwa wakizani kuwa maziwa yatawaponya vidonda vya tumbo, huu ni ujinga, usinywe maziwa hata kidogo kama unahisi kuwa una vidonda vya tumbo maana utakiona cha mtema kuni kama una ulcers halafu unakunywa maziwa.
somo zuri, barikiwa
Powa, somo hili ni gumu kuingia akilini kwakuwa wengi tumekwishazoea kula namna tunavyokula leo. Lakini fanyeni utafiti mdogo tu wa kufuatilia milo na tabia zao za kula watu wenye magonjwa/shida za kansa, pressure, unene kupita kiasi, kiharusi (stroke), kisukari, mafigo, ini, ugumba, na uhanithi. Fuatilia magonjwa ya watu wanaofanya kazi zifuatazo: wauza nyama buchani na machinjioni, supu na nyama choma, mama na baba lishe, wapishi mahotelini, wawindaji porini, wabunge na wafanyakazi wa ofisini na wala nyama maarufu utagundua kitu kinachofanana.
hakuna kitu kibaya kama kuishi kwa mazoea, nyakati zinabadilika so kuendelea kung'ang'ania 'eti mababu' walikula hivyo ni hatari zaidi maana nyakati zao na zetu ni tofauti mno.
Hiyo ni kweli kabisa, tusiishi kwa mazoea, siri kubwa ya afya yako imejificha kwenye vyakula unavyokula, chips/kuku, chips/mayai/nyama choma vitakuletea tu sifa bandia za mahips, matako makubwa, mapaja makubwa, miguu (usafiri) mikubwa, kitambi, shingo kubwa yenye mikunjo lakini afya mbaya mbaya mbaya mbaya kansa, pressure, ugumba, uhanithi kitandani, kisukari, fangasi zisizoisha, allergies, kushindwa kupumua, mafigo, n.k.
dhaa mkuu somo ni zuri na pia ni gumu kwel kweli...... natumah wote tuki fata hapa.....tutapunguza foleni hospitalini.......
nini kazi ya naji ya moto mwilini...? I mean kama ukinywa kila Asubuh.....
Sio kila kinacholiwa kinaweza kuliwa wakatiti wowote. Leo nitawapeni kwa uchache elimu kuhusu ulaji wa vyakula.
Vyakula vimegawanyika katika makundi makuu 6 ya kutia nguvu, kujenga mwili, kulinda mwili, kutia joto, madini na maji.
1. Katika kundi la Vyakula vya kutia nguvu (carbohydrates) viko mahindi, ubwabwa, uwele, ulezi, ngano, mihogo, mtama, viazi, maharage, kunde, n.k. Usagaji na ufyonzwaji mwilini wa kundi hili la vyakula unahitaji vimeng'enyo vinavyohitaji mazingira yasiyokuwa na acid kali, yaani vinahitaji alkaline environment kuanzia mdomoni hadi tumboni na kwenye utumbo.
2. Katika kundi la vyakula vya kujenga mwili (proteins) viko nyama za aina zote, mayai, maziwa. Usagaji wa vyakula hivi vinapoliwa unahitaji vimeng'enyo (enzymes) vinavyohihitaji kufanyakazi kwenye mazingira ya uchachu (acid) mwingi tumboni. Yaani kwenye alkaline environment nyama, maziwa, mayai havisagwi na kufyonzwa vizuri mwilini.
Ushauri: Kuhusu kula vyakula vya Carbohydrates na Protini: Usichanganye kwa wakati mmoja makundi haya mawili ya vyakula kwenye mlo mmoja li kuurahisishia mfumo wako wa chakula katika kusaga chakula ulichokula.
Kama utavichanganya pamoja mwili wako utavyonza sumu nyingi kutoka tumboni zinazotokana na kuoza (ferment) kwa chakula ambacho kinachelewa kusangwa tumboni, pia unaweza kupata kansa ya tumbo na utumbo. unashauriwa Kula ugali/ubwabwa na maharagwe, nyegele, choroko, dengu, n.k badala ya kula ugali/ubwabwa pamoja na nyama, mayai au maziwa ili kusaidia tumbo kusaga chakula haraka. Kula nyama, maziwa au mayai masaa 3 kabla au baada ya mlo wenye vyakula vya kutia nguvu.
3. Katika kundi la vyakula vinavyolinda mwili yapo matunda na mboga za majani. Matikiti maji ni miongoni mwa matunda yanayopendwa duniani kote yenye madini mengi hasa mbegu zake, LAKINI sasa tikiti maji na nyanya (oxalate) vina tabia mbaya ya kuzuia usagaji na ufyonzwaji wa aina nyingine za vyakula na virutubisho (madini na vitamins) na kuukosesha mwili rutuba na kusababisha vyakula kukaa sana tumboni. Matikiti maji yanapoliwa na vyakula vingine kwa wakati mmoja yanaweza kusababisha hali ya kujisikia kichefuchefu pia.
Ushauri:
a) Kuhusu tikitimaji: tikiti maji liliwe masaa 3 kabla au baada ya kula vyakula vingine.
b) Usile chakula pamoja na nyanya mbichi, nyanya ina kemikali (oxalate) inayozuia virutubisho vingine kufyonzwa haraka mwilini.
c) Kula vyakula vya carbohydrates na proteins pamoja na mboga za majani (greens) ili kuboresha usagaji na ufyonzwaji wake.
d) Maji yana tabia ya kupunguza kasi ya kusaga na kumeng'enya chakula tumboni, hivyo usinywe maji wakati wa kula, kunywa maji saa 1 baada au kabla ya mlo.
e) Kuchanganya nafaka (mahindi, mchele, mtama, ulezi, ngano, n.k) kwenye mlo mmoja hakuleti faida yoyote ya kiafya mwilini, aina moja tu ya nafaka ambayo haikukobolewa sana inaleta faida inayokusudiwa. epuka gharama zisizo za lazima kwa kuchanganya aina nyingi za nafaka au proteins (mayai, nyama, maziwa, samaki) kwa wakati mmoja kwenye mlo mmoja, hakuna faida kiafya kufanya hivyo.
f) epuka kuchanganya matunda baridi (matango, matikiti, parachichi, ndizi, karoti, n.k) na yale makali (machungwa, passions, ukwaju, mabungo, matofaa, maembe, zabibu, ndimu, limau, n.k) kwenye mlo mmoja au kuyachanganya na sukari. Yaani kula tango tu, au chungwa tu, au tikiti maji tu au ndizi tu kwa wakati mmoja.
g) Vyakula vilivyochachuka kama vile mtindi, kabichi, togwa, mbege, mvinyo vinasadia kusaga chakula haraka tumboni. Ukivipata usiviache.
h) Kunywa maziwa peke yake kwa wakati wa peke yake, angalau nusu saa kabla au baada ya kula milo ya aina nyingine au dawa. Epuka chai za maziwa pia kama unaweza.
Usiku: Usiku mwili unahitaji protein zaidi ili kupata matofali (amino acids) ya kuujenga mwili na kurekebisha sehemu za mwili zilizoharibika na kuumia wakati wa mchana. Wakati wa kulala mwili hauhitaji chakula kingi cha kutia mwili maana kazi zinazohitaji nguvu nyingi hakuna. Hivyo, ni marufuku kula sahani ya ugali/ubwabwa na kwenda kupanda kitandani kulala wakati huo huo, maana chakula hakitasangwa vizuri na mwili utatengeneza sumu nyingi sana na kuwa na uwekezano wa kuota ndoto mbayambaya tu usiku kucha.
Asubuhi: Mwili unahitaji chakula cha kutosha cha kutia nguvu, na matunda, juice, siagi, asali, sukari, mkate, kiporo cha ubwabwa ili kuupatia mwili nguvu nyingi za kuendesha mitambo ya mwili inayohitaji nguvu (break fast). Ianze siku yako kwa mlo wenye rutuba zote na kukutia nguvu nyingi sana.
Kama una swali lolote kuhusu namna ya kuchanganya vyakula uliza ujibiwe! Asalam aleykum.
Mama Yang amepata tatizo la figo amembiwa asipate potassium food na fruits naomba ushauri ni matunda gani hayana potassium na vyakula pia.asante
Asante sana Kavulata kwa somo zuri. Mm nina tatizo la acid reflux/heartburn,nimetumia dawa za kustop stomach acid production (ppi) but napata nafuu kdg,then hali inajirudia. Naomba nipe meal diet ya tatizo langu. Shukrani!