Kuletewa Balozi mtaalamu wa Ulinzi wa Masuala ya Mitandao ni 'Diplomatic Gesture' ?

Kuletewa Balozi mtaalamu wa Ulinzi wa Masuala ya Mitandao ni 'Diplomatic Gesture' ?

Kwa wale mliofatilia tukio la kukabidhi hati Ikulu Magogoni kwa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa Tanzania, mtakuwa mlisikia kuwa Balozi mpya wa Italy nchini ni mbobezi wa masuala ya 'Cyber Security'

Je hii ni diplomatic gesture? Kwamba viongozi wetu wakubwa wameonekana kulalamika dharani 'mambo ya mitandaoni' hasa yule wa Twita. Mawaziri, Wabunge, IGP, Spika, marehemu,wastaafu na Mama sasa hivi kwa nyakati tofauri wamemgusia yule wa kwenye 'Twita' na hivyo kuonesha ni tatizo huku kukiwa na uvujaji mkubwa wa taarifa. Kumekuwa na tetesi za kutumika rasilimali watu, fedha na muda bila mafanikio

Mimi sina ujuzi wowote wa masuala ya kidiplomasia lakini kuletewa Balozi mtaalamu na mjuzi wa masuala ya ulinzi wa mitandao je ni namna ya ku 'offer' huduma kusaidia kutatua matatizo? Kwamba mtu anajua una shida lakini hawezi kuanza kutoa msaada anakuwekea mazingira na kusubiri uombe wewe mwenyewe.

Tukumbuke pia kipindi hiki cha mlipuko wa ugonjwa wa Covid US wametuletea Daktari wa binadamu

Wataalamu wa Diplomasia karibuni
Angekuja Pierluigi Collina sijui ungeuliza kama amekuja kusaidia marefa wa soka la Bongo!?
 
Na kweli mama anafungua nchi ! Yaani sasa hivi mpaka balozi anachambuliwa na raia !?.hakika kazi iendelee

Nadhani kwa 'uwazi' huu hata sisi mabalozi wetu nje watakuwa wanateuliwa kufuatana na utumishi uliotukuka kwa nchi huku wakikidhi vigezo tosha vya kuwakilisha maslahi ya Tanzania nje yakiwemo masuala ya weledi mfano wa biashara, uchumi, ushawishi wa kuvutia wawekezaji, kujenga mahusiano mema ya kuwezesha miradi mikubwa iwe ya elimu, miundo-mbinu ya usafirishaji na kuvutia viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo, uvuvi na ufugaji kufanyika Tanzania.

Tanzania iachane kuteua mabalozi wake kwa kuwa "wamestaafu na kuchoka" waende kupumzika huko nje au tu kama hisani bila kujali kwanza maslahi ya nchi kwanza yatakayo pelekea ajira nyingi kupatikana mikoani na wilayani kupitia viwanda vya kuchakata mazao huko huko wilayani badala ya kukaribisha jeshi la machinga wanaouza ndala mikononi DSM kutokana na ukosefu wa ajiri huko kwao wilayani.
 
27 September 2017

"Why Turkey Stands Out as a Humanitarian Actor" - Dr. Mehmet Güllüoğlu


source : Turkish Heritage Organization
 
Kaeni kimya sisi tunaye Balozi Bashiru Ally Kakurwa bingwa wa KUNUNUA WAPINZANI NA KUIBA KURA KWENYE UCHAGUZI.
 
Balozi anatakiwa awe na maarifa mengi ili kusimamia maslahi ya taifa lake, hivyo hata Tanzania mabalozi wetu wanaoteuliwa kuiwakilisha Tanzania nchi za nje lazima wawe na ubobezi wa aina fulani kufikia maslahi na malengo ya diplomasia ya kiuchumi.

Mmm sio mbona wanapelekwa wazee kaka wastaafu
 
Narudia tena kauli yangu! Watanzania tukizaliwa tu tunakuwaga waganga wa kienyeji wapiga ramli ila kwa jinsi tunavyozidi kukuwa taaluma inapotea.
Tuna vinasaba vya uganga wa kienyeji...hasa wanaonedesha bodaboda
 
Kama yule kada aliyetaka kupewa ukurugenzi TPDC😂😂😂
Mkuu mngony wenzetu wapo mbali sana!
Sisi tumekariri mwafulani tumtupe wapi na kujuana kwingi pasipo kuangalia matunda ya mteuliwa ktk masrahi ya taifa.
 
Wewe umejuaje?

Kama ni kweli unataka kusema MTALIANO yupo tayari kufanya kazi na serikali ya Tanzania, je sisi(Tanzania) tunam OFFER nini iwe yeye binafsi au serikali ya ITALY?

Tukumbuke tumesha OFFER gesi kwa nchi ya Afrika mashariki ili tupeleke mahindi na sio sembe.
 
TANZANIA YENYE USHAWISHI KATIKA GEOPOLITICS NA DIPLOMASIA CHINI YA RAIS ALI HASSAN MWINYI
Viongozi wa zamani wa Tanzania marais na mawaziri walikuwa wana uwezo mkubwa wa kushawishi kwa soft power katika siasa za ki geopolitics na kidiplomasia kwa lugha ya Kiingereza na Kiswahili na hili pia kuonekana kutiririka mpaka kwa mabalozi kama Augustine Mahiga , Ami Mpungwe, John Malecela, Salim Ahmed Salim n.k:

Rais Ali Hassan Mwinyi wa Tanzania ambaye ni balozi namba moja na waziri wa mambo ya nje Joseph Rwegasira balozi namba 2 wa nchi ya Tanzania katika Mkutano wa Rwanda Peace Accord wakitiririka kwa umahiri kuanzia dakika 14:40' kushawishi makundi ya Rwanda kuweka silaha chini



After one long year of peace negotiations, the Rwanda government under President Juvenal Habyarimana and the rebel Rwanda Patriotic Front led by Colonel Alexis Kanyarengwe signed a peace accord in Arusha, Tanzania. The historic date was 4th August 1993, raising hopes that the civil war, which started when RPF invaded Rwanda from Uganda on 1st October 1990 was coming to an end. The event was witnessed by several world leaders, including Uganda’s Yoweri Museveni and Melchior Ndadaye of Burundi.
Source: OWANAPAEDIA
 
Kwa wale mliofatilia tukio la kukabidhi hati Ikulu Magogoni kwa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa Tanzania, mtakuwa mlisikia kuwa Balozi mpya wa Italy nchini ni mbobezi wa masuala ya 'Cyber Security'

Je hii ni diplomatic gesture? Kwamba viongozi wetu wakubwa wameonekana kulalamika dharani 'mambo ya mitandaoni' hasa yule wa Twita. Mawaziri, Wabunge, IGP, Spika, marehemu,wastaafu na Mama sasa hivi kwa nyakati tofauri wamemgusia yule wa kwenye 'Twita' na hivyo kuonesha ni tatizo huku kukiwa na uvujaji mkubwa wa taarifa. Kumekuwa na tetesi za kutumika rasilimali watu, fedha na muda bila mafanikio

Mimi sina ujuzi wowote wa masuala ya kidiplomasia lakini kuletewa Balozi mtaalamu na mjuzi wa masuala ya ulinzi wa mitandao je ni namna ya ku 'offer' huduma kusaidia kutatua matatizo? Kwamba mtu anajua una shida lakini hawezi kuanza kutoa msaada anakuwekea mazingira na kusubiri uombe wewe mwenyewe.

Tukumbuke pia kipindi hiki cha mlipuko wa ugonjwa wa Covid US wametuletea Daktari wa binadamu

Wataalamu wa Diplomasia karibuni
Sasa Mzee wangemleta Gatuso au Paul Maldini ingemaanisha nini ?
 
2 Jul 2012

Political Transition in Somalia: The Roadmap​


UN Special Representative for Somalia, Augustine P. Mahiga, lays out the roadmap of the country's political transition by August 2012. In the coming months, Somalia will elect both an inclusive new parliament and government.

Source : the United Nations Political and Peacebuilding Affairs

Source : Augustine P. Mahiga
Before joining the Tanzanian Foreign Service in 1983, Mr. Mahiga worked in the President’s Office as Acting Director General and Director of Research and Training from 1977–1983. He served in various capacities with the United Nations High Commission for Refugees (UNHCR), including as Chief of Mission to Liberia, Coordinator and Deputy Director of the humanitarian and refugee crisis in the Great Lakes Region, and UNHCR Representative in India, Italy, Malta, the Holy See and the Republic of San Marino.


Mr. Mahiga holds a PhD in Philosophy and International Relations from the University of Toronto, Canada. READ MORE
: Secretary-General Appoints Augustine P. Mahiga of United Republic of Tanzania Special Representative for Somalia | Meetings Coverage and Press Releases
 
Back
Top Bottom