Kuliko kukopa ili kushusha bei ya mafuta kwanini tusitumie Tozo zetu kufanya hivyo

Kuliko kukopa ili kushusha bei ya mafuta kwanini tusitumie Tozo zetu kufanya hivyo

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2019
Posts
9,863
Reaction score
20,806
Wakuu,

Waziri wa fedha alitangaza tozo zilizopitishwa na Bunge letu,na kujinasibu kuwa tumekusanya fedha nyingi Sana za tozo.

Kwa kuwa lengo la tozo hizi zilikuwa kujenga madarasa na vituo vya afya nchini lakini tulikopa tena kwa ajili ya ujenzi huo.

Kwanini tozo zile tusitumie kushusha bei ya mafuta nchini kuliko kukopa tena na tena kwa hatujui mfumuko huu wa bei utadumu kwa muda gani Duniani!je tutaendelea kukopa kama mfumuko wa bei utadumu?

Waziri wa fedha ameacha kutangaza kiasi cha mapato ya tozo zile Hadi leo!Mwambieni atuambie kiasi GANI tunacho Hadi Sasa Ili tuelekeze kwenye mafuta tushushe bei na kupambana na mfumuko wa bei nchini.

Hatuwezi endelea kukopa tu kama athari ya mafuta Duniani itazidi na kuwa endelevu!lazima tutumie tozo ambazo ni endelevu kuliko mikopo!

Deni la Taifa litapaa Sana KWA kutatua swala endelevu kama la mafuta lisilo tabirika.

Kama MKOPO ule wa IMF na Benki ya Dunia umeshaidhinishwa tuupeleke KWENYE mradi wa UMEME wa MTO RUFIJI.

Asanteni KWA kusoma
 
Serikali haina hizo hela za ziada... hizo tozo zilikuwa na matumizi tayari.
 
Serikali haina hizo hela za ziada... hizo tozo zilikuwa na matumizi tayari.
Mkuu
Utambue
Tozo zilikuwa za kujenga madarasa na vituo vya afya Lakini tukatumia fedha za uviko kujenga madarasa sasa tozo zitumike kushusha bei za mafuta!!
 
Mkuu
Utambue
Tozo zilikuwa za kujenga madarasa na vituo vya afya Lakini tukatumia fedha za uviko kujenga madarasa sasa tozo zitumike kushusha bei za mafuta!!
Ni kweli lakini serikali haijwahi kuwa na hela ya ziada, angalia hata utekelezaji wa bajeti, siku zote uko chini ya matarajio.
 
Back
Top Bottom